Hili la regulations hapana. Tanzania tupo hapa kwenye huu umasikini kwa kutokuwa na regulations ambazo haziko wazi na nyingi ambazo hazifahamiki vizuri na watumiaji. Ajali nyingi zinatokea kwa sababu ya wengi kutokujua sheria zinasemaje. Nilikuwa Tanzania kwa mfano dreva niliyekuwa nae alipita kwenye Zebra crossing wakati watembea kwa miguu walikuwa wanataka kuvuka barabara nikamuuliza kwa nini hakusimama. Akasema sio lazima, sasa hapa unajenga au unabomoa? We need regulations ambazo zisipotekelezwa lazima ziwe na meno makali.
Ajali nyingi zinazotokea hazikupaswa kuwa na maafa na tunapoteza Watanzania wengi kwa uzembe.
Kuhusu shule hapo napo lazima tuwe makini, Je, tunataka shule ziote kama uyoga bila regulations? Hili linanikumbusha jinsi bureau de change zilivyokuwa nyingi Bandari salama lakini ukweli zilikuwa zinatapeli pesa za Serikali kwa kufanya biashara. Bank zilikuwa zinaota kama uyoga lakini chini ya JPM ameweka sheria kali ndio sababu exchange rate ya Tsh imetengemaa (Regulation). Sheria zetu ziwe za kufanya shughuli au biashara ziwe madhubuti zaidi.
Swala la Banks kutokuwa na foleni nafikiri ni kwa sababu ya mobile money.
Kuhusu private school ratio/walimu, kulikuwa na tatizo kubwa kwenye elimu lakini naona Serikali inaliangalia hilo kwa macho mawili. Kuna Private schools nafikiri quality yake sio sawa na kile wanacho-charge. Hili ni tatizo lakini halina njia ya haraka kulitatua. Tunahitaji walimu qualified kufundisha masomo ambayo wanayaelewa vizuri, vile vile nafikiri Serikali ijitahidi katika ukaguzi kuona kwamba walimu wanafahamu vizuri kile wanachofundisha kwa sababu ukiwa na mwalimu mbovu usitegemee kuwa na wanafunzi bora. Kwenye elimu mimi nilisha toa maoni nafikiri yamo humu JF. TZ wawe na mkakati wa kuwapeleka wanafunzi kama 500-1000 kusoma nje hasa kwenye vyuo vikuu vya UK, USA and (Canada), Germany, Japan, Sweden, China and Russia. Vile vile kukuza exchange co-operation na vyuo vya nje.