Kosa kubwa wanalofanya wapinzani

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
21,441
40,534
Watanzania wameichoka CCM lakini kosa kubwa la wapinzani ni kuonesha kwamba wao ndiyo wanapambana na CCM badala ya kuwafanya watanzania wote wapambane na CCM, matokeo yake watanzania wanadhani kwamba wanaoshindwa siku zote ni wapinzani na wala wao hawahusiki.

CCM huwa inaonesha kwamba yenyewe inawakilisha matakwa mapana ya watanzania wakati wapinzani wao wanakuwa wako bize kuwaambia watanzania kwamba CCM ni mbaya na wao ni watu wema.

Watanzania wameaminishwa na wapinzani kwamba CCM ni wachafu, na hilo wamelikubali, kwa sasa ukisema kwamba CCM kuna mafisadi, watanzania hawashangai. Kwa kitendo cha wapinzani kuonekana ni wasafi, CCM wakisema wapinzani wana mafisadi watanzania wanastuka na kuchukia! Na hapo mara zote Kosa wanalolifanya wapinzani ni kushindwa kulinda utakatifu wao kinadharia!

Uchafu wote unaoumbuliwa hivi sasa na Magufuli unatokana na uendeshaji serikali uliokuwa unafanywa na Marais waliotangulia ambao wote wanatokana na CCM. Lakini leo hata kama "wanaotumbuliwa majipu" wanaonewa na watawala, wapinzani wakijaribu kuwatetea itaonekana kama wanakwenda kinyume na Uasili wao, yaani usafi. Na ni lazima wananchi watawachukia.

Kosa la wapinzani ni kujiweka kwenye nafasi ya kudumu ya kuikosoa CCM badala ya kuwa kwenye nafasi ya waendesha serikali watarajiwa. Nilikwenda kwenye Kampeni ya mgombea Ubunge mmoja wa UKAWA nikamsikia akisema "nichagueni ili niende kubweka dhidi ya serikali ya CCM" nikajisemea huyu naye kweli anaamini kwamba UKAWA itashinda na kushika dola?

Wapinzani geuzeni vita dhidi ya CCM isiwe kati yenu na CCM bali kati ya wananchi na CCM.

cc: "list of 46"
 
Kila siku stori hizihizi
Jaman tujenge nchi sasa tuache majungu yasiyo na maana
Tabia hizi za uswahil tunatoa wapi??
Tujenge umoja jaman wananchi wenye akili tunaona kinachooendelea na tunaofuatilia na kama kuihukumu ccm tutakuja kuihukumu 2020. Tumsaidie raisi kuonyesha madhaifu ayatumbue sasa kila siku stori mara za kuwaponda upinzani hazijengi tutazidi tu kubomoa umoja wetu
 
Na kibaya zaidi vyama vinajikita sana kuisema ccm ambayo imeshasemwa tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi nadhani ungekua ni wakati sasa wa vyama vya upinzani kuwaeleza wananchi sera zao na nini watawafanyia wananchi ikiwa watapewa ridhaa badala ya kubweka kila kukicha
 
Watanzania tunachotaka ni maendeleo tu sio kuwapa uongozi watu ambao kiu yao ni madaraka na si kutumikia wananchi. Yeyote anayetujali tutakuwa naye.
 
Uchafu wote unaoumbuliwa hivi sasa na Magufuli unatokana na uendeshaji serikali uliokuwa unafanywa na Marais waliotangulia ambao wote wanatokana na CCM. Lakini leo hata kama "wanaotumbuliwa majipu" wanaonewa na watawala, wapinzani wakijaribu kuwatetea itaonekana kama wanakwenda kinyume na Uasili wao, yaani usafi. Na ni lazima wananchi watawachukia.


cc: "list of 46"


Fisadi Lowasa na Sumaye unawaweka kundi gani hapo?
 
umesema kweli wapinzani walikosa ubunifu pale walipomchukua mtu waliyekuwa wanamsema ni mchafu na kuanza kuwaambia wananchi kuwa uchafu ni mfumo ni lugha ambayo mwananchi wa kawaida hawezi kuielewa ukichukulia wananchi wengi walikuwa wanakichukia ccm kwa sababu ya watu haohao waliojifanya wao ni kila kitu nchi hii.Kutokana na kosa hilo itachukua muda mrefu kwa upinzani kushika dola kwani CCM wamegundua kosa lao na wao wametumia nafasi hiyo kujiimarisha
 
Kosa la upinzani ni kubadili gea angani na kumchukua EL, Masha, Sumaye et al na kuwakabidhi wapeperushe bendera ya chama.
Hapo ndo watu wenye akili nyingi tuliposhtukia kuwa tumeibiwa mchana kweupeee
 
Kosa kubwa la upinzani, especially chama kikuu cha upinzani (Chadema) ni kushindwa kuonyesha kuwa wako tofauti na CCM iliyochokwa. Wao sasa hivi ndo vinara wa kulea na kutetea ufisadi, ndo vinara wa kung'ang'ania madaraka, ndo vinara wa kushindwa kusimamia wanachosema, wanabadili kauli kwa sababu za ajabu tu eti 'kubadilishia gia angani'. Unafikiri kwa hali hiyo wataweza kuaminiwa na watanzania wengi?
 
Watanzania wameichoka CCM lakini kosa kubwa la wapinzani ni kuonesha kwamba wao ndiyo wanapambana na CCM badala ya kuwafanya watanzania wote wapambane na CCM, matokeo yake watanzania wanadhani kwamba wanaoshindwa siku zote ni wapinzani na wala wao hawahusiki.

CCM huwa inaonesha kwamba yenyewe inawakilisha matakwa mapana ya watanzania wakati wapinzani wao wanakuwa wako bize kuwaambia watanzania kwamba CCM ni mbaya na wao ni watu wema.

Watanzania wameaminishwa na wapinzani kwamba CCM ni wachafu, na hilo wamelikubali, kwa sasa ukisema kwamba CCM kuna mafisadi, watanzania hawashangai. Kwa kitendo cha wapinzani kuonekana ni wasafi, CCM wakisema wapinzani wana mafisadi watanzania wanastuka na kuchukia! Na hapo mara zote Kosa wanalolifanya wapinzani ni kushindwa kulinda utakatifu wao kinadharia!

Uchafu wote unaoumbuliwa hivi sasa na Magufuli unatokana na uendeshaji serikali uliokuwa unafanywa na Marais waliotangulia ambao wote wanatokana na CCM. Lakini leo hata kama "wanaotumbuliwa majipu" wanaonewa na watawala, wapinzani wakijaribu kuwatetea itaonekana kama wanakwenda kinyume na Uasili wao, yaani usafi. Na ni lazima wananchi watawachukia.

Kosa la wapinzani ni kujiweka kwenye nafasi ya kudumu ya kuikosoa CCM badala ya kuwa kwenye nafasi ya waendesha serikali watarajiwa. Nilikwenda kwenye Kampeni ya mgombea Ubunge mmoja wa UKAWA nikamsikia akisema "nichagueni ili niende kubweka dhidi ya serikali ya CCM" nikajisemea huyu naye kweli anaamini kwamba UKAWA itashinda na kushika dola?

Wapinzani geuzeni vita dhidi ya CCM isiwe kati yenu na CCM bali kati ya wananchi na CCM.

cc: "list of 46"
 
Kuna watu wanataka kutuaminisha kwamba tatizo la wapinzani si kusimamia wanachokisema. Hivi waliosema wataleta Mahakama ya Kadhi walileta? Dar es salaam waliambiwa kwamba 2013 tatizo la maji kwenye jiji hilo litakuwa historia, leo shida ya maji Dar limekwisha? Tangu 1973 iliamuliwa Makao Makuu ya Serikali yawe Dodoma limetekelezeka?
 
Watanzania wameichoka CCM lakini kosa kubwa la wapinzani ni kuonesha kwamba wao ndiyo wanapambana na CCM badala ya kuwafanya watanzania wote wapambane na CCM, matokeo yake watanzania wanadhani kwamba wanaoshindwa siku zote ni wapinzani na wala wao hawahusiki.

CCM huwa inaonesha kwamba yenyewe inawakilisha matakwa mapana ya watanzania wakati wapinzani wao wanakuwa wako bize kuwaambia watanzania kwamba CCM ni mbaya na wao ni watu wema.

Watanzania wameaminishwa na wapinzani kwamba CCM ni wachafu, na hilo wamelikubali, kwa sasa ukisema kwamba CCM kuna mafisadi, watanzania hawashangai. Kwa kitendo cha wapinzani kuonekana ni wasafi, CCM wakisema wapinzani wana mafisadi watanzania wanastuka na kuchukia! Na hapo mara zote Kosa wanalolifanya wapinzani ni kushindwa kulinda utakatifu wao kinadharia!

Uchafu wote unaoumbuliwa hivi sasa na Magufuli unatokana na uendeshaji serikali uliokuwa unafanywa na Marais waliotangulia ambao wote wanatokana na CCM. Lakini leo hata kama "wanaotumbuliwa majipu" wanaonewa na watawala, wapinzani wakijaribu kuwatetea itaonekana kama wanakwenda kinyume na Uasili wao, yaani usafi. Na ni lazima wananchi watawachukia.

Kosa la wapinzani ni kujiweka kwenye nafasi ya kudumu ya kuikosoa CCM badala ya kuwa kwenye nafasi ya waendesha serikali watarajiwa. Nilikwenda kwenye Kampeni ya mgombea Ubunge mmoja wa UKAWA nikamsikia akisema "nichagueni ili niende kubweka dhidi ya serikali ya CCM" nikajisemea huyu naye kweli anaamini kwamba UKAWA itashinda na kushika dola?

Wapinzani geuzeni vita dhidi ya CCM isiwe kati yenu na CCM bali kati ya wananchi na CCM.

cc: "list of 46"
Siku zote Lengo kubwa la chama chochote cha siasa ni kushika Dora. Au hujui hilo mkuu. Haitawezekana mpinzani kukisifia chama kilichopo madarakani. Kikubwa ambacho ningeweza kusema ni kwamba sisi wananchi ambao hatunufaiki na siasa moja kwa moja haina haja ya kufuata mapenzi ya chama au ushabiki maana ndio unaotuponza
 
CCM inazifahamu namna mbalimbali za kukiri makosa inayoyafanya na kuwaangukia (kuomba radhi) wananchi inaowakosea. CCM imeweza kutengeneza chemistry nzuri sana na wananchi wa ngazi zote za maisha. Sikumshangaa rais Magufuli wakati wa kampeni alipokuwa anawasalimia wananchi wa makabila mbalimbali kwa kutumia salamu za lugha zao, ule ni mkakati mkubwa sana, yaani ujumbe ni kwamba japo CCM ina madoa mengi mno lakini bado ni chama ambacho mgombea wake anao ukaribu na hao hao waliotendewa vibaya na CCM.

Wapinzani wanatanguliza lugha za dharau kila wanapokwenda, hawajui wala hawajawahi kufahamu umuhimu wa kuwaangukia wananchi wanaokwenda kuwaomba kura. Kiburi cha wapinzani kwa mfano kimekuwa kikisikika hata baada ya JPM kuingia madarakani, waunga mkono wa UKAWA wanaandika humu JF kwamba rais wa awamu ya tano ujanja wake ni kuwasalimia wananchi kwa lugha zao lakini hajui lugha ya kingerez. Sasa hicho ni kiburi ambacho hakiwasaidii wapinzani zaidi ya kuwafanya waonekane ni watu wasiokuwa hata na ule ustaarabu wa kuwa na fikra zenye akili timamu.

Wapinzani wajipange kweli kweli ili waweze kutengeneza dira yao kuelekea 2020, watafute mtu mwenye kufanana na dira hiyo. Wajifunze kuangukia (kujishusha mbele ya wananchi). Ili uwepo wao katika sehemu nyingi za Tanzania uweze kuwapatia waungaji mkono wa pilika zao za kisiasa.
 
Kosa kubwa la upinzani, especially chama kikuu cha upinzani (Chadema) ni kushindwa kuonyesha kuwa wako tofauti na CCM iliyochokwa. Wao sasa hivi ndo vinara wa kulea na kutetea ufisadi, ndo vinara wa kung'ang'ania madaraka, ndo vinara wa kushindwa kusimamia wanachosema, wanabadili kauli kwa sababu za ajabu tu eti 'kubadilishia gia angani'. Unafikiri kwa hali hiyo wataweza kuaminiwa na watanzania wengi?
Kabisa. Na ukisema tu kuhusu UKAWA ili wajirekebisha utasikia umetumwa naLumumba wanasahau kwamba hata katika campaign ilionekana kabisa wananchi wameichoka CCM sasa kwao huo iulikuwa mtaji mkubwa sana. Sasa hawajachelewa cha muhimunm waache ubushi wasikilize ushauri:
1. Siasa za kuti=okatoka Bungeni yaani zimetuchosha mpaka basi yaani hazina tena tija si kisiasa ( kwa upande wao) wala si kimaendeleo ya wananchi
2. Wananch wanachokitaka ni maendeleo sio maneno kila siku ooh CCM mbaya cha muhimu ni kutenda na kufanya mazuri ili wewae tofauti na hao wanaowaona sio.
3. Hii tabia ya kusema mbona CCM wanafanya kama hivi iishe kabisa kwani sisi wanacnhi tunachotaka ni chama kitakachofanya mazuri na sio mbona hao wamefanya hivi. Mimi walinimaliza nguvu kabisa wakati wa uchaguzi wa Viti maalumu. Hapo wangetumia ubunifu wangewaweka kina mama mashupavu na bila upendeleo wowote wangepabnda chati sasa mabo ya yaleyale wanazidi kujumaliza.
4. Waache jazba wanapotoa hoja zao! Aidha UKAWA aandaeni semina elekezi ( Maana nasita kumwambia msamiati huu Mh. Magufuli) ili wabunge wenu wajue roles and responsibilities zao halafu na Mipaka yao la sivyo watabaki na hoja oooh mimi nimechaguliwa na wananchi, so what?!?! Watendeeni haki wananchi waliowachagua. Kuna wabunge sasa hivi wanazubaa wanasubiri Bunge watoke nje badala ya kwenda majimboni kwao kufanya kazi kama kina Mh. Prof, J. ili waweze kuwatyumikia wananchi kwa miaka mingine ijayo! Wake up guys!
 
Back
Top Bottom