Koboko (black mamba) ana kiburi, jeuri na dharau sana ila nitamfundisha adabu

yule hupaswi kumsogelea... nitamuua kesho.
 
Huna adabu kijana yani umeshampa jina la koboko,
Kwanini ulazimishe kupita hiyo njia wakati kuna koboko na unaifahamu hatari yake..
Alafu amekupa onyo baso husikii..
Umemzidi umri lakini pumbavu inakuja tu yenyewe harakaharaka
 
Duuuuuh..mkuu kuwa makini..huyo kiumbe msikie tu
Mimi nilipo kwasasa ni nje ya mji na hao jamaa wanaishi jirani tu kama mita 200 kutoka kwenye makazi ya watu...kuna mchunga ng’ombe alipita na mifugo yake ikawa kero kwa wajomba ..huwezi amini baada ya dakika 40 ng’ombe 20 walikuwa walipotoka kabla hawajaja duniani..
 
Koboko ana sumu ya kuua ngombe wazima mia moja na hamsini. Sumu yake nusu saa haiishi. Ana spidi kuliko gari inayopita kwenye rough road- km 25 kwa saa. Kwa hiyo akiamua kukufuata ukikimbia anakudunga faster. Njia pekee ya kumuua sio fimbo- ni kubeba chungu kilicho wazi cha uji wa moto kichwani. Akiwa kwenye mti atapenda kukudunga utosini. Akiruka akudunge anatumbukia kwenye uji wa moto anakufa. Lakini hilo linahitaji ujasiri wa kipekee. Ukimwendea na fimbo utakuwa marehemu ndani ya dk 29
 
Ukienda kumua usisahau kuchukua video ili kutuaminisha zaidi...,
 
Yaani mkuu kwenye battle unayotaka kuizua na huyo kiumbe sikushauri maana angekuwa anaweza kupiga picha yeye ndio angeleta mrejesho alivo kudedisha wewe.
 
Huna adabu kijana yani umeshampa jina la koboko,
Kwanini ulazimishe kupita hiyo njia wakati kuna koboko na unaifahamu hatari yake..
Alafu amekupa onyo baso husikii..
Umemzidi umri lakini pumbavu inakuja tu yenyewe harakaharaka
Afadhari yako umejaribu kuvunja li code maana wengi wameshindwa hata kutambua kua sio nyoka koboko bali ni mtu. Mimi mwrnyewe sijamjua ila ukicheki maelezo ya mtoa maada unaona kabisa haongelei nyoka halisi bali mtu
 
Zamani sana niliwahi kumkuta kwenye ka kichaka fulani hivi lakini nilikuwa cjajua kama ni yeye, nikaanza kumrushia mawe na fimbo yeye akawa anajirudisha nyuma na mi namfuata, ghafla nikastukia nanyakuliwa navutwa kwa nguvu kurudishwa nyuma, wakati bado nashanga shangaa nikatulizwa na vibao viwili matata sana, akili kuja kukaa sawa nikamsikia aliyenivuta anasema (mama mmoja hivi hata simjui) we mtoto mjinga sana, hivi KOBOKO ni kuchezea hivyo unadhani huyo ni kifutu eeh (KIFUTU ni yale manyoka manene ambayo ni nadra sana kukuuma, lakini likikuuma unaoza kwa haraka sana kuanzia pale ulipoumwa)

Kumbe lile dude wakati linarudi nyuma lilikuwa limeshakasirika, basi ile jioni tukasikia kwenye ka kichaka kalekale mbuzi 12,ngombe 2, kondoo 4 na mchungaji wao walikuwa wamepoteza maisha, basi yule mama aliyeniokoa pale kimiujiza akaja kusema nyumbani......nikajikuta nachezea kipigo kizito kutoka kwa mama, halafu baadae ndio akanipa darasa kuhusu hilo DUBWASHA......ndugu yangu wewe nakusihi tu ungeachana na huo ujinga unaotaka kujaribu kuufanya
 
Hahahahahahaa pole sana mkuu japo mtoa maada hananishi nyoka halisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…