industriousman
Member
- Jul 7, 2021
- 49
- 23
Ukikutana na mwanafunzi mwenye ulemavu wa akili unaweza kumshangaza Mungu na kumchekesha shetani.
Uwezo wa kupambania masomo hana, fikra zake na stori zake ni namna ya kumvua kufuli demu mkali anaewalaza macho pale darasani.Ratiba za vigodoro, kamari na namna anavyomchukia mwalimu mnoko pale shuleni.Matokeo yake kitaaluma yanatia huruma na yeye mwenyewe anahuzunisha sana, halafu ukimuuliza mbona anafeli na hana jitihada zozote kubadili hali yake anakujibu ''Kufeli mtihani wa shule, sio kufeli mtihani wa maisha"
Ukimtazama labda maisha anayajua basi, unaishia tu kujisemea ''Mungu saidia huyu kijana" Maisha ya nyumbani kwao yamedumaa, wazazi wake wanahaha tangu jua linachomoza mpaka linatua kumsomesha aje kubadilii hali ya mambo halafu kijana mwenyewe anawaza namna ya kumdhibiti demu wake anaemlia shilingi zake anazoiba kwenye mifuko ya mashati na suruali za baba'ke kama sio pochi za mama'ke baada ya kufanya vibarua kwa mabepari weusi.
Sijui ni nani aliwamezesha huu ujinga kudharau elimu na kuona maisha baada ya kufeli shuleni ni rahisi sana bila elimu.Bahati mbaya maisha yenyewe hayategemei elimu tu ya darasani yanataka mambo mengi ikiwemo elimu unayoipata kila siku nje ya darasa.Bora hata angekuwa anajishughulisha basi hata kutafuta elimu ya nje ya darasa masikini akitoka shule ni kwenye vijiwe vya ku-bet, kuvuta bangi na kuvizia watoto wakishua wakitumwa dukani.Akitoka shule ni kwenye vibaraza vya umbea na kuchambana na mashosti zake waliofeli darasani na mtaani wanaishi kwa huruma za wasio na huruma kwa mabinti za wazazi wenzao
Mtihani wa shule kafeli na mtihani wa maisha anaelekea kufeli vilevile wala hashtuki zaidi zaidi anajitahidi kuikimbia mitihani yenyewe kwa kubagua kazi na kutaka maisha anayoyawaza kwa sababu aliaminishwa na motivational speaker kuwa ''kile unachofikiria ndicho huwa" anatumia muda mwingi kufikiria maisha mazuri anayoyapenda kuliko kuziweka fikra zake katika vitendo ili aukimbie ugonjwa wa ufukara unaowatesa nyumbani kwao.
Hebu endelea kuwashauri wadogo zako wa sekondari, hizi falsafa za ''kufeli mtihani wa shule sio kufeli mtihani wa maisha" zinazalisha kizazi cha walemavu wa akili.Shule wanafeli na maisha wanafeli vilevile na kuishia kupiga watu ngeta, kuvuta bangi, wizi na kufungua biashara ya ngono kwa mitaji ya miili yao.
Great Industrious.
There is story in everything
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Uwezo wa kupambania masomo hana, fikra zake na stori zake ni namna ya kumvua kufuli demu mkali anaewalaza macho pale darasani.Ratiba za vigodoro, kamari na namna anavyomchukia mwalimu mnoko pale shuleni.Matokeo yake kitaaluma yanatia huruma na yeye mwenyewe anahuzunisha sana, halafu ukimuuliza mbona anafeli na hana jitihada zozote kubadili hali yake anakujibu ''Kufeli mtihani wa shule, sio kufeli mtihani wa maisha"
Ukimtazama labda maisha anayajua basi, unaishia tu kujisemea ''Mungu saidia huyu kijana" Maisha ya nyumbani kwao yamedumaa, wazazi wake wanahaha tangu jua linachomoza mpaka linatua kumsomesha aje kubadilii hali ya mambo halafu kijana mwenyewe anawaza namna ya kumdhibiti demu wake anaemlia shilingi zake anazoiba kwenye mifuko ya mashati na suruali za baba'ke kama sio pochi za mama'ke baada ya kufanya vibarua kwa mabepari weusi.
Sijui ni nani aliwamezesha huu ujinga kudharau elimu na kuona maisha baada ya kufeli shuleni ni rahisi sana bila elimu.Bahati mbaya maisha yenyewe hayategemei elimu tu ya darasani yanataka mambo mengi ikiwemo elimu unayoipata kila siku nje ya darasa.Bora hata angekuwa anajishughulisha basi hata kutafuta elimu ya nje ya darasa masikini akitoka shule ni kwenye vijiwe vya ku-bet, kuvuta bangi na kuvizia watoto wakishua wakitumwa dukani.Akitoka shule ni kwenye vibaraza vya umbea na kuchambana na mashosti zake waliofeli darasani na mtaani wanaishi kwa huruma za wasio na huruma kwa mabinti za wazazi wenzao
Mtihani wa shule kafeli na mtihani wa maisha anaelekea kufeli vilevile wala hashtuki zaidi zaidi anajitahidi kuikimbia mitihani yenyewe kwa kubagua kazi na kutaka maisha anayoyawaza kwa sababu aliaminishwa na motivational speaker kuwa ''kile unachofikiria ndicho huwa" anatumia muda mwingi kufikiria maisha mazuri anayoyapenda kuliko kuziweka fikra zake katika vitendo ili aukimbie ugonjwa wa ufukara unaowatesa nyumbani kwao.
Hebu endelea kuwashauri wadogo zako wa sekondari, hizi falsafa za ''kufeli mtihani wa shule sio kufeli mtihani wa maisha" zinazalisha kizazi cha walemavu wa akili.Shule wanafeli na maisha wanafeli vilevile na kuishia kupiga watu ngeta, kuvuta bangi, wizi na kufungua biashara ya ngono kwa mitaji ya miili yao.
Great Industrious.
There is story in everything
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app