Kozi za udereva chuo cha Taifa cha Usafirishaji(NIT)

Kozi za udereva chuo cha Taifa cha Usafirishaji(NIT)

Sasa naomba kuuliza je nit inapokea watu walio kuwa na uzoefu wa udereva kabisa au hata hambao hawajawai kuwa madereva ili nawenyewe wajifunze?
 
Sasa naomba kuuliza je nit inapokea watu walio kuwa na uzoefu wa udereva kabisa au hata hambao hawajawai kuwa madereva ili nawenyewe wajifunze?
Kigezo kikuu ni leseni yenye uhai kama imeexpire unaenda TRA unatafuta learner tatizo la pale ni Interview yao unapewa mbasi mkubwa wakati umezoea kuendesha IST kama ujazoea na ujawai kuendesha magari makibwa na una uzoefu na magari hayo usiende utakuwa umewapa bule 30,000 ya interview mim nilifel interview yao ila now ni mwezi wa pili nipo na roli kubwa la mchanga natafuta experience nikijiisi nmeiva narudi tena
 
Jamani naomba kujua hiyo Senior driving course ndyo sh ngap ,na inakuwa na madaraja mangap i?katika hyo course lakin pia inachukua mda .mana m nilikuwa natafta driving ya week 2 ,au hata 3
 
Habari zahumu ndani
Naomba msaada wa mawazo

Nina leseni daraja D E C1 C2 C3 NA E nataka nikasome maaana sikusomaga nifanyaje naanza wap hapa sielewi kila sehem napokwenda wanataka Cheti

Ninavigezo vyote Chet cha form4 kizur cha form 6 chet cha jkt nimekosa chet cha udereva sasa naazaje nianze kusomea wap
Ashnte
nenda NIT kasome ili upate cheti. kujiunga hawahitaji chet chochote zaid ya lesen yako.
 
naomba kujua ivi ukitaka kujiunga na vip (advance driver) na umeshapita veta inatakiwa uwe na vigezo gani vingine
unatakiwa kuwa na leseni ya udereva
kama lesen yako n daaraja D inabid uwe umekaa nayo miaka miwili
kama ni daraja E unatakiwa uwe umekaa nayo mwaka mmoja
ada ni 400 000. mda n week 2. venue NIT Dar.
 
Jamani naomba kujua hiyo Senior driving course ndyo sh ngap ,na inakuwa na madaraja mangap i?katika hyo course lakin pia inachukua mda .mana m nilikuwa natafta driving ya week 2 ,au hata 3
tazama hapaView attachment 1532478
20200809_213148.jpg
 
Jamani naomba kujua hiyo Senior driving course ndyo sh ngap ,na inakuwa na madaraja mangap i?katika hyo course lakin pia inachukua mda .mana m nilikuwa natafta driving ya week 2 ,au hata 3
Kaka hiyo senior n hatar inatka uwe na vigezo: uwe na chet cha grade two &one we unavyo...?
 
Sasa naomba kuuliza je nit inapokea watu walio kuwa na uzoefu wa udereva kabisa au hata hambao hawajawai kuwa madereva ili nawenyewe wajifunze?

Uwe dereva ambae sio mbabaishaji,maana pale unaenda jifunza sheria za barabarani za kima taifa.
 
Hellow wadau nimekua mfuatiliaji wa hichi chuo muda mrefu sana....

Elimu inayotolewa chuo cha taifa cha usafirishaji kozi fupi kwa madereva.

1. Advanced drivers grade 2 (VIP)
2. Advanced drivers grade 1 (VIP)
3. Senior drivers course.

Ningependa kufahamu ni kwanini hawaruhusu dereva kusoma kozi zote. Kwa kufuata ratiba ya kozi iliyopangwa na chuo.

Bali inamtaka dereva kusubiri mwaka mmoja. Na kisha kurudi chuoni kundelea na kozi nyingine.

Hivyo kumaliza kozi tatu ambazo jumla zina muda wa wiki 12. Inakuchukua miaka 5. Kumaliza kozi tatu tuu.

(Kwa madai ya kwamba unaifanyia kazi mwaka mmoja) Kazi mtaani hakuna hivyo unasubiri mwaka upite. Urudi kuendelea.

Ingekua pia afadhali kwa madereva kusoma kozi zote kwa mwaka mmoja. Ingepeleka pia ajira kwa baadhi ya madereva ambao vigezo hvyo ni tatizo. Na wangepata uzoefu mzuri pia. Kwasababu wamepitia shule.

Kama ni swala la uzoefu ni jukumu la mwajiri kufanya chaguzi la dereva.

  • Kusoma na kusubiri miaka yote hyoo inakatisha tamaa sanaa...
  • Allieweka huu utaratibu alikua na madhumuni gani.
  • je hizo kozi ni bora kuliko masters, kwasababu kuna watu wanamaliza digrii na kuunga masters.
-

Nifahamisheni wapendwa.

Bob lee Swagger.
Haraka haraka haina baraka
 
Habari
Naitwa fadhili natafuta kazi ya udereva mpiga kazi wala sio mzembe
Msomi yupo smart mda wote tuwasiliane
0654960981
Tembelea Jukwaa La Ajira Mara Kwa Mara Unaweza Kupata Mishe. All the Best.
 
humu jf inaonesha madereva sio wengi..

Nnogeshe kidogo, mkuu hiyo vip course asikuambia mtu ina mtonyo mrefu, ww soma uhandisi weee lakini tanesco tukikutana nakuzidi mshah, kwa tanesco dereva anagonga hadi mil1.2 hawa madereva wa vip wana mawe.......ngumu kuipata lakini simple kutumbua mihela... vumilia tu mkuuu nenda kawaulze madereva wa NSSF,PSPF,TFS,TBS,DAWASCO,WIZARANI wakuambie mitonyo yao
👏👏👏👏👏👏
 
Back
Top Bottom