Kudai malipo kwa ukombozi leo ni aibu,masimango na kinyume na nia ya mwalimu katika liberation

Phillemon Mikael

Platinum Member
Nov 5, 2006
10,557
8,672
Leo nimesikiliza hotuba ya Rais Magufuli akiongea mbele ya Rais Zuma kafanya kosa kubwa sana ambalo pengine linatokana na kutoijuwa vema historia ya ukombozi kusini mwa Africa , au kutojua historia ya TANU .

Mwalimu Nyerere alisema "..Tanzania haiwezi kuwa huru kama nchi zingine za Africa Zitakuwa kwenye ukoloni ",toka hapo miaka ya uhuru sera yetu ya nje ilikuwa kusimamia ukombozi wa mwafrica .., na katika hili alisimamia yeye mwenyewe moja kwa moja akisaidiwa mwanzo kwa karibu na OSCAR NATHANIEL KAMBONA na baadaye na RADHID KAWAWA kabla ya kuundwa rasmi kwa kamati ya Ukombozi na Mtendaji Mkuu kuwa BRIG GEN HASHIM MBITA .

Tumejitolea sana hilo kweli lakini toka mwanzo Mwalimu alikataa kabisa kuweka kigezo cha kulipwa pesa , MWALIMU"S DOCTRINE AND HUMANITY IN LIBERATION ...hata viongozi wengi waliofuatia hakuna hata mmoja akiwemo MWINYI ambaye alipokea nchi katika mazingira magumu sana baada ya mwalimu kuwekewa vikwazo na IMF na WB wakizikataa sera zake za Ujamaa NA Kujitegemea .

Mwalimu alimkabidhi Mwinyi akijuwa hilo ,alumueleza " naelewa hawa watu hawanitaki mimi kwa ajili ya misimamo yangu , namimi sintaweza kujeuka nyuma" ,ila aliahidi kumshauri na ndiye specifically alimshauri alegeze masharti ikiwemo kukubali biashara huria ...ambapo yeye angekubali ingekuwa fedheha na ushindi kwa wazungu

Miaka mitano ya Mwinyi aliendelea na mapambano Majeshi yetu yakiwa Msumbiji na mengine yalikuwa yanasimamia Uganda hadi mwaka 1986, kama kuna wakati tungejeuka na kuanza kuwadai tuliowasaidia ulikuwa huo kama tulistahimili iweje tuje kujivua nguo leo ...

TANZANIA imebaki na hiyo heshima na hata kama tunaona hawajali lakini haiondoi ukweli kuwa tunayo kura ya turufu kwa ukanda huu"sphere of infuence" watanzania hatuhitaji kulipwa na hizi nchi bali tunahitaji kufanya nazo BAISHARA basi!! tusijivue nguo uzeeni ....
Unajua ni kama kumsomesha mtu alafu unaanza kumdai kwa kuwa ana kazi na watoto wako hawana kazi .....busara ni kukaa kimya na Mungu atakupa kwa ziada ..maana ukianza kukumbusha ni kama MASIMANGO...
Hivi hata kama watatulipa ....vipi kuhusu DAMU za askari wetu waliokufa kwenye mapambano...na familia zao wao wanastahili kulipwa nini ???? kuna ma agent TISS na wa jeshi walikuwa wakiingia na wapigania uhuru hadi SOUTH AFRICA wapo waliokamatwa ...na hata miili yao isionekane na wala ndugu zao hawajui wako wapi kutokana na nature ya usiri wa kazi hizo wakati huo ......watadai nini???

Viongozi walikuwapo enzi ya Mwalimu haya yakifanyika wapo ,ni vema wakamshauri Rais kuwa hata kwa mila za kiafrica Wema huwa haukumbushwi...bali muungwana ukimtendea akabaki na deni atabaki kulipa tu ..kwa kuwa atabakia na ile kauli " sijui nikulipe nini "....isije siku tukakutana na viongozi wasio wastaarabu huko wakatuambia " watanzania tuwalipe shilingi ngapi kwa kutusaidia ukombozi na kutoa maisha yenu?"

Misingi yetu ilikuwa ya UTU na UHURU NA HESHIMA WA MWAFRICA KAMA TUMEUPATA BASI TUFANYE KAZI KWA BIDII
 
Watanzania kwa unafiki tunaongoza!

Tunapenda kubadilisha maneno kwa faida ya mtaji wa kisiasa.

Kwa nini hushangai kuwa mpaka sasa tunawadai Uganda zaidi ya dola milioni 9 kwa ajili ya fidia ya vita vya uganda? Kwa nini hatukuwasamehe tu kwa sababu tuliwasaidia kumuondoa Rais Amin nchini Uganda. Ikumbukwe kuwa tulikuwa tunawadai dola milioni 123 lakini tukawasamehe na kuwapunguzia madai.

LINK>>Vita vya Kagera: Uganda imeanza kuilipa Tanzania

Rais amesema itakuwa vizuri zaidi kama Rais Zuma atafanikisha mkopo wa riba nafuu katika BRICS development bank ambayo kwa sasa inaitwa The New Development Bank kwa ajili ya ujenzi wa reli ili pia hata wa south Africa wakiamua kuja kutembelea kwa njia ya reli maeneo ambayo Tanzania iliwapa hifadhi iwe ni rahisi na kwa haraka.
 
Kila anaekuja anamuomba yaani ni sawa na baba mwenye mji kila ukipata mgeni unaanza kumwekeza shida zako ili uoate unafuu hii sio issue ni kujichoresha kwani uko alikosema akaombewe msaada hawezi ingia kinamna akapata alafu si alisema sie ndo tuombwe sio kuomba
 
Kila anaekuja anamuomba yaani ni sawa na baba mwenye mji kila ukipata mgeni unaanza kumwekeza shida zako ili uoate unafuu hii sio issue ni kujichoresha kwani uko alikosema akaombewe msaada hawezi ingia kinamna akapata alafu si alisema sie ndo tuombwe sio kuomba
 
Amenishangaza, kwanza huko si kuomba msaada ni kudai malipo

Kwa wanaoelewa misingi ya ukombozi ,unaweza kujificha chini ya uvungu kwa aibu ya yale maneno ........,hivi pia jiulize familia za KINJEKETILE,MANGI MELI,MKWAWA ,SONGEA etc walioongoza early resistance against wazungu .....walishawahi kulipwa ..
Waliopigana Uganda kuzuia uvamizi wa Iddi Amin wengine hadi leo wanadai ....wa ukombozi hadi leo walilipwa ....ndio Uje ujiulize leo hii Tukiombwa invoice Tutaandika nini ???
Ni bora ungeniambia unawadai wakoloni kwa kututawala kuliko kumdai kaka yako kwa kumkomboa kwenye minyororo.......kwenye koo zetu kuna watu tunabaki tu kuwaheshimu kwa kuwa babu zetu wanasema waliwasaidia na inatosha kiasi kila tukiwa na sherehe au misiba huko vijijini .....lazima tunawashukuru hadharani ....na kuwapa heshima kimapokeo ..kwa kuwa tuliambiwa na wazee wetu kuwa tuwaheshimu ..
Lakini pia koo za kiafrika kuna zingine ni maadui kwa ajili ya mapokeo ..HESHIMA YA TANZANIA KWA WAAFRIKA ITAENDELEA KUWEPO KIMAPOKEO NA HIYO ITATUPA FURSA NZURI TUKIITUMIA KUFANYA BIASHARA NA SIO KUOMBA MALIPO
 
Kila anaekuja anamuomba yaani ni sawa na baba mwenye mji kila ukipata mgeni unaanza kumwekeza shida zako ili uoate unafuu hii sio issue ni kujichoresha kwani uko alikosema akaombewe msaada hawezi ingia kinamna akapata alafu si alisema sie ndo tuombwe sio kuomba

Na huwa inapendeza hotuba za wakuu wa nchi zinajibiwa ....ni kama ile ya mfalme wa Morocco aliombwa uwanja ...hatukumsikia akijibu hotuba kusema alikuwabali au la amelishwa maneno ...ila kwa heshima anaweza kufanya lakini tujue uchumi wa nchi zetu hizi za kiafrika hautofautiani sana kiasi cha kuombana mambo makubwa makubwa ...zaidi tuhimize raia wetu wafanye biashara baina yao serikali zetu zipate kodi
 
Na huwa inapendeza hotuba za wakuu wa nchi zinajibiwa ....ni kama ile ya mfalme wa Morocco aliombwa uwanja ...hatukumsikia akijibu hotuba kusema alikuwabali au la amelishwa maneno ...ila kwa heshima anaweza kufanya lakini tujue uchumi wa nchi zetu hizi za kiafrika hautofautiani sana kiasi cha kuombana mambo makubwa makubwa ...zaidi tuhimize raia wetu wafanye biashara baina yao serikali zetu zipate kodi
Facts
 
Kwa wanaoelewa misingi ya ukombozi ,unaweza kujificha chini ya uvungu kwa aibu ya yale maneno ........,hivi pia jiulize familia za KINJEKETILE,MANGI MELI,MKWAWA ,SONGEA etc walioongoza early resistance against wazungu .....walishawahi kulipwa ..
Waliopigana Uganda kuzuia uvamizi wa Iddi Amin wengine hadi leo wanadai ....wa ukombozi hadi leo walilipwa ....ndio Uje ujiulize leo hii Tukiombwa invoice Tutaandika nini ???
Ni bora ungeniambia unawadai wakoloni kwa kututawala kuliko kumdai kaka yako kwa kumkomboa kwenye minyororo.......kwenye koo zetu kuna watu tunabaki tu kuwaheshimu kwa kuwa babu zetu wanasema waliwasaidia na inatosha kiasi kila tukiwa na sherehe au misiba huko vijijini .....lazima tunawashukuru hadharani ....na kuwapa heshima kimapokeo ..kwa kuwa tuliambiwa na wazee wetu kuwa tuwaheshimu ..
Lakini pia koo za kiafrika kuna zingine ni maadui kwa ajili ya mapokeo ..HESHIMA YA TANZANIA KWA WAAFRIKA ITAENDELEA KUWEPO KIMAPOKEO NA HIYO ITATUPA FURSA NZURI TUKIITUMIA KUFANYA BIASHARA NA SIO KUOMBA MALIPO
Hakika
 
Phillemon Mikael, ni nini exactly alichoongea?! Mbona naanza kutaka kujisikia aibu kabla sijapata undani wake?!

Halafu pamoja na mambo mengine, hivi anafahamu kwamba OAU iliunda kamati mbalimbali ambazo zilikuwa na makao yake makuu kwenye nchi mbalimbali na moja ya kamati hiyo ni Kamati ya Ukombozi iliyokuwa na makao makuu yake mjini Dar es salaam!!

Kwahiyo, pamoja na passion ya Baba wa Taifa kuhakikisha Afrika yote inakuwa huru lakini pia Tanzania ilikuwa ndiyo makao makuu ya Kamati ya Ukombozi na kwahiyo tulikuwa tunaitundea haki wajibu wetu huo!!!

Kwahiyo ina maana kuna mtu alikuwa anazungumzia suala la malipo kwa sisi kutekeleza wajibu wetu, au?!!
 
Hii tabia ya kimatonya mbaya sana, wageni wataambiana na watakata miguu kuja hata kutusabahi
Kila anaekuja anamuomba yaani ni sawa na baba mwenye mji kila ukipata mgeni unaanza kumwekeza shida zako ili uoate unafuu hii sio issue ni kujichoresha kwani uko alikosema akaombewe msaada hawezi ingia kinamna akapata alafu si alisema sie ndo tuombwe sio kuomba
 
Tafadhalini wakuu, hiyo hotuba mkuu alikuwa anaisoma au aliitoa kichwani au alichomekea, maana mwandishi wa Rais anayeweza kuandika maneno aina hiyo atakuwa hafai.
 
Akawaombe huko ambako hataki kwenda tatzo ni kwamba alikua ndan ya system pasipo kujua inandaje kaivaa pasipo kujiandaa akidhan mambo simple analeta vibur flow anadhan mchezo aende akaombe misaada uko sio kwa masikin wenzetu
Kiongozi mzuri ni yule anaeandaliwa kuongoza ila huyu amigo hakuandaliwa wala kujiandaa...ndo mana licha ya mazuri machache anayofanya bado anakurupuka ktk mengi pia!
 
Back
Top Bottom