apolycaripto
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 644
- 225
Ufuasi wa siasa katika vyama hujengwa katika misingi ya itikadi. Swali la kujiuliza ni Je, wanaojiuzulu kwa kumuunga mkono rais kisha wanaenda kuchukua kadi za chama (ambacho kinaongozwa katika misingi ya itikadi) ni sahihi?
Hivi huyu Rais atakapomaliza muda wake, hawa watu watamuunga mkono nani?
Nakiona chama A kinaelekea kufanya makosa yaleyale ambayo yanakisumbua chama B.
Kwa sisi ambao tumekuwa tukipambana chama A, tunaposhindwa katika kura za maoni, imekuwa rahisi sana kushawishiwa kwamba ingia chama B utapita kwa urahisi. Kweli matokeo chanya tumeyaona lakini kwa upepo huo huo chama B kinapukutika. Hivi hii haiwezi kuleta mpasuko kwa chama A katika nyakati za usoni?
Ni dhahiri kuwa wimbi hili la sasa limechagizwa na ahadi za vyeo, kupewa fursa ya kutetea nafasi ile ile. Vipi mambo yakiwa tofauti?
Naziona nyakati mbaya za chama A kwa siku za usoni kama chama B kinavyotaabika sasa.
Siasa ni sayansi, through experiment we can get a better solution.
Hivi huyu Rais atakapomaliza muda wake, hawa watu watamuunga mkono nani?
Nakiona chama A kinaelekea kufanya makosa yaleyale ambayo yanakisumbua chama B.
Kwa sisi ambao tumekuwa tukipambana chama A, tunaposhindwa katika kura za maoni, imekuwa rahisi sana kushawishiwa kwamba ingia chama B utapita kwa urahisi. Kweli matokeo chanya tumeyaona lakini kwa upepo huo huo chama B kinapukutika. Hivi hii haiwezi kuleta mpasuko kwa chama A katika nyakati za usoni?
Ni dhahiri kuwa wimbi hili la sasa limechagizwa na ahadi za vyeo, kupewa fursa ya kutetea nafasi ile ile. Vipi mambo yakiwa tofauti?
Naziona nyakati mbaya za chama A kwa siku za usoni kama chama B kinavyotaabika sasa.
Siasa ni sayansi, through experiment we can get a better solution.