Viwanja vile viliuzwa kwa watumishi wa serikali kwa milioni za kitanzania 32. Na kwa sheria, mmiliki haruhusiwi kubadilisha jina kwenye hati au kukichukulia mkopo benki kwa muda wa miaka 25, ingawa wapo wengi wanaochakachua sheria hiyo; inawezekana huyo anayekiuza ni mtumishi aliyejichokea kimaisha, anaona isiwe tabu, akamate mamilioni yake akajenge nyumba yake kinyerezi au boko, na kuanzisha mradi wa kuku, boda boda n.k, ili mradi siku ziende. Vinginevyo kuna faida gani kuishi katika nyumba mbele ya ufukwe wa bahari, maeneo ya uzunguni, huku hauna hata senti tano mfukoni baada ya kustaafu ukurugenzi wa idara ya nyuki wizara ya maliasili au mkurugenzi wa ajira, wizara ya vijana?