katika maisha yetu ya kila siku ni rahisi sana kuona madhaifu ya wenzetu,huku tukiamini kuwa sisi tuko salama.ubaya unakuja pale tu mabaya yetu yanapoanikwa live kwa wengine.tunajiona kama tumedhalilishwa na hivyo ili kujifariji tunajaribu kujisafisha kwa kila namna ili kuupinga ukweli,badala ya kuchukua jitihada za kujifunza kuishi vizuri na watu, tunapoteza muda mwingi kulumbana na watu na kuendekeza chuki kwa vile tu fulani kaweka mambo yangu hadharani.hakuna mkamilifu,ila wajanja wa maisha ni wale walio tayari kujifunza kila siku ili kwamba wawe kielelezo kwa wengine wanaomtazama.hatutakiwi kuwa waoga wa kufanya makosa au kukosolewa bali tunapaswa kuwa jasiri wa kukubali ukweli na kuanza na pale tulipo haribu.