Kuhakiwa kwa Akaunti ya Facebook

Kuhakiwa kwa Akaunti ya Facebook

Umkonto

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2018
Posts
3,115
Reaction score
5,368
Akaunti yangu ya Facebook imehakiwa (Hacked), ingawa mimi siyo maarufu ila nina friends zaidi ya elfu 4 na nimejiunga kwenye pages na groups mbalimbali za ndani na nje ya nchi, ambapo nilikuwa natumia kutangaza biashara za hapa na pale, pamoja na kuburudika na nilipokuwa nataka mambo sirias sirias nakuja huku Jamii Forum.

Kwa sasa siwezi kufanya chochote katika akaunti yangu na hata wahusika wa Facebook hawana msaada wowote kwa sababu hawana direct contacts zaidi ya zile(help tips) zilizosetiwa ambazo zimeshindwa kunitatulia tatizo langu.

Tatizo langu ni kwamba, haka(hacker) ka-hack akaunti yangu na kufuta email na namba yangu ya simu ambazo nilitumia kufungulia akunti yangu. Kwahiyo, ninashindwa ku-recover password kwa sababu facebook haitambui email wala namba ya simu kwa sababu vimeondolewa kwenye akaunti yangu na jamaa kaweka email yake. Mimi nilitumia gmail, ila kwa sasa verification code inatumwa kwenye hotmail ambayo haka kaiweka baada ya kuondoa yangu. Hiyo hotmail inaoenekana herufi chache kama inavyokuwaga. Mfano "s.........a@hotmail.com

Nikajaribu kusachi kwa majina akaunti yangu ya Facebook inaonekana ila ndiyo hivyo nikiweka email au namba ya simu ili ni-recover password, verification code zinaenda kwenye hotmail ya haka (Hacker).

Nilipoona inagoma nikaenda kwenye email niliyosajilia, nikakuta notifications kwamba, email na namba za simu katika Facebook vimeondolewa location ikiwa ni Netherlands, na mpaka IP adress imeoneshwa kasoro mtu aliyefanya hivyo.

Nikajaribu kuvuta kumbukumbu, inawezekana nili-click links ambazo ndizo zimeiba taarifa zangu za siri kuhusu akaunti yangu.

Suluhisho pekee la kurudisha akunti yangu ni kwa Facebook ku-reverse akaunti ya awali na kunitumia verification code. Maelezo ya ku-reverse email yapo katika "help tips" za Facebook lakini hakuna sehemu ya kubonyeza ili wali-reverse akunti ya awali.

Kwa udhaifu huu wa kushindwa ku-reverse email ya awali, naona mtandao wa Facebook si salama kabisa, kwa sababu nilipo-search google nimekutana na watu kadhaa wanalalamika wamehakiwa na kuondolewa email na namba zao za simu, hivyo inakuwa ngumu ku-recover akaunti zao kwa sababu hawawezi kupata verification code.
 
Pole mzee, acc yako possibly ni potential kiasi cha mtu kui hack au kama hao followers ameona watamsaidia, lakini sasa mtu wa Netherlands atake followers wa kibongo why??? Au ame fake location...
 
Pole mzee, acc yako possibly ni potential kiasi cha mtu kui hack au kama hao followers ameona watamsaidia, lakini sasa mtu wa Netherlands atake followers wa kibongo why??? Au ame fake location...
Sijajua ni kitu gani kimefanyika
 
Hata mm kipindi hicho ilichukuliwa na jamaa wa Kenya.....nenda kwenye password change badili nywila....mara nyingi huwa wanakuwa hawana umiliki nayo 100%


Japo mm namba niliojiungia nilikwisha poteza nikacheki hakukuwa na picha za ajabu nikaipotezea
 
funguka mkuu , hakuna details zaid ulizompa uyo haka mpaka akaweza kukulog out ..
 
Kuna jamaa wanaojifanya mabinti , wanawasiliana na wewe , itakuwa umewapa information wakaamue kula kichwa ,
 
Kuna jamaa wanaojifanya mabinti , wanawasiliana na wewe , itakuwa umewapa information wakaamue kula kichwa ,
Nachohisi niliclick links fulani fulan nilitumiwa kama sms nikazifungua
 
Back
Top Bottom