Kulipia Daraja la Nyerere Kigamboni

Kulipia Daraja la Nyerere Kigamboni

Smartbeing

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2014
Posts
323
Reaction score
425
Hivi hakuna namna serikali inaweza kufanya ili kuwapunguzia mzigo wananchi wa Kigamboni wanaolazimika kulipia daraja wavuke kwenda kwao on a daily basis?

Serikali inaweza kulipa deni hilo kwa NSSF kupitia kodi za wananchi maana madaraja mengine yamejengwa kwa kodi za wote. Yaani mlipa kodi Kigamboni amechangia ujenzi wa daraja la Mkapa na Busisi, kwanini walipakodi wa huko wasichangie la Kigamboni?

Alternatively, orodha ya wananchi wanaoishi Kigamboni wanaopita na magari ingejulikana halafu wangekuwa wanalipa kwa mwaka hata 100,000/= halafu wanaepuka usumbufu wa kulipia kila siku.

Kazi iendelee
 
Kwani kila kuvuka ni sh.ngapi? Kumbuka hayo mashirika ya serikali yana tengeneza hiyo miradi kwa ajili ya kupata faida so kama waliona huo mradi utawalipa waendelee tu kukusanya maduhuli.
 
Hivi hakuna namna serikali inaweza kufanya ili kuwapunguzia mzigo wananchi wa Kigamboni wanaolazimika kulipia daraja wavuke kwenda kwao on daily basis?

Serikali inaweza kulipa deni hilo kwa NSSF kupitia kodi za wananchi maana madaraja mengine yamejengwa kwa kodi za wote. Yaani mlipa kodi Kigamboni amechangia ujenzi wa daraja la Mkapa na Busisi, kwanini walipakodi wa huko wasichangie la Kigamboni?

Alternatively, orodha ya wananchi wanaoishi Kigamboni wanaopita na magari ingejulikana halafu wangekuwa wanalipa kwa mwaka hata 100,000/= halafu wanaepuka usumbufu wa kulipia kila siku.

Kazi iendelee
Umeandika point mkuu.niliwahi kuwaza,hivi hata lile daraja la Busis nalo litalipiwa,na hilo la cocobeach je? vipi kuhusu lile la Malagalasi kigoma,na kule ifakara je, na kule rufiji?mbona kule hawalipii?

Labda tufafanuliwe ni lini zile gharama zitakuwa zimeisha,je mpaka sasa ni shilingi ngapi zimeshapunguzwa kutoka kwenye deni la msingi hapo kwenye daraja la kigamboni?
 
Kwanini watozwe wananchi wakati daraja lenyewe limejengwa kwa kodi za wananchi....hai-make sense. Ina maana hapo wanalipa mara mbili....
Yanayotozwa ni magari, kama hutaki kulipa hiyo tozo, zungukia kongowe tu, utafanya tathimini mwenyewe mafuta ya kuzungukia kule, au kupitia darajani wapi ni gharama zaidi then, utaamua.
 
Hivi hakuna namna serikali inaweza kufanya ili kuwapunguzia mzigo wananchi wa Kigamboni wanaolazimika kulipia daraja wavuke kwenda kwao on daily basis?

Serikali inaweza kulipa deni hilo kwa NSSF kupitia kodi za wananchi maana madaraja mengine yamejengwa kwa kodi za wote. Yaani mlipa kodi Kigamboni amechangia ujenzi wa daraja la Mkapa na Busisi, kwanini walipakodi wa huko wasichangie la Kigamboni?

Alternatively, orodha ya wananchi wanaoishi Kigamboni wanaopita na magari ingejulikana halafu wangekuwa wanalipa kwa mwaka hata 100,000/= halafu wanaepuka usumbufu wa kulipia kila siku.

Kazi iendelee
Naunga mkono hoja serikali iilipe NSSF kupitia Kodi zetu.
 
Umeandika point mkuu.niliwahi kuwaza,hivi hata lile daraja la Busis nalo litalipiwa,na hilo la cocobeach je? vipi kuhusu lile la Malagalasi kigoma,na kule ifakara je, na kule rufiji?mbona kule hawalipii?

Labda tufafanuliwe ni lini zile gharama zitakuwa zimeisha,je mpaka sasa ni shilingi ngapi zimeshapunguzwa kutoka kwenye deni la msingi hapo kwenye daraja la kigamboni?
Busisi, selander sio ya kulipia.
 
Umeandika point mkuu.niliwahi kuwaza,hivi hata lile daraja la Busis nalo litalipiwa,na hilo la cocobeach je? vipi kuhusu lile la Malagalasi kigoma,na kule ifakara je, na kule rufiji?mbona kule hawalipii?

Labda tufafanuliwe ni lini zile gharama zitakuwa zimeisha,je mpaka sasa ni shilingi ngapi zimeshapunguzwa kutoka kwenye deni la msingi hapo kwenye daraja la kigamboni?
Lazima mtofautishe sio kila daraja lazima lilipiwe kuna miundombinu mingine ni ya lazima lakini sio ya muhimu, daraja la malagalasi ni la lazima, rufiji, kilombelo, ili watu wafike upande wa pili, huwezi watoza watu tozo, lakini haya ya kigamboni, coco beach hayo sio ya lazima, kwani hata yasipokuwepo watu upande wa pili wataweza kufika kwa kupitia njia nyingine, hivyo anayepita hapo anakuwa ameamua mwenyewe, kulipa hizo tozo..
 
Hivi hakuna namna serikali inaweza kufanya ili kuwapunguzia mzigo wananchi wa Kigamboni wanaolazimika kulipia daraja wavuke kwenda kwao on daily basis?

Serikali inaweza kulipa deni hilo kwa NSSF kupitia kodi za wananchi maana madaraja mengine yamejengwa kwa kodi za wote. Yaani mlipa kodi Kigamboni amechangia ujenzi wa daraja la Mkapa na Busisi, kwanini walipakodi wa huko wasichangie la Kigamboni?

Alternatively, orodha ya wananchi wanaoishi Kigamboni wanaopita na magari ingejulikana halafu wangekuwa wanalipa kwa mwaka hata 100,000/= halafu wanaepuka usumbufu wa kulipia kila siku.

Kazi iendelee
Mimi nashauri mapato yatokanayo na hili daraja asilimia ndogo iende kwenye halimashauri ya kigamboni isaidie kubora huduma za jamii.
 
Lazima mtofautishe sio kila daraja lazima lilipiwe kuna miundombinu mingine ni ya lazima lakini sio ya muhimu, daraja la malagalasi ni la lazima, rufiji, kilombelo, ili watu wafike upande wa pili, huwezi watoza watu tozo, lakini haya ya kigamboni, coco beach hayo sio ya lazima, kwani hata yasipokuwepo watu upande wa pili wataweza kufika kwa kupitia njia nyingine, hivyo anayepita hapo anakuwa ameamua mwenyewe, kulipa hizo tozo..
Hiyo ndiyo mipango kipumbavu zaidi,kwa nini hizo nguvu zisielekezwe kwenye mahitaji ya lazima? kila siku tunaona taarifa zinaonyesha watu huko maeneo ya vijini hawa mawasiliano na maeneo mengine kwa sababu ya kukatika vidaraja wakati wa mvua,mama zetu wanafia njiani wakati wa ujauzito, wengine wanashindwa kusafirisha mazao yao kutoka mashambani ili yatufikie huku mjini.
 
Inabidi tutofautishe miundo mbinu iliyogharimiwa 100% na serikali e.g Salender, busisi, Maragarasi n.k, hii kwakua serikali haifanyi biashara gharama zake ni bure, wewe tu na mafuta yako.

Iliyojengwa kwa ubia kati ya serikali na private entity(PPP) km hili daraja la kigamboni.
Uhusika wa serikali ktk miundo mbinu hii kunaifanya serikali kua na sauti hivyo kusaidia kupunguza gharama ingawa bado private entity itahitaji ku recover gharama zake na kupata faida..kununua deni km mnavyoshauri inategemea na mkataba wao km walikubaliana wataliendesha kwa miaka 30 or 100 inabidi muwe wapole, deni halinunuliki otherwise watumie ubabe.

Na iliyojengwa na private entity 100% km ile Bypass wanayojenga wachina kule nairobi kenya watakayoindesha kwa miaka 30. Kwakua hii ni 100% private hapa ht sauti ya serikali ktk kupanga bei ni ndogo ndio mana tunaskia kule gharama ni Ksh 300 sawa na buku 6 kupitisha gari, hii ingekua kwetu wapenda dezo tulio ktk uchumi wa kibepari ila mindset za ki communist nadhani tungeandamana kabisa.
 
Busisi, selander sio ya kulipia.

Hiyo ndiyo mipango kipumbavu zaidi,kwa nini hizo nguvu zisielekezwe kwenye mahitaji ya lazima? kila siku tunaona taarifa zinaonyesha watu huko maeneo ya vijini hawa mawasiliano na maeneo mengine kwa sababu ya kukatika vidaraja wakati wa mvua,mama zetu wanafia njiani wakati wa ujauzito, wengine wanashindwa kusafirisha mazao yao kutoka mashambani ili yatufikie huku mjini.
Unajua tena, wanasiasa!!wakati mwingine wana ubinafsi, kutokana na masilahi yao!!unajenga mradi badaye unakuja kuwa kero kwa uliowajengea
 
Back
Top Bottom