mimi najivunia mvi zangu sioni sababu ya kuzificha kwani nitakuwa ninajihadaa mwenyewe.............pili kwa wale ambao hawapendi ziwe nyingi jibu ni kula kwa kiasi na kufanya mazoezi................tumia njia za asilia badala ya madwa katika kupunguza kuzeeka kwa haraka.........haraka ambako husababishwa na mwili kukosa mazoezi au kuvimbishwa na milo kupita kiasi.......
Mbona sio mvi peke yake zinazonyesha kua huyu jamaa ni mzee,labda wanaume wengine wanaona haya mvi lakini mie sioni mvi ni aibu kwa mwamume au tatizo lininyime raha ya kula vyangu...
Kwa hiyo unajivunia kula mno na kutofanya mazoezi au?
Mimi naona bado unajihadaa mwenyewe kwa kujilazimisha na kutulazimisha tuamini kuwa mvi ni busara na shikamoo ni hekima. Ndugu yangu, MVI na KIPARA ni matokeo ya ukosefu wa lishe iliyobalance au kuchoka kwa mwili wako kuzalisha cells zinazohusiana na ukuaji na ubora wa nywele. Kama unaamini mvi ni akili, basi next year utakuwa Head Teacher kwenye moja ya shule za kata wilayani kwako, endelea kuzifuga.
Mvi ni dalili ya ukubwa, na mtu anaye ukataa ukubwa ujuwe ni f a l a tu.
Tusitaifishe mambo binafsi......kuwa na mvi au kutukuwa nazo ni jambo binafsi
Nenda kwenye job interview na mamvi ukione.......
Nilishakujibu kuwa kupendeza ni mtizamo wa mtu. Wewe unaweza kuona unapendeza na mvi mwingine akaona hapendezi.
Na kama kupendeza kwako siyo ishu, mbona uliuliza kama ukiwa na mvi unakuwa hujapendeza? Wewe umeona mvi zinakupendeza sasa juu ya nini uulize wenzako wanataka wapendeze ili iweje
Kwa hiyo hapa unawaza kutongozwa au?
Hivi binti yako akitongozwa na kijana unapata faida gani ambayo akitongozwa na mzee utaikosa? Mi nilidhani suala ni binti yako kuwa makini na wazee na vijana!
Mvi ni dalili ya ukubwa, na mtu anaye ukataa ukubwa ujuwe ni f a l a tu.
atawatofautishaje? kama na wazee wa rika langu nao bado wanajitia poda usoni na utosini kumhadaa mwanangu.......lol
mvi si uzee..mbona vijana wadogo cku hizi wana mvi kibao kichwa kizima
Moja kati ya sifa za mtu mzee ni KUNG'OKA MENO. Ikiwa leo mtu ameng'oka meno na akaamua kuweka ya bandia, hii inatafsirikaje, body repair au kuwahadaa vijana?
Kwa hiyo una certificate kwa ajili ya mwanao kuhadaiwa na vijana ila inakuuma mwanao akihadaiwa na wazee.
MWAMBIE MWANAO AACHE UHUNI, wazee au vijana wote ni uhuni. Mwambie asipende kuvuliwa chupi. Na ukiona mtoto wako anadanganyika namna hiyo, usipigane na waongo, pigana na tabia ya mwanao ya kujifanya dust bin
Ukubwa pia huambatana na kupungua kwa nguvu za kiume na makunyanzi, navyo mnavishangilia au mnabadili nutrition kusave purpose?
Matusi ya nini? Mimi sidhani kama mtu kukataa mvi ni kukataa ukubwa. Lini ulimsikia mtu aliyebadili nywele akikataa miaka yake? WEKA TOFAUTI YA KUKATAA MVI NA KUKATAA UKUBWA.
Na nikukumbushe kuwa kuna watoto wa umri wenu nao wana mvi, na wao ni wazee?
we mtoa mada huna jipya,, mjini hakuna wazee bana kuna watu wazima tu.. ni sawa na wewe tukuulize ukioga unamtegea nani? si ubaki na uchafu tu
Kila binadamu ana mtazamo wake na maamuzi yake kulingana na kitu roho yake inapenda na kupata amani.
Wakati mwingine mvi zinakosesha amani (kwa wazee) kila ukijiangalia unaona mvi, hii inakukumbusha kuwa wewe umeshakomaa vya kutosha na kilichobaki ni kuvunwa tu! (kufa) kwa maana hiyo, ni heri uzipotezee mvi kwa kuzitia rangi ili zisikukumbushe kila mara kuwa wewe ndio umefika mwisho pamoja na kwamba ukweli unabaki pale pale. Hii inasaidia kujiona uko sawa na wengine huondoa mawazo kwamba muda wako umeisha.
Elewa mawazo haya si kwa wote. Kuna wengine hata akijiangalia hawazi chochote kuhusiana na mvi zake. Mazingira tunayoishi yanaweza kuchangia kuziona mvi ni mvuruga amani moyoni au kutojali kuona mvi. Uzee mbaya mweeeeeeh!