Korea ya Kaskazini yaonyesha Kiburi kwa UNSC

Ben Saanane

JF-Expert Member
Jan 18, 2007
14,581
18,124
Duru Za Kimataifa: Pyongyang-Korea ya Kaskazini

Masaa machache yaliyopita Taifa la Korea ya Kaskazini limefanya majaribio mapya ya Makombora ya Masafa mafupi(Short Range Missiles) .

Jana nchi wanachama wa UN Security Council walipiga kura ya pamoja na kupitisha azimio la vikwazo vikali baada ya Urusi juzi kuchelewesha kura hiyo kwa kutaka kwanza wasome rasimu ya Azimio baada ya Kikao cha Obama na Rais Xi Jinping wa China hivyo Urusi wakataka kuona kama Maoni yao kwenye Rasimu yapo sawa kabla ya hatua ya upigaji Kura.

Jana niliandika mahali muda mfupi baada ya kusoma azimio namba 2270(2016) la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa(UNSC Resolution 2270) juu ya kuiwekea vikwazo vikali zaidi(Tough Sanctions) Korea ya Kaskazini kuwa hawa watu sio rational actor kwenye siasa za kimataifa kama Irani ya sasa na nikasema reaction ya Rais wao Kim Jong-Un inaweza kuwa ya kijeuri zaidi.

Ndivyo ilivyotokea masaa machache yaliyopita.Hapa ni sawa na kutuma ujumbe wa jeuri kwa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuonyesha hasira dhidi ya Azimio namba 2270(2016) lililolenga kuhakikisha inabanwa kurudi kwenye meza ya mazungumzo(Negotiation Table) badala yake wamejibu kwa Millitary Action .Ukaidi!

Vikwazo vinahusisha kuzuia wataalamu wa kijeshi wa Korea ya kaskazini kutoa huduma za kijeshi kama walivyofanya kufundisha jeshi la polisi la Uganda Recently,Mabenki na Taasisi za Fedha marufuku kufanya kazi na Korea ya Kaskazini,Marufuku kukodishia au kuiuzia ndege Korea ya Kaskazini,Makampuni 12 na watu 16 wamekuwa blacklisted ambao ni washirika na serikali ya Kim Jong-Un,Biashara ya mafuta na Korea marufuku,Hakuna kununua malighafi ya Chuma kutoka Korea ,Meli zote zikaguliwe na pia bidhaa za anasa kwenda Korea Marufuku na hata Magari(Trucks) ambayo yanaweza kugeuzwa kuwa magari ya kijeshi marufuku kuiuzia Korea

Je,China mshirika wa karibu atakubali kutimiza wajibu wake kutekeleza azimio dhidi ya North Korea?

Pamoja na kuwa naona kila Dalili ya Korea ya Kaskazini kuendeleza majaribio,lakini katika sheria za kimataifa jaribio lao la masaa machache yaliyopita sioni kama limekiuka sheria za kimataifa kama lile la Mwezi January maana lilivunjilia mbali Mkataba wa kudhibiti Makombora ya Masafa Marefu na ya Hatari (Anti-Ballistic Missiles Treaty)

Wakati Iran ilipowekewa Vikwazo,Tanzania ilituhumiwa kuwa meli zenye bendera yake zilitumika kukwepa Vikwazo dhidi ya Iran

Safari hii Tannzania inahitaji kuwa makini zaidi kwani Korea ya Kaskazini ni Bingwa wa Kukwepa Vikwazo.

Tayari Balozi wa Kudumu wa Marekani Umoja Wa Mataifa Samantha Power ameshatoa angalizo kuwa Korea ni Mabingwa wa Sanctions EVasion.

Aluta Continua,Victory Ascerta....

Ben Saanane
 
Ukiachana na vikwazo ivi hamna njia nyingine ya kukanyoosha hako ka bwana mdogo kwasababu hivyo vikwazo vinawaumiza wananchi lmakini sio hako ka bwana mdogo kenyewe muda wote kanabembea tu.
 
Duru Za Kimataifa: Pyongyang-Korea ya Kaskazini

Masaa machache yaliyopita Taifa la Korea ya Kaskazini limefanya majaribio mapya ya Makombora ya Masafa mafupi(Short Range Missiles) .

Jana nchi wanachama wa UN Security Council walipiga kura ya pamoja na kupitisha azimio la vikwazo vikali baada ya Urusi juzi kuchelewesha kura hiyo kwa kutaka kwanza wasome rasimu ya Azimio baada ya Kikao cha Obama na Rais Xi Jinping wa China hivyo Urusi wakataka kuona kama Maoni yao kwenye Rasimu yapo sawa kabla ya hatua ya upigaji Kura.

Jana niliandika mahali muda mfupi baada ya kusoma azimio namba 2270(2016) la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa(UNSC Resolution 2270) juu ya kuiwekea vikwazo vikali zaidi(Tough Sanctions) Korea ya Kaskazini kuwa hawa watu sio rational actor kwenye siasa za kimataifa kama Irani ya sasa na nikasema reaction ya Rais wao Kim Jong-Un inaweza kuwa ya kijeuri zaidi.

Ndivyo ilivyotokea masaa machache yaliyopita.Hapa ni sawa na kutuma ujumbe wa jeuri kwa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuonyesha hasira dhidi ya Azimio namba 2270(2016) lililolenga kuhakikisha inabanwa kurudi kwenye meza ya mazungumzo(Negotiation Table) badala yake wamejibu kwa Millitary Action .Ukaidi!

Vikwazo vinahusisha kuzuia wataalamu wa kijeshi wa Korea ya kaskazini kutoa huduma za kijeshi kama walivyofanya kufundisha jeshi la polisi la Uganda Recently,Mabenki na Taasisi za Fedha marufuku kufanya kazi na Korea ya Kaskazini,Marufuku kukodishia au kuiuzia ndege Korea ya Kaskazini,Makampuni 12 na watu 16 wamekuwa blacklisted ambao ni washirika na serikali ya Kim Jong-Un,Biashara ya mafuta na Korea marufuku,Hakuna kununua malighafi ya Chuma kutoka Korea ,Meli zote zikaguliwe na pia bidhaa za anasa kwenda Korea Marufuku na hata Magari(Trucks) ambayo yanaweza kugeuzwa kuwa magari ya kijeshi marufuku kuiuzia Korea

Je,China mshirika wa karibu atakubali kutimiza wajibu wake kutekeleza azimio dhidi ya North Korea?

Pamoja na kuwa naona kila Dalili ya Korea ya Kaskazini kuendeleza majaribio,lakini katika sheria za kimataifa jaribio lao la masaa machache yaliyopita sioni kama limekiuka sheria za kimataifa kama lile la Mwezi January maana lilivunjilia mbali Mkataba wa kudhibiti Makombora ya Masafa Marefu na ya Hatari (Anti-Ballistic Missiles Treaty)

Wakati Iran ilipowekewa Vikwazo,Tanzania ilituhumiwa kuwa meli zenye bendera yake zilitumika kukwepa Vikwazo dhidi ya Iran

Safari hii Tannzania inahitaji kuwa makini zaidi kwani Korea ya Kaskazini ni Bingwa wa Kukwepa Vikwazo.

Tayari Balozi wa Kudumu wa Marekani Umoja Wa Mataifa Samantha Power ameshatoa angalizo kuwa Korea ni Mabingwa wa Sanctions EVasion.

Aluta Continua,Victory Ascerta....

Ben Saanane
Kumbe upo vizuri huku mkuu ila sanction ni propaganda tuu
 
Ila kusema ukweli vikwazo vya safari hii kiboko sijui hali ya wananchi itakuaje mAana wameBAN almost evrthin kasoro food and medicine....me naona bora warud kwenye meza ya mazungumzo maana ht huyo baba yao CHINA kashawageuka
 
Duuh ila huyo dogo wa north n mtabe sasa south nayo ijipange maana ma spy wa north wataanza kazi ..kule kupata wasicho nacho
 
Sometimes necessary just to alert big powered states not to feel that, they are alone in this world.
 
sanctions ni propaganda tu and they have never worked anywhere. the problem is whenever they run for sanctions only the poor suffer and not the politicians, it is time now for the UN to revisit its sanctions policy because they have no any significance but rather are tools for injustice to the poor.
 
sheri za kimataifa zipi,si waseme tu sheria za marekani ( USA),alafu eti wanawekewa saction ya kuwapelekea magari,hivi hawa watu wanatengeneza ( Missiles) watashindwa kutengeneza gari na bado nchi yao inazalisha chuma.
 
sheri za kimataifa zipi,si waseme tu sheria za marekani ( USA),alafu eti wanawekewa saction ya kuwapelekea magari,hivi hawa watu wanatengeneza ( Missiles) watashindwa kutengeneza gari na bado nchi yao inazalisha chuma.
Mkuu umeongea point sana.

Hawa North Koreans wameweza kutengeneza satellites na kuweza kuzirusha (kwa kutumia technology ya rockets) na kuweza kuziweka hizo satellites kwenye orbits vizuri kabisa pasipo shaka. Na wamefanya hivyo pasipo msaada wa hao USA (vinara wa vikwazo)

Na North Korea yupo kwenye vikwazo for decades. Lakini wamezidi kusonga mbele. Kwa hiyo hivi vikwazo vipya ni propaganda tu. Na ndio maana vimejibiwa kwa military action.
 
Ila kusema ukweli vikwazo vya safari hii kiboko sijui hali ya wananchi itakuaje mAana wameBAN almost evrthin kasoro food and medicine....me naona bora warud kwenye meza ya mazungumzo maana ht huyo baba yao CHINA kashawageuka
unafikiri kim jong un anajali wananchi wake basi! yy akishiba tu nakupata ela ya kutengezeneza silaha basi maisha yanasonga....yule jamaaa hajali habari za watu kuishi magum aisee mwehu sana yule
 
sheri za kimataifa zipi,si waseme tu sheria za marekani ( USA),alafu eti wanawekewa saction ya kuwapelekea magari,hivi hawa watu wanatengeneza ( Missiles) watashindwa kutengeneza gari na bado nchi yao inazalisha chuma.
mkuu umeisoma ile UNHSC vizuri?? zile sanctio ztazid kuumiza sana uchumi wa north korea,,kumbuka nowuchumiwaoukohoisana kiac kwamba ili kuendesha shughulizakila siku za kijeshi bajet ya wizara yao ya ulinzi ni zaidi ya 25% ya total GDP yao so kimsingihizi sanctions zitwaumiza,kumbuka miez sitailiopita waliiandikia barua marekani wazungumze ili wawaondolee vikwazo kwakuwa vinawaumiza...sasa hivi vya safar hii ambavyo mchina ameshiriki kuvitunga ni vikali zaidi
 
Hizo sanctions zinawapa wa NK fursa ya kujitathmini na kujitosheleza zaidi. Ila ifike mahala Amerika nayo iheshimu maamuzi ya nchi zingine. Wao wanazo silaha hizo, kwanini wengine wasiwe nazo?
 
Ukiachana na vikwazo ivi hamna njia nyingine ya kukanyoosha hako ka bwana mdogo kwasababu hivyo vikwazo vinawaumiza wananchi lmakini sio hako ka bwana mdogo kenyewe muda wote kanabembea tu.

kungekuwa na mafuta kama mashariki ya kati wangeshaingia kitaaaamboo... na midege yao ya vita .. tatizo jamaa ni maskini hana lolote
 
mkuu umeisoma ile UNHSC vizuri?? zile sanctio ztazid kuumiza sana uchumi wa north korea,,kumbuka nowuchumiwaoukohoisana kiac kwamba ili kuendesha shughulizakila siku za kijeshi bajet ya wizara yao ya ulinzi ni zaidi ya 25% ya total GDP yao so kimsingihizi sanctions zitwaumiza,kumbuka miez sitailiopita waliiandikia barua marekani wazungumze ili wawaondolee vikwazo kwakuwa vinawaumiza...sasa hivi vya safar hii ambavyo mchina ameshiriki kuvitunga ni vikali zaidi
kama hivyo vikwazo vinaumiza uchumi wao kwa namna yoyote wangekuwa walishafanya kama wanavyo ambiwa na UNHSC,na kama vitakuwa vinawaumiza na hawataki kuacha jua kuna mawili either ni propaganda zinasambazwa na western countries kuwa uchumi wa korea ni mbovu au kuna kitu wanakihofu ambacho kitawaangamiza zaidi-kwa hiyo wanaona kwao ni bora kuwekewa vikwazo kuliko kukubaliana na matakwa ya UNHSC
 
kama hivyo vikwazo vinaumiza uchumi wao kwa namna yoyote wangekuwa walishafanya kama wanavyo ambiwa na UNHSC,na kama vitakuwa vinawaumiza na hawataki kuacha jua kuna mawili either ni propaganda zinasambazwa na western countries kuwa uchumi wa korea ni mbovu au kuna kitu wanakihofu ambacho kitawaangamiza zaidi-kwa hiyo wanaona kwao ni bora kuwekewa vikwazo kuliko kukubaliana na matakwa ya UNHSC
Vikwazo vinaumiza wewe Ila tyu dogo mbishi hasa hivi vya safari hii mpk China kalalamikia inaweza kupata wakimbiz weng kutoka NK...na Vikwazo vya this time vimeBAN hadi fuel,gold,coal export,n.k
 
Ukiachana na vikwazo ivi hamna njia nyingine ya kukanyoosha hako ka bwana mdogo kwasababu hivyo vikwazo vinawaumiza wananchi lmakini sio hako ka bwana mdogo kenyewe muda wote kanabembea tu.

Wanakanyoosha kwa kosa gani linalozidi kuivamia Libya na Iraq?
 
Back
Top Bottom