Mr Why
JF-Expert Member
- Nov 27, 2019
- 2,992
- 5,660
Ufafanuzi wa Mh Rostam Aziz kuhusiana na umiliki wa Migodi unadhihirisha kuwa Polepole ametengeneza uzushi wa kuchafua biashara za Mh Rostam Aziz na inaweza kumgharimu Polepole kwa kiasi kikubwa huko mbeleni kwasababu anazungumza kwa kuzusha bila kuwa na ushahidi kamili
Baadhi ya Watanzania waliotizama mahojiano ya Rostam Aziz wamepata ufafanuzi wa kina
Shutuma kuhusiana na migodi, Mh Rostam anasema kuwa migodi mikubwa ya Tanzania inamilikiwa na kampuzi za Kimataifa kwa miaka mingi na wakati huo Mh Rostam alikuwa akifanya ukandarasi katika baadhi ya kampuni hizi kwa muda mrefu
Hayati Magufuli akamuuliza Mh Rosta kwanini na yeye asijaribu kumiliki biashara za migodi badala ya kuwa mkandarasi wa kampuni za nje kwa muda mrefu ndipo Mh Rostam akapata wazo la kujaribu kumiliki
Mh Rostan hakununua share za Serikali kama anavyozushiwa na watu wenye chuki dhidi yake badala yake alikwenda kununua share za kampuni hizo za nje ya nchi ikiwemo Australia na Marekani kwasababu ndiko liliko chimbuko la Kampuni hizo na alinunua kwakufuata taratibu zote za uwekezaji wa Kimataifa
Mh Rostam anasema kuwa aliuziwa share nje ya nchi kama wageni wengine wa Kimataifa wanavyouziana share za kampuni hizi wakiwa nje ya nchi, na tofauti kubwa na wawekezaji wengine wa nje ya nchi ilikuwa asili yake ya Tanzania
Mh Rostam anasema kilichofanyika ni Kampuni hizi za Kimataifa ambazo zimekuwa zikimiliki migodi hii kwa muda mrefu kuamua kuuza share zao kwa wamiliki wapya lakini kwasababu alikuwa na uwezo wa kununua akafanikiwa kupata umiliki
Mh Rostam anasema kuwa badhi ya migodi mfano mgodi wa makaa ya mawe bado hajaanza kuchakata makaa ya mawe kwasababu mpaka sasa anaendelea kukamilisha taratibu za umiliki hivyobasi uzushi wa kuwa makaa ya mawe yanauzwa na Mh Rostam unafaa kupuuzwa
Kuhusu matumizi ya makaa ya mawe kutumika kuyeyusha vyuma kama baadhi ya Watanzania wanavyodai sio ya kweli kwasababu makaa yanayovunwa sasa yanakwenda kutumika kuendeshea viwanda nje ya nchi kwa mujibu wa maelezo ya Mh Rostam
Mh Rostam anasema kuwa anapokea shutuma mbaya kutoka kwa Watanzania wenye roho mbaya ikiweno Polepole kwasababu wana chuki juu ya yeye kufanikiwa kuwa na uwezo wa kufanya biashara kubwa ambazo Watanzania wamekuwa wakiamini hawawezi bali wageni ndio wenye uwezo huo peke yao
View: https://youtu.be/twTNb51Vu0A?si=-VQYuVidvVf8VTce
Baadhi ya Watanzania waliotizama mahojiano ya Rostam Aziz wamepata ufafanuzi wa kina
Shutuma kuhusiana na migodi, Mh Rostam anasema kuwa migodi mikubwa ya Tanzania inamilikiwa na kampuzi za Kimataifa kwa miaka mingi na wakati huo Mh Rostam alikuwa akifanya ukandarasi katika baadhi ya kampuni hizi kwa muda mrefu
Hayati Magufuli akamuuliza Mh Rosta kwanini na yeye asijaribu kumiliki biashara za migodi badala ya kuwa mkandarasi wa kampuni za nje kwa muda mrefu ndipo Mh Rostam akapata wazo la kujaribu kumiliki
Mh Rostan hakununua share za Serikali kama anavyozushiwa na watu wenye chuki dhidi yake badala yake alikwenda kununua share za kampuni hizo za nje ya nchi ikiwemo Australia na Marekani kwasababu ndiko liliko chimbuko la Kampuni hizo na alinunua kwakufuata taratibu zote za uwekezaji wa Kimataifa
Mh Rostam anasema kuwa aliuziwa share nje ya nchi kama wageni wengine wa Kimataifa wanavyouziana share za kampuni hizi wakiwa nje ya nchi, na tofauti kubwa na wawekezaji wengine wa nje ya nchi ilikuwa asili yake ya Tanzania
Mh Rostam anasema kilichofanyika ni Kampuni hizi za Kimataifa ambazo zimekuwa zikimiliki migodi hii kwa muda mrefu kuamua kuuza share zao kwa wamiliki wapya lakini kwasababu alikuwa na uwezo wa kununua akafanikiwa kupata umiliki
Mh Rostam anasema kuwa badhi ya migodi mfano mgodi wa makaa ya mawe bado hajaanza kuchakata makaa ya mawe kwasababu mpaka sasa anaendelea kukamilisha taratibu za umiliki hivyobasi uzushi wa kuwa makaa ya mawe yanauzwa na Mh Rostam unafaa kupuuzwa
Kuhusu matumizi ya makaa ya mawe kutumika kuyeyusha vyuma kama baadhi ya Watanzania wanavyodai sio ya kweli kwasababu makaa yanayovunwa sasa yanakwenda kutumika kuendeshea viwanda nje ya nchi kwa mujibu wa maelezo ya Mh Rostam
Mh Rostam anasema kuwa anapokea shutuma mbaya kutoka kwa Watanzania wenye roho mbaya ikiweno Polepole kwasababu wana chuki juu ya yeye kufanikiwa kuwa na uwezo wa kufanya biashara kubwa ambazo Watanzania wamekuwa wakiamini hawawezi bali wageni ndio wenye uwezo huo peke yao
View: https://youtu.be/twTNb51Vu0A?si=-VQYuVidvVf8VTce