Kodi ya VAT

Kodi ya VAT

ndiuka

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2009
Posts
699
Reaction score
825
Wakuu,

Kwa wale wataalamu wa masuala ya kodi naomba kuelimishwa je ni mfanyabiashara wa aina gani anapaswa kulipa VAT tra?

Mfano: mfanya biashara anaesupply chakula shuleni kwa mtaji wa milioni 2 na risit anatoa za efd na Hana kampuni amesajili business name tu halmashauri, je baada ya kulipwa anastahili kulipa VAT tra?
 
Wakuu,

Kwa wale wataalamu wa masuala ya kodi naomba kuelimishwa je ni mfanyabiashara wa aina gani anapaswa kulipa VAT tra?

Mfano: mfanya biashara anaesupply chakula shuleni kwa mtaji wa milioni 2 na risit anatoa za efd na Hana kampuni amesajili business name tu halmashauri, je baada ya kulipwa anastahili kulipa VAT tra?
Kwa mwezi mauzo yako ni kiasi gani? Umeanza kusupply toka lini?

Umeuliza usaidiwe naomba usidanganye.
 
Wakuu,

Kwa wale wataalamu wa masuala ya kodi naomba kuelimishwa je ni mfanyabiashara wa aina gani anapaswa kulipa VAT tra?

Mfano: mfanya biashara anaesupply chakula shuleni kwa mtaji wa milioni 2 na risit anatoa za efd na Hana kampuni amesajili business name tu halmashauri, je baada ya kulipwa anastahili kulipa VAT tra?
Ili uweze kukusanya VAT sharti la kwanza ni kusajiliwa. Kuna vigezo vimewekwa ambavyo ukivikidhi utasajiliwa kukusanya na kuwakilisha ritani zako TRA. Kikubwa ni kwamba kama biashara yako haina turnover inayozidi 100M kwa mwaka na hiyo biashara haipo kwenye list ya biashara ambazo ni lazima zisajiliwe VAT basi huna vigezo vya kukusanya (kutoza) wala kuwakilisha ritani za VAT kwa mamlaka. Mfano wa biashara ambayo ni lazima isajiliwe VAT ni biashara inayohusu mambo ya utalii
 
Wakuu,

Kwa wale wataalamu wa masuala ya kodi naomba kuelimishwa je ni mfanyabiashara wa aina gani anapaswa kulipa VAT tra?

Mfano: mfanya biashara anaesupply chakula shuleni kwa mtaji wa milioni 2 na risit anatoa za efd na Hana kampuni amesajili business name tu halmashauri, je baada ya kulipwa anastahili kulipa VAT tra?

Kuna vigezo viwili (2) vikubwa vya kusajiliwa VAT;

1. Mauzo ghafi ya biashara (turnover) yako kwa mwaka yawe Tshs 100million na kuendelea

2. Bidhaa au huduma unayouza/kutoa iwe haijasemehewa (exempted) kwenye sheria ya VAT

Sijafaham una-supply chakula gani katika hayo mashule, but kama ni NAFAKA hizo karibu zote ziko EXEMPTED. Ila kama ni MIKATE na mauzo kwa mwaka ni 100+million, unakidhi kusajiliwa VAT

Ahsante.
 
Back
Top Bottom