Kugawagawa mikoa

Kugawagawa mikoa

Ukweli kuongeza idadi ya mikoa ni faida kwa upande wa siasa tu na si kwa wananchi wa kawaida. Ukweli nikwamba katika ofisi za halmashauri za wilaya huduma zote zinazohusu wananchi zinapatikana hapo. Mkurugenzi, madiwani na wakuu wa idara ndio kila kitu wilayani. Mwananchi wa kawaida kupata shida ya kwenda mkoani ni nadra sana.

Tena mimi napendekeza ziongezwe wilaya zingine kadri inavyowezekana.

Kuongeza mikoa mipya nikutanua goli kuwa na nafasi kubwa ya kuwazawadia vibaraka nafasi za kujisitiri.

Hivi ninini umuhimu wa RC, RAS, RPC, RMO. Walioko wilayani wanatosha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wakati mwingine inafaida kuna wilaya moja ilikuwa km 240 ndiyo unafika mkoani tena hakuna lami, kama huduma za afya ukipewa rufaa kwenda mkoani piga picha barabara ya vumbi, wakiagiza kifaa lazima kipitie mkoani na mkoa ukipokea unajadili hiki kitaenda vipi wilayani ikiwa mkoa hauna hapo angalia wilaya iliomba wizarani kuna faida zake mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo yaani kama upande wa afya wilaya inakosa mpaka ex-ray wakiagiza ikiletwa mkoani waamue

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwahiyo tuwe tunaanzisha mikoa mipya ili ziwepo hospitali zenye x ray? Hujui kama nimakosa makubwa sana hospitali ya wilaya kutokuwa na x ray?

Tatizo wakuu wa mikoa wamepewa majukumu mengi ambayo ilifaa wapewe wakuu wa wilaya maana wakuu wa wilaya wenyewe ndio wako karibu na wananchi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kabisa sijaona sababu ya kuitenganisha Mbeya na Mbozi,Iringa na Njombe..
 
Back
Top Bottom