Mshiiri
JF-Expert Member
- Jun 16, 2008
- 2,012
- 516
Inavyoonekana chama tawala kimeamua kutengeneza mazingira ya kupoteza imani na wananchi kwa kuona kwamba wanahitaji mabadiliko na wao wameshindwa kuwapa watanzania sasa wanatumia njia za matisho na kejeli na kujitoa ufahamu hata kwa wale wenye weledi wa sheria alimradi wapate fursa ya kutenda mambo yao ya kishenzi ambayo wameyatenda tangu kuanzishwa kwa vyama vingi nchini - udikteta.
Kulinda kura ni haki ya msingi ya raia kama ilivyo kujilinda wenyewe kwa kuwa hata dola zinatenda kusaidia chama tawala - aibu sana.
Sasa mimi pengine ningekuwa na wazo wananchi tuzuie access kwa watu wasiohusika kwenda eneo la kupiga kura ama kupeleka maboksi, ama hot pots, ama mabegi ya fedha, ama kupitisha gari lenye maboksi, ama mtu yeyote tutakayemtilia shaka na ikiwa lile siyo eneo lake la uchaguzi asipewe fursa kwenda eneo la kupiga kura kwa njia yeyote ile hadi matokeo yatoke.
Hii ni haki ya msingi na acha wao chama tawala waongelee kuhusu mita mia mbili (200), sisi tutaongelea kuhusu access ya majizi ya kura. Hapa bado tutakuwa tumelinda kura zetu
Nawakilisha
Kulinda kura ni haki ya msingi ya raia kama ilivyo kujilinda wenyewe kwa kuwa hata dola zinatenda kusaidia chama tawala - aibu sana.
Sasa mimi pengine ningekuwa na wazo wananchi tuzuie access kwa watu wasiohusika kwenda eneo la kupiga kura ama kupeleka maboksi, ama hot pots, ama mabegi ya fedha, ama kupitisha gari lenye maboksi, ama mtu yeyote tutakayemtilia shaka na ikiwa lile siyo eneo lake la uchaguzi asipewe fursa kwenda eneo la kupiga kura kwa njia yeyote ile hadi matokeo yatoke.
Hii ni haki ya msingi na acha wao chama tawala waongelee kuhusu mita mia mbili (200), sisi tutaongelea kuhusu access ya majizi ya kura. Hapa bado tutakuwa tumelinda kura zetu
Nawakilisha