Kuhamia Dodoma ni Utajirisho kwa Mawaziri?

Boreless

Member
Aug 25, 2009
61
39
Kwa dhati nampongeza Rais Dk. Magufuli kwa uamuzi wa Serikali yake kutimiza ndoto ya Taifa kuhamishia makao makuu Dodoma. Pamoja na pongezi hizi, kuna jambo moja nimeshtukia linakinzana na kaulimbiu na jitihada za Rais kupunguza matumizi ya taaasisi za umma hasa kwenye mambo kama posho za safari na malazi.

Lililonishtua ni kwamba kama hakutachukuliwa tahadhari ya haraka, Serikali hii itaingia ghalama kubwa mno katika kulipa posho za safari na kujikimu kwa Mawaziri na watendaji wengine wa Serikali ambao kiitifaki tayari wamehamia Dodoma. Kwa mfano Waziri Mkuu alikuwa kiongozi mkubwa wa kwanza kuhamia Dodoma Septemba mwaka jana. Lakini toka ahamie, kwa wastani asilimia 20 yupo Dodoma, 30% ziara mikoa mingine na 50% yupo Dar es Salaam. Wiki hii Waziri na wizara ya Utumishi wa Umma nayo iliuaga mji kwa mbwembwe kuwa inaelekea Dodoma. Lakini kumbe kilichoondoka ni magari ya mizigo Waziri bado yuko Dar! Mifano iko lukuki.

Kiitifaki hawa watumishi wanapohesabika kuhamia Dodoma, Dar na mikoa mingine inahesabika kama kazi nje ya kituo. Hivyo watumishi hao hutakiwa kulipwa posho ya malazi na ya kujikimu.

Ikiwa waliojitangaza kuhamia Dodoma muda wao mwingi wanautumia Dar maana yake ni kuwa ghalama za kuendesha Serikali zitaongezeka katika kulipa posho. Na kwa wale wasio waadilifu watatumia mwanya huo huo kuongeza mapato. Hivyo ni muhimu suala la viongzo na ofisi zilizokwishajitangaza kuhamia Dodoma zidhiitiwe kwa kuwekewa utaratibu juu ya posho za ugenini hasa Dar es Salaam. Ikumbukwe wengi wa wanaohama wanaacha familia na vitega uchumi vyao Dar. Kwa hiyo kuna kila kichocheo cha wao kupenda kurudi au kutumia muda mwingi Dar.

[HASHTAG]#TutafakariDodoma[/HASHTAG]
 
Wanafiki chadema acheni watu watimize ahadi zao kwa wananchi. Nyie hata ofisi ya chama imewashinda kwa miaka 30!!!
Yeyote aliye makini atakaposoma andiko langu, halafu akapitia maoni yako, haraka sana anang'amua kuwa tunaishi dunia mbili tofauti na vilevile uwezo wetu kifikra na katika kuanisha mambo unatofautiana mbali mno. Jaribu kusoma upya nilichoandika na jipe muda wa kutafakari kabla hujaandika maoni yako.
 
Wanafiki chadema acheni watu watimize ahadi zao kwa wananchi.
Nyie hata ofisi ya chama imewashinda kwa miaka 30!!!
Bila kujali itikadi maoni yake yana msingi na ni vizuri kwa wakuu kuutumia ushauri au maoni yake sincerely sijui km una akili timamu 'sorry to say that''
 
Wanafiki chadema acheni watu watimize ahadi zao kwa wananchi.
Nyie hata ofisi ya chama imewashinda kwa miaka 30!!!
Duuu hata kwenye issues za msingi unaingiza uchadema na uccm hii ni balaa kwa taifa, angalizo la huyu ndugu limekaa vizuri sana na linaakisi hali Halisi itakavyokua lisipoangaliwa
 
Wanafiki chadema acheni watu watimize ahadi zao kwa wananchi.
Nyie hata ofisi ya chama imewashinda kwa miaka 30!!!
acha na ficha ujinga wako,hapa yanaongelewa maslahi ya taifa.usifanye kulinganisha mambo ya wizara kuhamia dodoma na chadema kujenga office,soma kwa makini na tafakari upya.
 
Sidhani km hayo maoni yako yata apply kwa JPM na hii itawalazimisha kuhamia mapema iwezekanavyo.Hata hivyo hili zoezi Lina gharama zake ambazo haziepukiki ili kufikia malengo yaliyowekwa.
 
Kwa uelewa wangu,Perdiem ni posho ya safari anayolipwa mtumishi anapokuwa amesafiri kikazi nje ya kituo chake cha kazi mfano kasafiri kwenda nje ya mkoa,nje ya nchi,katoka nje ya wilaya,n.k. na ambako atapaswa kuwepo huko kwa siku kadhaa akitekeleza majukumu aliyopangiwa/aliotumwa kuyafanya.

Sasa serikali itakapokuwa imehamia Dodoma,mawaziri bado watakuwa entitled kulipwa perdiem tena ukizingatia wana magari ya serikali yanayowahudumia kwa kuwapeleka na kuwarudisha popote pale wanapotoka?

Ningekuwa mbunge wa upinzani swali hili ningemuuliza Waziri Mkuu siku ya kuulizla maswali ya papo kwa papo kwa waziri mkuu au waziri mwenye dhamana kupitia kipindi cha maswali ma majibu.

Mbali na wabunge wa upinzani hata waandishi wa habari mnaweza kumuuliza swali hili Waziri Mkuu au hata Katibu Mkuu kiongozi.

Tunahangaika na watumishi hewa lakini malipo yenye utata bado yako mengi sana.
 
Wala hakuna haja ya kuuliza hilo swali kwa Waziri Mkuu maana jibu lake ni Rahisi.

JIBU.

Wizara zilizohamia Dodoma ina maana makazi yao na Ofisi zao zipo Dodoma.
Per Diem watapewa kama watatoka nje ya Dodoma.
Mfano:Kama watumishi wa Wizara hizo watakuja Dar es Salaam kikazi ni lazima walipwe per diem.
 
Kama vile una majibu then unajiuliza maswali kujijibu hapo hapo:(:(

Umesema mtumishi akisafiri.nje ya kituo.cha kazi anatakiwa kulipwa na hiyo ni sheria ya utumishi, kwa hiyo kama kituo cha kazi ni Dodoma akitoka nje ya Dodoma atalipwa kama sheria inavyosema.

Sioni swali lipo wapi hapo;)
 
Wala hakuna haja ya kuuliza hilo swali kwa Waziri Mkuu maana jibu lake ni Rahisi.

JIBU.

Wizara zilizohamia Dodoma ina maana makazi yao na Ofisi zao zipo Dodoma.
Per Diem watapewa kama watatoka nje ya Dodoma.
Mfano:Kama watumishi wa Wizara hizo watakuja Dar es Salaam kikazi ni lazima walipwe per diem.
Una hakika hilo huwa linafanyika kwa wakubwa hawa?
 
Una hakika hilo huwa linafanyika kwa wakubwa hawa?

Kama halifanyiki ndio fursa stahiki ya kupata majibu kupitia Maswali ya papo kwa papo Bungeni.
Kuna Waziri mkubwa nae alitangaza ameshahamia Dodoma lakini mara nyingi anaonekana DSM.Kama analipwa Per Diem bila shaka anaikomba Hazina ya Taifa.
 
Wanafiki chadema acheni watu watimize ahadi zao kwa wananchi.
Nyie hata ofisi ya chama imewashinda kwa miaka 30!!!

Nyie wenye Miaka 55 tuonyesheni hata jengo moja mlilojenga,tunaojua vyema majengo yote mmepora serikalini.Si bora hao CDM wanamiaka 20,na kungekuwa na FAIR play kwenye siasa leo CDM wangekuwa mpaka na TV na Redio yao
 
Wanafiki chadema acheni watu watimize ahadi zao kwa wananchi.
Nyie hata ofisi ya chama imewashinda kwa miaka 30!!!

Post yako ni udhihirisho wa jinsi gani vijana wa Lumumba mlivyokuwa wakurupakaj, nina uhakika hujasoma mada iliyopo umekimbilia kutoa shutuma kwa Chadema huo ni ujuha wa kiwango cha juu sana, na kama ndiyo huko kubembeleza kuteuliwa kwa akili kama hizi hata ujumbe wa mtaa wewe hutoshi.
 
Raisi mwenyewe kasema atahamia dodoma ifikapo 2020 hii maana yeke nini?

1.vikao vyote vya baraza la mawaziri vitapaswa kufanyika dar es salaam kwa kuwa Raisi ndiye chairman wa baraza hilo hivyo posho za kuwa nje ya kituo cha kazi kwa mawaziri, madreva na wasaidizi wao pamoja na mafuta ya magari zitahusika hapa.

2.Mrejesho wowote wa waziri yeyote utalazimika kufanywa ikulu ya dara es salaam hapa napo rejea gharama kama zinavyoonekana haya ya kwanza hapo juu.

3.Ugeni wowote utakaohitaji uwepo wa mawaziri utapokelewa dar es salaam hapo napo ni uraji mtupu kwa watu

ACHENI WIVU NI WAKATI WA MAWAZIRI NA WASAIDIZI WAO KUFAIDI MATUNDA YA MAAMUZI MABOVU.
 
Back
Top Bottom