Kulinganisha usafi wa Njombe na Moshi au Iringa si sahihi

kisinja

JF-Expert Member
Sep 30, 2013
241
295
Kwa maoni yangu nadhani kitendo cha kulinganisha hali ya usafi kwa Manispaa ya Moshi au Manispaa ya Iringa kwa kulinganisha na Mji mdogo kama Njombe si sawa. Nadhani Njombe inapaswa kushindana na Miji yenye ngazi ya miji kama Tunduma, Makambako, Hai, Himo, Korogwe N.K. Kuiweka katika kundi la Manispaa kama Iringa, Moshi, au Dodoma si sawa sana.

Hailindani hata kwa miundo mbinu iliyoko, idadi ya watu, Kiwango cha maji safi na maji taka nk. Vinginevyo kama wizara imetumia kigezo cha kutopata mgonjwa wa kipindupindu pekee inaweza kuwa sawa kwa upande wao ili kutoa Motisha. Na kama ni hivyo dhana ya mashindano hayo na vigezo vyake basi vibadilike kidogo.

Otherwise Hongera sana Iringa kwa kushika nafasi ambayo mimi naweza kuiita ni nafasi ya kwanza kwa usafi kwa level ya Miji yenye hadhi kama yako.

Keep it up!!!!!!
 
Back
Top Bottom