Kujielewa 101: Usitafute pongezi wala kusifiwa, ukisifiwa au kupongezwa usishukuru

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,243
12,769
Moja ya mambo yaliyowaingiza wanadamu wengi matatizoni ni kutafuta pongezi na sifa. Moja ya mambo yaliyopelekea watu kutapeliwa, kudhuriwa, kupta hasara na kuwa-taken advantage of ni kusifiwa na kupongezwa.

Asilimia kubwa ya pongezi na sifa unazopewa ni za kinafiki, ni za watu wanaotaka kitu kutoka kwako. Pongezi na sifa huwa ni katika kukulainisha. Epuka sana kufuatilia pongezi na sifa.

Jenga ukuta kuzuia pongezi na sifa. Jenga akili yako isijali pongezi na sifa. Njia moja ni kukumbuka kutoshukuru mtu akikupongeza au akikusifia, hilo litamdiscourage asiendelee na mpango wake wa kukulainisha.

Njia ya pili ni kuacha kutafutiza kupongezwa na kusifiwa, kwa jinsi gani? Acha kuelezea mafanikio na mipango yako kwa watu. Acha habari za mwanangu hivi, kazi yangu vile, biashara yangu hivi, mke wangu vile, mume wangu kalikwenda kakarudi nk nk.

Ukiacha kujali na kufuatilia kusifiwa na pongezi utaishi maisha huru sana.
 
Ukiweza kukwepa mambo haya matatu basi maisa yako yatakua vyema sana. Dunia imechafuka kwasababu watu wameshindwa kuyakontrol mambo haya.
  1. Tamaa ya Pesa
  2. Tamaa Uongozi/Madarak
  3. Tamaa ya Umaarufu na Sifa
Mkuu sidhani kama haya ni matatizo ila ni matokeo ya matatizo mengine(primary source)
 
Ila kubwa kuliko ukiona unasifiwa sifiwa na wanawake jua huo ni mtego mwaisa sio muda unapigwa.
 
kuna na wale ambao waliamua kuanzisha chama kabisa cha machawa na hii yooote ni kule kule tu ujuha ujinga kpuuzi kujipendekeza akili ndogo etc etc , kiujumla watu wanaacha kutafuta maisha wanakuwa wajinga wajinga , kwa weli waafrika wengi hatutumii akili zetu ipasavyo.
 
Ukiweza kukwepa mambo haya matatu basi maisa yako yatakua vyema sana. Dunia imechafuka kwasababu watu wameshindwa kuyakontrol mambo haya.
  1. Tamaa ya Pesa
  2. Tamaa Uongozi/Madarak
  3. Tamaa ya Umaarufu na Sifa
Everyone of us must choose one of these two:
1. The pain of discipline.
2. The pain of regret.

Number 1 or Number 2 Sir?
 
Moja ya mambo yaliyowaingiza wanadamu wengi matatizoni ni kutafuta pongezi na sifa. Moja ya mambo yaliyopelekea watu kutapeliwa, kudhuriwa, kupta hasara na kuwa-taken advantage of ni kusifiwa na kupongezwa.

Asilimia kubwa ya pongezi na sifa unazopewa ni za kinafiki, ni za watu wanaotaka kitu kutoka kwako. Pongezi na sifa huwa ni katika kukulainisha. Epuka sana kufuatilia pongezi na sifa.

Jenga ukuta kuzuia pongezi na sifa. Jenga akili yako isijali pongezi na sifa. Njia moja ni kukumbuka kutoshukuru mtu akikupongeza au akikusifia, hilo litamdiscourage asiendelee na mpango wake wa kukulainisha.

Njia ya pili ni kuacha kutafutiza kupongezwa na kusifiwa, kwa jinsi gani? Acha kuelezea mafanikio na mipango yako kwa watu. Acha habari za mwanangu hivi, kazi yangu vile, biashara yangu hivi, mke wangu vile, mume wangu kalikwenda kakarudi nk nk.

Ukiacha kujali na kufuatilia kusifiwa na pongezi utaishi maisha huru sana.

Jamaa katoa kitu
Sema KITU!
Asee wana JF njooni mezani
Msipotee
 
Kwetu tuna msemo unasema Sifa zinaua...
Ila pia Kanisani tunasema Mungu Wetu anapenda Sifa, ndo maana kuna SAA huwa tunaimba nyimbo za Sifa! Sasa unanichanganya hapa...

Wale wazee wa inspiration utasikia wanasema ili uweze kutoboa...share mipango yako itakufanya uisimamie na ku inspire wengine.
Kazi ipoo
 
Kwetu tuna msemo unasema Sifa zinaua...
Ila pia Kanisani tunasema Mungu Wetu anapenda Sifa, ndo maana kuna SAA huwa tunaimba nyimbo za Sifa! Sasa unanichanganya hapa...

Wale wazee wa inspiration utasikia wanasema ili uweze kutoboa...share mipango yako itakufanya uisimamie na ku inspire wengine.
Kazi ipoo
Ni kweli....wazungu na watu walioendelea hawanaga shida kushare vitu wanavyofanya...kwa sababu anaamini anachokifanya...

Sisi hatujiamini na hatuamini tunachokifanya...so tunaona kufichaficha ndo solution...kumbe kuexpose inaweza kuwa ni msaada kwako pia katika kuimprove hicho kitu...

Duniani hatuishi peke yetu...
Imagine mtu unajua coding au una skills flan...usishare na wenzako capabilities kisa unaogopa utaonekana una majivuno?



Tusiangalie negative tu....
 
Back
Top Bottom