Unazungumzia Dar ama mkoani?Nakupa gharama zangu, nimefyatua tofali 2400.
Kukodi mashine 50000/=
Fundi kila tofali kufyatua ni tsh. 150/=(tulivyoelewana) jumla ni 360,000/=
Mifuko ya cement ilikuwa 71 jumla yake 923000/=
Usafiri mifuko ya cement sh.50,000/=
Mchanga Lorry 8 kubwa jumla sh, 420,000/=
Gharama ya maji ilikuwa bure.
gharama zote ni kama sh.1,803,000/=
Kama ningeamua kununua moja moja, tofali 2400.
Kila tofali linauzwa sh.1000, hivyo jumla ingekuwa 2,400,000/=
Kubeba na kushusha kila tofali ni sh.200/= ingekuwa jumla ni 480,000/=
Usafiri wa tofali zote trip kama 8 hivi kila trip sh.50,000/= ingekuwa 400,000/=
Jumla gharama zote kununua ingekuwa 3,280,000/=
Hivyo kwa ujenzi wangu niliokoa kama kiasi cha sh.1,477,000/=Hela ya fundi kunijengea boma
Conclusion: gharama hizi inategemea location, ulinzi nk. piga mwenyewe hesabu lakini kufyatua mwenyewe ni nafuu, kwa vile unaponunua, hata anayekuuzia gharama zake ameingiza humo kwenye bei yake.
Asilimia kubwa ya wauza matofali siku hizi wanatoa huduma za usafiri na kushusha kwa kuchangia kiasi kidogo sana, hardly Tsh 100 mpaka 200 tu kwa tofali...Mkuu ni wapi hapo unachajiwa sh 1000' garama ya tofali pamoja na kulisafirisha mpaka kwako. Na wanazingatia umbali wa kiasi gani?
Ha ha..usawa unabana, tunapeana ushauri angalau vibanda vyetu visogee, mimi niliitafuta jamaa wanitengenezee, jamaa wakawa wanatoa tofali 45 badala ya 30 niliyowaambia,mifuko mingine wanapiga, then jamaa mwingine nikampa kazi ya kumwagilia kila siku mara 2..akawaanamwagilia mara 1 na mimi ananiambia mara 2 ile pesa ya maji anakula yeye.Acha roho mbaya mkuu.
Maeneo yote ya Kigamboni,Kibada,Tuangoma...wauza matofali wengi sana wala huitaji kwenda mbali sana.Mkuu ni wapi hapo unachajiwa sh 1000' garama ya tofali pamoja na kulisafirisha mpaka kwako. Na wanazingatia umbali wa kiasi gani?
DaimaUnazungumzia Dar ama mkoani?
Kama mkoani labda utanishawishi...
Ulitumia siku ngapi na hiyo mashine ukalipa 50,000 tu?
Je ni mashine ya mkono au vibrated?
Na je, kama ni mkono uimara wa tofali una uhakika nao kiasi gani?
Unaposema maji bure ulikuwa unachota mtoni? Na je mchotaji ni huyo huyo fundi au we mwnyewe?
Hakuna kisicho na gharama Boss.
Muda uliopoteza kusimamia unaweza kadiria Tsh ngapi?
Kwa Dar es salaam kufyatua tofali mwenyewe inaweza kuwa ni gharama kubwa kuliko haya ya kununua.
Binafsi nimefanya option zote hizi. Ila sitathubutu kufyatua mwenyewe tena. Maana ni presha na hasara sana nilipata.
Mapendo.
Na mimi nasubiri jibu tangu juzi. Hizi lorry 8 kubwa za mchanga ni lorry ninazozijua mimi au?Mkuu naomba nieleweshe hapo, lori kuba za mchanga 8sh 420.000, yaani 52500 kila moja au
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna kitu watu wanshindwa kuelewa gharama za material hazibadiliki isitoshe unapata kazi ya kulinda tofali tena na muda unaongezeka unaweza kuta hapo ulipo hauna miundo mbinu rafiki kufyatulia tofali bora kununuaTofali moja ni 1050 × 2400 ni 2,560,000/= kufyatua mwenyewe utakuja kugharamika zaidi mbeleni...
Gharama ya tofali it is nothing kwenye ujenzi wa nyumba usiingie risk ya kupiga tofali mwenyewe km huna muda na uzoefu
Mhandisi
Nashukuru sana mkuu, umenirahisishia na kupata sehemu ya kuanzia.
Mungu akupe hekima zaidi.
Paragraph ya mwisho, umemaliza kila kitu na ndio ukweliUnazungumzia Dar ama mkoani?
Kama mkoani labda utanishawishi...
Ulitumia siku ngapi na hiyo mashine ukalipa 50,000 tu?
Je ni mashine ya mkono au vibrated?
Na je, kama ni mkono uimara wa tofali una uhakika nao kiasi gani?
Unaposema maji bure ulikuwa unachota mtoni? Na je mchotaji ni huyo huyo fundi au we mwnyewe?
Hakuna kisicho na gharama Boss.
Muda uliopoteza kusimamia unaweza kadiria Tsh ngapi?
Kwa Dar es salaam kufyatua tofali mwenyewe inaweza kuwa ni gharama kubwa kuliko haya ya kununua.
Binafsi nimefanya option zote hizi. Ila sitathubutu kufyatua mwenyewe tena. Maana ni presha na hasara sana nilipata.
Mapendo.
Uzoefu wako mkuu muhinu kusikia.
Ipo Architect.vipi kuhusu ramani umeshapata kiongozi
kweli kabisa, wakamuungishe mzee yusuphAcheni roho mbaya nendeni mkanunue tofali na wengine wapate kula.