Hizo ni security patch hazina shida huwa zinatolewa ili kufix bugs za currently running OS version ya simu yako unayotumia mpaka pale watakapoacha mara nyingi zinakuaga kila mwezi, baada ya miezi 2 au 3 inategemeana na kampuni za watengeneza simu walivyo schedule kwenye mfumo wao wa OTA (Over-The-Air)....
Ambacho haushauriwi kua na haraka nacho ni ku update Android Version moja kwenda ingine ikiwa tu imetoka siku chache, mara nyingi ni risk inabidi usubiri stable version kwani early released OS version inaweza kua na bugs za kutosha ikapelekea kitendo ume update tu basi simu inazima (soft brick), inaingia bootloop (yaani inawaka afu inaishia kwenye logo tu ndio bootloop), au inaifanya simu yako kua ina drain chaji haraka, simu kuchemka sana (Overheating)....
Mfano sasa hivi Google wako kwenye beta program ya Android 14 ambayo walianza April, May, June na July na labda wewe simu yako ingekua kwenye hii program ya kupokea hizo beta releases za Android 14 (Upside Down Cake kama inavyoitwa na wenyewe) basi ungejionea mwenyewe mabadiliko ya simu yako huenda ungepata matatizo kama niliyokutajia hapo juu au simu ingekaa poa bila tatizo, na ungekuja hapa kuomba ushari wa ku update OS versions za beta mimi nisingeli kushauri kama huna utaalamu na mambo ya Android Software...