Ndugu yangu, huyo kijana namuona kama kijana wangu.. shule za serikali hazina gharama na nyingi ni za bweni! Chakula na malazi atapewa hapo hapo shuleni.. shule zingine zinamilikiwa na taasisi za kidini na nyingi wanatoa ufadhili wao wenyewe hivyo wewe utawajibika kuchangia gharama za kawaida sana. Kumbuka huyu anahaki ya kupata elimu kama watoto wengine hivyo lengo lako lisiishie tu kurahisisha mawasiliano kati yako wewe na yeye bali uende mbali zaidi ili tumtengenezee mtoto mazingira ya kujitegemea