Kuhamisha pesa kutoka M-Pesa - CRDB

Kuhamisha pesa kutoka M-Pesa - CRDB

G_Carson

Member
Joined
Dec 23, 2017
Posts
15
Reaction score
13
Habari nilitakiwa nilipe TRA kupitia account yao ya CRDB, Kwa Bahati mbaya nikatuma direct kupitia simu yangu,na kumbe nilitakiwa nikalipe moja kwa moja CRDB BANK.

Niliporudi kwa watu wa TRA wakanambia hiyoo hela uliyolipa kupitia simu yako ya mkononi direct ndio imeshapotea hiyoo,,kalipe bank hela nyingine.

Msaada,

Hivi hiyo ni sahihi kweli? Kwamba ukikosea hela ikaenda TRA kwa makosa,hyo pesa hairudi tena na kama hairudi ni haki kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wasikuetee utani na pesa,,,,,nenda vodacom makao makuu chukua statement ya iyo transaction zen nenda police kitengo cha wizi wa mitandaoni ndo utapata majibu yaliyo nyooka...kama pesa kutoka voda sio pesa halali ila kutoka crdb ndo pesa halali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Malipo ya serikali yote yanatumia payment gateway moja tu inayokupa control number ya kulipia haijalishi umelipia kwa simu au bank gani lazma muamala usome kwa mfumo wa malipo.

Nimeprint zaidi ya mara 1 ile form ya malipo ya TRA nkajaza nalipia kwa CRDB ila wakala akalipia kwa NMB na malipo yakapokelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mfumo wa malipo ya serikali kwa sasa, fanya kama umetoa sadaka hiyo fedha, maana mlolongo wa kuipata unaweza kutumia mara 10 ya hiyo uliyotuma
 
G_Carson,
hayo majibu yao ni sahii. itifiki za kurudisha hela mzunguko sana. hata benk teller akikosea hayo mambo ya tra ni hasara kwa benki
inaweza kuchukua miaka hata miwili kuirejesha kwa strong follow up
 
I feel sorry for you brother.

Hizi teknolojia nzuri zinapoenda vizuri. Ila zikienda against unaweza hisi dunia inakuangukia.

Niliwahi toa 1M toka NBC kwenda tigopesa mwaka 2014. Hela haikufika tigopesa ila kwenye kwenye account iliondoka.

Ilinichukua mwaka na nusu ile hela kuirudisha. Tena baada ya kumfahamu mtu ndani ya benki kunisaidia.

Hapo ndo nilijua hizi teknolojia sio reliable 100%.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usipotoshwe na majibu ya juu juu unayopewa humu na baadhi ya watu, pesa yako uliyotuma kamwe haitopotea!. Nenda Vodacom ukasitishe huo muamala au wakaitume hiyo pesa kwenye akaunti uliyopewa ya CRDB. Usiende kubembeleza, hiyo ni pesa yako halali na Voda wana jukumu la kuifikisha pale unapotaka kuituma.
 
Usipotoshwe na majibu ya juu juu unayopewa humu na baadhi ya watu, pesa yako uliyotuma kamwe hatopotea!. Nenda Vodacom ukasitishe huo muamala au wakaitume hiyo pesa kwenye akaunti uliyopewa ya CRDB. Usiende kubembeleza, hiyo ni pesa yako halali na Voda wana jukumu la kuifikisha pale unapotaka kuituma.
Kuna tofauti ya kumpotosha mtu na kumwambia ukweli. Fedha ikashatoka kwenye muamala wa MPesa kwenda kwa ajili ya malipo akaunti ya benki mlolongo wale wa kuipata ni headache, transaction ya kuirudisha kwenye account yako ni ngumu mno. Si rahisi kihivyo unavyosema. Kuna jamaa yangu alilipa hivyo hivyo kutoka Mpesa kwemda NMB laki saba, ilikuwa Julai 2019, leo ni Machi 6, 2020 bado anahangaikia kuipata hiyo fedha. Usimpotoshe, Mpesa wenyewe wanakuambia hawama access ya kuirudisha muamala uliofanya malipo kwenye account ya benki. That's it.
 
Kwa maelezo haya,basi kuna uzembe mahali na siyo kama kuna usumbufu. Km ulimpata mtu akakusaidia na ukaipata pesa yako,why kwingine kuwe na usumbufu kiasi cha kukatisha tamaa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio mchezo.mm ilinitokea ya kutoa bank kwenda m pesa nikakosea namba.kupiga voda wakasema niende bank nilivyoenda bank nikajaza form baada ya wiki ilirud pesa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
I feel sorry for you brother.

Hizi teknolojia nzuri zinapoenda vizuri. Ila zikienda against unaweza hisi dunia inakuangukia.

Niliwahi toa 1M toka NBC kwenda tigopesa mwaka 2014. Hela haikufika tigopesa ila kwenye kwenye account iliondoka.

Ilinichukua mwaka na nusu ile hela kuirudisha. Tena baada ya kumfahamu mtu ndani ya benki kunisaidia.

Hapo ndo nilijua hizi teknolojia sio reliable 100%.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo sio teknolojia, tatizo ni business process inayotumia hiyo teknolojia, je kuna sera yoyote ya refund. Teknolojia hufanya kazi vyema kama mifumo ndani inafanya kazi vyema
 
System ya kulipia Tra bado haijaunganishwa na mitandao ya simu hivyo hiyo transaction lazima ikatae, pesa yako kama kweli ilikatwa basi itarudishwa
 
Sio mchezo.mm ilinitokea ya kutoa bank kwenda m pesa nikakosea namba.kupiga voda wakasema niende bank nilivyoenda bank nikajaza form baada ya wiki ilirud pesa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nadhani umeenda nje ya mada.

Kinachoongelewa ni namba ya malipo ya Tra ikishaudaka 'mpunga' huwa haiutemi, piga galagaza.

Namba ya malipo ya Tra ikiishakumeza hela hata kwa bahatimbaya, kuirejesha ni msala ulioshinda wajanja wengi.

Tufike mahali tukubaliane kuwa mfumo huo umekaa kipigaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom