Kituo cha afya kata ya Rabuor wilayani Rorya kiko taabani

Kituo cha afya kata ya Rabuor wilayani Rorya kiko taabani

Sango Ochwera

Member
Joined
Mar 20, 2013
Posts
98
Reaction score
26
Wakati wananchi wilayani Rorya mkoa wa Mara wakiendelea kuvuta subira kuelekea maisha bora kwa kila mtanzania,hali ya huduma za afya wilayani humo inazidi kuwa mbaya kila kukicha.

Kituo cha afya cha kata ya Rabuor Tarafa ya Luo imbo ambacho kinahudumia wakazi wapatao 13626 kutoka vijiji vya makongoro,rabuor na oliyo hakina dawa kwa zaidi ya miezi mitatu sasa.

Sambamba na ukosefu huo wa dawa,kituo hiki hakina wataalamu kama clinical officer(co),nurse,labaratory technician na assistant labaratory technician.Kutokana na hali hiyo wananchi wanaofika kituoni hapo kupata matibabu husikilizwa maelezo yao na kisha huandikiwa dawa na kutakiwa kwenda kununua.

Aidha kituo hiki cha afya kina upungufu mkubwa wa samani kiasi cha wahudumu wachache waliopo kutumia madumu ya mafuta ya kula ya ujazo wa lita 20 kama viti.


Source:mimi mwenyewe.
 
Hakoka hiyo ndio hali halisi omera hata mitaa ya mika, ingri na utegi nilipopata kuishi
 
Wakati wananchi wilayani Rorya mkoa wa Mara wakiendelea kuvuta subira kuelekea maisha bora kwa kila mtanzania,hali ya huduma za afya wilayani humo inazidi kuwa mbaya kila kukicha.

Kituo cha afya cha kata ya Rabuor Tarafa ya Luo imbo ambacho kinahudumia wakazi wapatao 13626 kutoka vijiji vya makongoro,rabuor na oliyo hakina dawa kwa zaidi ya miezi mitatu sasa.

Sambamba na ukosefu huo wa dawa,kituo hiki hakina wataalamu kama clinical officer(co),nurse,labaratory technician na assistant labaratory technician.Kutokana na hali hiyo wananchi wanaofika kituoni hapo kupata matibabu husikilizwa maelezo yao na kisha huandikiwa dawa na kutakiwa kwenda kununua.

Aidha kituo hiki cha afya kina upungufu mkubwa wa samani kiasi cha wahudumu wachache waliopo kutumia madumu ya mafuta ya kula ya ujazo wa lita 20 kama viti.


Source:mimi mwenyewe.


si wanakusanya cost sharing/chf, kwa nini wasinunue ata ivyo viti tu.
 
osyepuna hayo ndo mliyataka kwani nimekutana na mbunge wenu lameck(ccm)
anasema mpaka arudishe pesa yake aliyowahonga wakt wa uchaguzi ndo mpate
dawa zaidi ya hapo mta r.i.p CCM OYEEE
 
Back
Top Bottom