Ndagullachrles
Senior Member
- Jun 20, 2023
- 198
- 209
Niliwahi kuandika juu ya jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro kukamata basi la kampuni ya Extra Luxury Coach likiwa na shehena ya dawa za kulevya iana ya mirungi ikisafrishwa kutoka mkoani Arusha kwenda Jijini Dar es salaam mwaka 2023.
Basi hilo T643DVL, lilikamatwa eneo la majengo mapya wilaya ya Same baada ya askari wa usalama barabarani kulifanyia ukaguzi na kukutana na shehena hiyo, sijui polisi walimalizana vipi na wamiiliki wa basi hilo maana hatukuwahi kusikia tena habari zake,(soma habari hiyo hapo chini.
Kwa mara nyingine tena mabasi ya kampuni hiyo wamewasotesha abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Arusha kwenda Dar es salaam bila kuwapatia usafiri ndani ya wakati kwa mujibu wa taratibu baada ya basi lao kudaiwa kuharibika wilayani same mkoani Kilimanjaro .
Mkasa huo umewakumba abiria hao April 29 mwaka huu baada ya kukaa tangu saa moja jioni hadi kesho yake kwa maana ya April 30 kabla ya kufaulishwa kwenye basi la Kampuni ya Esther Luxury Coach.
Kabla ya mkasa huo, basi hilo lilikamatwa wilayani mwanga likidaiwa kusafrisha nyara za seikali lakini haijulikani jambo hilo liliishaje kutoka kwa maofisa wa maliasili na utalii waliofika eneo hilo na kufanya upekuzi kwenye basi hilo na kisha mzigo huo kuruhusiwa kuendelea na safari.
Mbali na hilo,abiria hao wanadaiwa kutozwa nauli ya sh,50,000 kutoka Arusha kwenda Dar es salaam kwa basi lenye choo ndani lakini matokeo yake wakapakizwa kwenye basi lisilokuwa na choo cha ndani,
Abiria mmoja alituma ujumbe kwa maofisa wa LATRA na hapa nautuma kama ulivyo.
"Hii basi ni ya kufungiwa,T791DXM ,tumekata tiket ya Luxury Bus yenye choo ndani na online inaonekana ni Extra Luxury Coach lakini si kweli,tumepakiwa kwenye basi halina choo,pia basi ilikuwa liondoke saa 12 lakini limechelewa sana kuondoka Arusha"
"Tumefika Himo tumekamatwa mpaka sasa basi limebeba nyara za serikali ,abiria tunateseka bila sababu ya msingi na tofauti ya basi la Luxury na ambalo si Luxury,pesa hatujarudishiwa,naomba hili ulifuatilie tafadhali"
"Tumefika Same basi tena limesimama,abira hatuna taarifa yoyote tumewekwq tu hapa".
"Mkuu hili basi abiria wamefaulishwa same muda huu ndo wanaondoka tangu jana saa moja jioni gari lilikwama Same na Trafiki naona wameliachia".
"Imagine abiria ambaye saa hizi alitakiwa kuwa amefika Dar ndo kwanza yupo Same",anamalizia abira huyo kwa kuhoji.
Mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni hiyo aliyefahamika kwa jina la Massawe pamoja na kukiiri kutokea kwa mkasa huo anadai abiria waliendelea na safari baada ya kupatiwa usafri mwingine lakini pia akadai abiria walirejehsewa nauli zao kwa wale waliokata tiketi za sh,50,000 kwa basi lenye choo ndani .
SOMA HII YA MIRUNGI > Basi la Extra Luxury limekamatwa na mirungi 55kg
Basi hilo T643DVL, lilikamatwa eneo la majengo mapya wilaya ya Same baada ya askari wa usalama barabarani kulifanyia ukaguzi na kukutana na shehena hiyo, sijui polisi walimalizana vipi na wamiiliki wa basi hilo maana hatukuwahi kusikia tena habari zake,(soma habari hiyo hapo chini.
Kwa mara nyingine tena mabasi ya kampuni hiyo wamewasotesha abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Arusha kwenda Dar es salaam bila kuwapatia usafiri ndani ya wakati kwa mujibu wa taratibu baada ya basi lao kudaiwa kuharibika wilayani same mkoani Kilimanjaro .
Mkasa huo umewakumba abiria hao April 29 mwaka huu baada ya kukaa tangu saa moja jioni hadi kesho yake kwa maana ya April 30 kabla ya kufaulishwa kwenye basi la Kampuni ya Esther Luxury Coach.
Kabla ya mkasa huo, basi hilo lilikamatwa wilayani mwanga likidaiwa kusafrisha nyara za seikali lakini haijulikani jambo hilo liliishaje kutoka kwa maofisa wa maliasili na utalii waliofika eneo hilo na kufanya upekuzi kwenye basi hilo na kisha mzigo huo kuruhusiwa kuendelea na safari.
Mbali na hilo,abiria hao wanadaiwa kutozwa nauli ya sh,50,000 kutoka Arusha kwenda Dar es salaam kwa basi lenye choo ndani lakini matokeo yake wakapakizwa kwenye basi lisilokuwa na choo cha ndani,
Abiria mmoja alituma ujumbe kwa maofisa wa LATRA na hapa nautuma kama ulivyo.
"Hii basi ni ya kufungiwa,T791DXM ,tumekata tiket ya Luxury Bus yenye choo ndani na online inaonekana ni Extra Luxury Coach lakini si kweli,tumepakiwa kwenye basi halina choo,pia basi ilikuwa liondoke saa 12 lakini limechelewa sana kuondoka Arusha"
"Tumefika Himo tumekamatwa mpaka sasa basi limebeba nyara za serikali ,abiria tunateseka bila sababu ya msingi na tofauti ya basi la Luxury na ambalo si Luxury,pesa hatujarudishiwa,naomba hili ulifuatilie tafadhali"
"Tumefika Same basi tena limesimama,abira hatuna taarifa yoyote tumewekwq tu hapa".
"Mkuu hili basi abiria wamefaulishwa same muda huu ndo wanaondoka tangu jana saa moja jioni gari lilikwama Same na Trafiki naona wameliachia".
"Imagine abiria ambaye saa hizi alitakiwa kuwa amefika Dar ndo kwanza yupo Same",anamalizia abira huyo kwa kuhoji.
Mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni hiyo aliyefahamika kwa jina la Massawe pamoja na kukiiri kutokea kwa mkasa huo anadai abiria waliendelea na safari baada ya kupatiwa usafri mwingine lakini pia akadai abiria walirejehsewa nauli zao kwa wale waliokata tiketi za sh,50,000 kwa basi lenye choo ndani .
SOMA HII YA MIRUNGI > Basi la Extra Luxury limekamatwa na mirungi 55kg