Kuhusu kanzidata (database) ya Sekretarieti ya Ajira

Kuhusu kanzidata (database) ya Sekretarieti ya Ajira

Mbishi 4 real

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2014
Posts
640
Reaction score
655
Kwanza napenda kuipongeza sekretarieti ya ajira kwa kuwasaidia vijana ( watoto wa wakulima ) kupata ajira serikalini sababu bila ya nyinyi hali ingekua ngumu sana kwa sisi walalahoi kupata ajira serikalini.Nasema hivyo kwasababu taasisi nyingi za serikalini zimejaa undugu kiasi kwamba huwezi kupata kazi bila ya kuwa na mtu unaemfahamu katika taasisi unayotaka kuomba kazi.

Sekretarieti ya ajira imekua na utaratibu wa kuendesha usaili kwa kada mbalimbali na wanaofaulu hupangiwa vituo vya kazi.Kwakua nafasi zinakua finyu wale ambao wamefaulu lakini hawakupangiwa vituo vya kazi majina yao huifadhiwa kwenye kanzidata (database) kama majina ya reserves(akiba).

Kitu ambacho nadhani wanachotakiwa kufanya ni kuweka hadharani majina ya waliopangiwa vituo vya kazi na vilevile waweke wazi majina ya wale ambao wameingia kwenye database ili nao wawe na matumaini flani hata kama ikitokea sio wote watakaopata nafasi lakini angalau wajue kwamba ni wangapi wameingia kwenye database.

Kwakumalizia napenda kuwapongeza kwa kuwasaidia watoto wa wakulima ambao hawana wa kuwashika mkono katika mchakato mzima wa kupata ajira serikalini.

Asante.
 
Kk unachokizungumza ni sahihi waweke majina ya reserve at least tujue kua anymoment the chance happened unajitwika zigo la ajira kwakweli
 
Mibinafsi hata celewi maaana interview mbili mpk oral lkn cjawah ona jina langu baada ya oral ss sielewi nimefauluuu au?
 
Mibinafsi hata celewi maaana interview mbili mpk oral lkn cjawah ona jina langu baada ya oral ss sielewi nimefauluuu au?

Shida ni kwamba hawaweki hadharani majina yaliyopo kwenye database,waweke hadharani ili wahanga wa ajira waweze kujijua kama wapo kwenye database au la.
 
Hizo ajira balaa!, nimeitwa mara nane na nmehudhuria mara moja nikafika mpaka oral nikajua nitapata kwa jinsi nilivyokuwa nime perfom vizuri. Sikuitwa na sijarudia tena kuhudhuria huko japo naendelea ku apply huko. Wenye bahati zenu endeleeni mm nipo upande wa pili huku
 
Kwanza napenda kuipongeza sekretarieti ya ajira kwa kuwasaidia vijana ( watoto wa wakulima ) kupata ajira serikalini sababu bila ya nyinyi hali ingekua ngumu sana kwa sisi walalahoi kupata ajira serikalini.Nasema hivyo kwasababu taasisi nyingi za serikalini zimejaa undugu kiasi kwamba huwezi kupata kazi bila ya kuwa na mtu unaemfahamu katika taasisi unayotaka kuomba kazi.

Sekretarieti ya ajira imekua na utaratibu wa kuendesha usaili kwa kada mbalimbali na wanaofaulu hupangiwa vituo vya kazi.Kwakua nafasi zinakua finyu wale ambao wamefaulu lakini hawakupangiwa vituo vya kazi majina yao huifadhiwa kwenye kanzidata (database) kama majina ya reserves(akiba).

Kitu ambacho nadhani wanachotakiwa kufanya ni kuweka hadharani majina ya waliopangiwa vituo vya kazi na vilevile waweke wazi majina ya wale ambao wameingia kwenye database ili nao wawe na matumaini flani hata kama ikitokea sio wote watakaopata nafasi lakini angalau wajue kwamba ni wangapi wameingia kwenye database.

Kwakumalizia napenda kuwapongeza kwa kuwasaidia watoto wa wakulima ambao hawana wa kuwashika mkono katika mchakato mzima wa kupata ajira serikalini.

Asante.

Ni kweliii kabisaa@mbishi 4 real
 
Hizo ajira balaa!, nimeitwa mara nane na nmehudhuria mara moja nikafika mpaka oral nikajua nitapata kwa jinsi nilivyokuwa nime perfom vizuri. Sikuitwa na sijarudia tena kuhudhuria huko japo naendelea ku apply huko. Wenye bahati zenu endeleeni mm nipo upande wa pili huku

Kuna moja ya Tantrade nilikisha siku 4 mfululizo nakumbuka nilikuwa the best..

Baada ya oral, sijui ilikuwaje ase..
Kwanza wanasema Tantrade walipeleka watu wao badala ya watu waliokuwapo kwenye mchakato
 
Mm nakuunga mkono mleta uzi ase, ifikie hatua ili tujilidhishe kuwa mchakato huko wazi basi watoe orodha ya watu waliobaki kwenye kanzidata..

Ila pia mm nashauri hata maksi za oral ziwekwe hadharan, tufahamu uwezo wetu pia, ili tuweze kujisahihisha wenyewe kuwa tunakosea wap
 
Mkuu kwa uzoefu nlioupata utaratibu wa hawa jamaa ni kuwa wa
1. Sekretarieti ya ajira huwa wanashortlist kupitia written interview. 2. Ukifanikiwa oral interview jukumu linakuwa chini ya taasisi husika wao ndio wanaratibu the process,ila who is the best maamuzi yanabaki kwa a taasisi husika.
3. Kanzi data inatunzwa na taasisi husika kwa kushirikiana na sekretarieti. Hivyo ikiwa ni taasisi kubwa majina watatoa wao toka kwenye kanzidata yao. Mimi nliwahi kuhudhuria moja..wakati wa oral nikaona wote ni toka taasisi hiyo isipokuwa mmoja tu ndo alitoka sekrrtarieti.
Kwa ujumla jamaa wako fair sana.,hivyo tusikate tamaa na tufanye maandalizi ya nguvu tukibahatika kuitwa kwenye usaili. Inawezekana siku moja ikawa yako.
 
jaman tunapenda kulalamika sana...wakitoa majina yaliyopo kwenye database halafu usipoitwa utaanza kulalamika....xo hatuhitaji kuyajua na lengo letu ni kupata ajira husika na sio kuingia kwenye database...kuingia kwenye database ni huruma yao tu..na inapotokea kuna shirika linataka mtu na halitaki gharama za interview ndo linachukua mtu kwenye database kama yupo..basi wafanye ukishindwa umeshindwa tu....maana tunalalamika....mbona hatulaumu na private waweke database
 
Watoe majibu ndiyomaana ya intervie, sasa tutajuaje, kuna watu wanatika mikoa mbalimbali halafu unafanya interview hawakupi jibu
 
jaman tunapenda kulalamika sana...wakitoa majina yaliyopo kwenye database halafu usipoitwa utaanza kulalamika....xo hatuhitaji kuyajua na lengo letu ni kupata ajira husika na sio kuingia kwenye database...kuingia kwenye database ni huruma yao tu..na inapotokea kuna shirika linataka mtu na halitaki gharama za interview ndo linachukua mtu kwenye database kama yupo..basi wafanye ukishindwa umeshindwa tu....maana tunalalamika....mbona hatulaumu na private waweke database
 
Hizo ajira balaa!, nimeitwa mara nane na nmehudhuria mara moja nikafika mpaka oral nikajua nitapata kwa jinsi nilivyokuwa nime perfom vizuri. Sikuitwa na sijarudia tena kuhudhuria huko japo naendelea ku apply huko. Wenye bahati zenu endeleeni mm nipo upande wa pili huku
Kaka kwanza pole kwa unayopitia ila naomba nikutie moyo endelea kupambana usikate tamaa na naongea aya coz nina ushuuda mm mwenyewe nilifanya written pia nikafaulu nikaitwa oral lakini nafasi husika nilizofanyia pepa wala sijapata na nilijua wakat natoka kwenye interview ya oral lazima nipate nafasi yangu ila mungu si athumani sikukata tamaa kabisa juzi tu nimeona jina langu kwenye portal ya utumishi so pambana usiache kumuomba mungu kila la kheri ndugu
 
Na kwanini huwa Kuna ukomo wakuweka watu kwenye hii data base
 
Kaka kwanza pole kwa unayopitia ila naomba nikutie moyo endelea kupambana usikate tamaa na naongea aya coz nina ushuuda mm mwenyewe nilifanya written pia nikafaulu nikaitwa oral lakini nafasi husika nilizofanyia pepa wala sijapata na nilijua wakat natoka kwenye interview ya oral lazima nipate nafasi yangu ila mungu si athumani sikukata tamaa kabisa juzi tu nimeona jina langu kwenye portal ya utumishi so pambana usiache kumuomba mungu kila la kheri ndugu
Interview ulifanya lini na jina limetoka lini kwenye tangazo la ajira?
 
Back
Top Bottom