Kuhusu woga/hofu

Kuhusu woga/hofu

PERECY

Member
Joined
Jan 11, 2012
Posts
29
Reaction score
16
WanaJF,

Tarehe 3 Januari 2009 niliandika katika Diary yangu kuhusu woga nikiwanukuu watu mashuhuri, na hapo ndipo ninapotaka kusema kwa dhati kwamba wapambanaji wote woga/hofu iwe mwiko. Hatima ya nchi yetu haihitaji mzaha, vijembe, watu wanatakiwa kuleta mabadiliko kwa ustawi wa maendelao yao:-

  1. Aung San Suu Kyi: Mshindo wa Nobel na mtetezi wa haki za binadamu - Burma (Myanmar): " WOGA SI TABIA ASILIA YA WATU WASTAARABU".
  2. Dorothy Thompson - Mwandishi wa Kimarekani, Mpinzani wa Ufashisti wa Adolf Hitler - 1930: "UHAI WA BINADAMU HUANZA KUCHIPUA PALE TU ANAPOUSHINDA WOGA".

  • "Hakuna kitu kinachoharibu akili yetu kama woga, kwamba silaha ya watu woga ni mabavu na ubabe, kwamba penye ukweli hakuna woga."
  • Kwamba wanaoendekeza woga ni wale tu ambao hukataa ukweli na hawafanyi uchambuzi wa kina kuhusu chimbuko la matatizo na matukio yanayowasumbua; na,
  • Kwamba woga huongezeka tunapokuwa gizani, na njia pekee ya KUUFUKUZA NI KUWASHA TAA!"

Mwingine ni:
  1. Waswidi: "Hofu hufanya jambo doogo kuba na kivuli kikubwa.
  2. William Allen White, Mwandishi mashuhuri na jasiri - Mmarekani: " Siogopi yatakayotokea kesho kwa sababu nimeyaona ya jana, na ninaipenda leo".

Watanzania, TUTAFAKARI!
 
Mkuu watanzania tunatakiwa tuige watu wa mataifa ya Misri,Libya,Tunisia na kwingineko vinginevyo huyu mkoloni mweusi atatuangamiza sisi na vizazi vyetu.
 
Back
Top Bottom