Kukopesha kwenye biashara

Kukopesha kwenye biashara

Kukopesha ni moja kati ya msingi muhimu kwenye biashara, kwani humtengenezea Imani mteja ya kuwa we ndo mtu sahihi kufanya nae biashara kwani utamhudumia hata akiwa hana pesa

Lakini pia ni chanzo Cha kushuka kibiashara( cause sometimes sio wote wanaolipa), kupoteza wateja pindi unapowadai, na muda mwingine hupelekea uhasama kati muuzaji na mnunuzi

Jambo la muhimu ni kujua mteja gani sahihi kwa kukopeshwa na yupi si sahihi kwa mkopo, ili kuepukana na usumbufu usio wa lazima
 
Kopesha wote ila mwanamke usimkopeshe, hata akitoa machozi ya damu.
Cha kufanya wewe mpe tu kama msaada. Anaweza asilipe au asilpe kabisa.
Jamani
 
Kukopesha ni moja kati ya msingi muhimu kwenye biashara, kwani humtengenezea Imani mteja ya kuwa we ndo mtu sahihi kufanya nae biashara kwani utamhudumia hata akiwa hana pesa
Umetisha mkuu
 
Kwenye biashara yangu mm sikopeshi. Maana nimeona kukopesha ni kujitengenezea maadui tu.
 
Kwa wafanyabiashara wote, je unaweza fanya bihashara bila kukopesha? Bihashara yoyote ile iwe kubwa au ndogo.

Je, ni zipi faida za kukopesha na zipi hasara za kukopesha kwenye bihashara?

Welcome
Inategemea na aina ya biashara.. Mfano BIASHARA YA DAWA ZA BINADAMU. Unamkopesha mgonjwa akipona hakulipi
 
Nakuasa, punguza mikopo hasa kwa biashara changa.

wengine tukishakopa tunahama mtaa kabisaa
 
Kopesha wote ila mwanamke usimkopeshe, hata akitoa machozi ya damu. Cha kufanya wewe mpe tu kama msaada. Anaweza asilipe au asilpe kabisa.
duuu ungejua mtu ambaye ni mlipaji mzuri ni mwanamke usingesema hivi aiseee daaah
 
Fanya biashara lakini usikopeshe ata mia, wakopaji ni wazuri wakati wakiwa na shida wakishakopa utajua hujui.
 
Biashara zote kubwa zinakopesha kwa nini wewe mwenye mtaji mdogo unaogopa kukopesha?; wazabuni wote wanaofanya kazi na serikali wanakopesha, iwe ujenzi au kupeleka vifaa n.k Muhimu ni kumtathmini mteja wako kama anauwezo wakuja kulipa
 
Back
Top Bottom