Kufeli kwa shule za serikali

Matokeo mabaya kwa shule za serikali angalieni wakuu wa shule wengi ni wabovu na sio wabunifu wanashindwa kuwasimamia walimu wao hivyo serikali m-deal na hawa wakuu pia ikiwezekana muwachague walimu wa sayansi wawe wakuu wa shule.
nimeangia huku nikajua kuna mambo ya msingi, kumbe mtoa mada haharisha barabarani. yaani unaongea swala la kuwawajibisha wakuu wa shule, huku unaacha kuongea swala la kuiwajibisha serikali kwa kugoma kuajiri walimu waliomaliza elimu yao tangu mwaka juzi. kwanini usinyumbue akili na ukaona kama serikali yetu mbovu nayo inasababisha shule zetu za umma kuendelea kufanya vibaya kutokana na kuendelea na msimamo wao mchafu wa kuwasomesha namba watoto wa wanyonge kwa kutowapatia walimu wa kuwafundisha!!!
 
Shule za serikali enzi zetu zilikuwa best
enzi hizo shule za umma zilikua poa kulinganisha na za binafsi kwasababu
1. uwekezaji ktk shule za binafsi ulikua ni mdogo
2. kipindi hicho shule za umma zilikua chache na serikali ulikua inaajiri walimu waliokua wanamaliza vyuo.
3. kwa kiasi kikubwa, wanafunzi waliokua wanachaguliwa na kuripoti kt shule za umma walikua wenye uwezo mkubwa kutokana na mchujo wa kupenya ktk kuchaguliwa ktk shule chache zilizokuwepo. pia wanafunzi hao walikua hawahamii ktk shule za binafsi kwani shule za umma ndizo zilizokua zinafanya vizuri.
4. shule za binafsi walikua wanapata wanafunzi vilaza waliokosa nafasi za kuchaguliwa ktk shule za umma. vipanga wote walikua hawahamii shule binafsi kutokana shule za binafsi kuwa na ada kubwa na ufaulu mdogo.
5. ...

kwasasa shule za umma ziko nyumba ya shule za binafsi kwasababu
1. kuongezeka kwa shule a umma (hasa za kata). japo serikali zilizopita zilijitahidi kwa kiasi chao ktk kuboresha elimu kwa kuajiri walimu, ila changamoto ktk shule hizo ni nyingi na hazijaisha. hii imepelekea kuyumba kwa shule za umma.
2. kutoajiri walimu ktk shule za umma kwasasa. huu uongozi wa bana matumizi, tukajenge uwanja wa ndege wa kimataifa kule chato unaathiri elimu yetu.
3. uwekezaji mkubwa ktk shule za binafsi. shule za binafsi zinazofanya vizuri zimewekeza sana ktk elimu. changamoto almost zote za kielimu hazipo ktk shule hizo. mazingira mzuri ya kufundisha na kujifunzia, walimu wa kutosha wanaolipwa vizuri, n.k.
4. shule za binafsi zinapata wanafunzi vipanga tena kwa mchujo wa kitaalamu. sio kama huku kwetu tunajisifu kua 98% ya waliomaliza la saba, wamechaguliwa kujiunga form one. huku walio wengi hawajui hata kusoma wala kuandika. vipanga wanavutiwa ktk shule za binafsi hasa ktk mambo ya mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia, na uwepo wa walimu wa kutosha wanaofanya kazi kwa moyo kutokana na kulipwa vizuri.
5. ...
 
Waalim ni wito sio kaz
hii kauli ni mbaya sana na ndiyo inayotumika kuwatesa walimu. halamshauri nzetu na serikali yetu, Mungu anawaona jinsi kwa jinsi wanavyowatesa walimu wetu, hali inayopelekea kuwashusha moyo wa kutufundishia watoto wetu, na hatimae watoto wetu wanarudi na sifuri wakati tuliuza ngimbe wakasome. usirudii tena kuongea kauli mbaya kama hii
 

wewe wa juu, soma coment ya huyu wa chini kisha useme neno.

 
Police hawahawa tunaonunua wote michicha na tembele mtaani ndo wapewe miposho hiyo acha utani ww
 
Police hawahawa tunaonunua wote michicha na tembele mtaani ndo wapewe miposho hiyo acha utani ww
kama hujui na hilo kwasasa, basi ukale malimao. kwa taarifa yako polisi kwasasa wako vizuri. stori ulizohadithiwa hapo zamani, ambazo ndizo umekuja kutuhadithia leo, sio za kweli kwasasa. polisi wako poa kwasasa huku walimu wakiwa na njaa kali.
 
kila mtu abebe msalaba wake, Private na msalaba wake na nyinyi wananchi kufeli kwa watoto wenu ndio msalaba wenu
 
Usilinganishe shule za kata na shule za enzi zetu.
Hadi sasa Matokeo ya Mbopo au Kitonga huwezi kufananisha na ya Kisutu au Kibasila, Azania, au Kambangwa.

Kabla hata hatujaenda kulinganisha hizi shule za kata na shule binafsi.

Nimesoma Sekondari za serikali za Dar kipindi cha Mkapa.

Shule za serikali za wilaya sijui mkoa niite ni tofauti na za kata.
1. Waalimu wazoefu katika mbinu za kumuwezesha Mwanafunzi kufanya vizuri.

2. Ilikua elimu nafuu sio elimu bure. Tulilipa ada lakini pia tililipia gharama za Maabara, Masomo ya Upishi na ushonaji, Maktaba na Mitihani ya kujipima kila wiki (kidato cha nne, hapa naimani walimu walipata motisha)

Shule zote zilikua maeneo yanayofikika kirahisi kwa usafiri wa jumuia isipokua Zanaki ilikua kamwendo kiasi ila kwa wanafu sio mbali

Baadhi ya shule kulikua na hostel kwa ajili ya kidato cha nne, wa sayansi walipendelewa zaidi.

Maabara zilikua (naamini hadi sasa) maabara kweli zenye vifaa vyote..

Uzio pia una umuhimu sana katika maendeleo ya wanafunzi kitaaluma.

Shule za kata zimekosa yote hayo. Mbaya zaidi hata lile lengo la kuanzisha shule kila kata sijalielewa.
Mwanafunzi kamaliza shule ya msingi Changanyikeni au Mlimani. Anapangiwa Mbopo au Njechele. Au kamaliza Manzese unampangia Saranga. Hao wanaopanga huwa hawafikirii suala la miundombinu? Huko maeneo jirani na walikomaliza la 7 hakuna shule ya kuwapeleka?

Mazingira yakiboreshwa katika hizo shule yatasaidia hawa watoto kutoka na alama nzuri.

Kwangu mimi shule kuwa ya Mwisho haiumizi. Kinachouma ni yale matokeo ya mtoto.

Tusiime ni ya 92 kitaifa, Mmiliki hiyo namba inamuumiza ila kama ingekua ni mzazi maskini wa Kitonga au Somangali akaambiwa shule yao ni ya Mwisho ila wanamatokeo yale, asingeumia kama hivi ambapo hakuna 1,2 wala 3. Ni 4 na 0.

Miundombinu! Miundombinu

Japo na utandawazi nao ni changamoto kwa kizazi hiki.
 

Mkuu;
Nashindwa kuelewa. Ati mtu asiye na wito umpe incentives za kutosha. Incentives zitakaa zitoshe kweli?? Kila siku tunatamani nyongeza, ikiwekwa, tunatamani tununuliwe magari, tulipiwe masomo ni lini tutasema imetosha??
Kuhusu ufaulu mdogo, tuseme basi waalim waliotumbuliwa wameonewa kabisa?? Elimu ya Tz kweli imevurugwa na mchawi aliyeiloga keshakufa. Sijui litafanyika nini elim irudi tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…