Ta Kamugisha
JF-Expert Member
- May 17, 2011
- 3,536
- 2,187
Enzi za shule ya Msingi, nilikuwa napenda sana michezo mimi na mdogo wangu, ingawa mzee alikuwa hapendi tuwe tunachelewa kutoka kucheza mpira maana alikuwa Mjeda JWTZ
Ila tulikuwa na tabia ya kuiba Ice cream, kwa jina maarufu ziliitwa "ashikilimu" nadhani wote mnazifaham. Tulikuwa tunaziiba tulipokuwa tunataka kwenda kuoga maana friji ilikuwa inakaa kwa mfanyakazi "House Girl"
Tulipigwa marufuku kula Ashikilimu kwa sababu ya kifua, si unajua utoto ukikatazwa kitu ndio kwanza unatengeneza njia ya kukifanya ulichokatazwa
Sasa basi, siku za mwizi ni 40, maana ilikuwa ni desturi yetu kuiba ashikilimu kila siku na kwenda kuzilia bafuni, hapa naongelea miaka 90's. Maana tulipendelea kuogea bafu la nje ili tujinafasi na ashikilimu zetu, ukiiba nyingi unakula nyingi.
Siku hiyo tumezama chumba cha house girl kumbe Mjeshi yupo dirishani anatuchora maana dirisha lilikuwa halijafungwa na sisi tulimuacha nje ya geti anaosha gari lake, tukachukua zile ashikilimu tukazibana na taulo kwenye tumbo au kiunoni kila mmoja tukaiba tatu tatu, ukishaziiba unazifunga vzr kiunoni na kutoka speed mpaka bafuni.
Ukishaziweka kiunoni unatakiwa utoke nduki ya hatari mpaka bafuni maana zinachoma kwa ubaridi si unajua barafu inavyochoma!!!
Kumbe mjeshi anatuchora tu dirisha maana pazia hatukuzifunga, ile tunatoka nje kwa speed ya umeme ili tuwai bafuni, mara mjeshi akatusimamisha.....kah....
Dah ilikuwa hatari, akaaza kutuuliza maswali madogo madogo....kwanini mmechelewa kuoga?....kwanini mmechelewa toka uwanjani? .....shuleni mmesoma nini? Yaani alituhoji maswali kama dakika 10......
Aisee uku sisi tunacheza mguu pande...mguu sawa maana barafu zilikuwa zinaunguza balaaa, uzalendo ukatushinda aisee tukazitupa chini.....
Mjeshi sasa....akasema hii ndio nilitaka kuona maana nilijua zitawaunguza tu.....zilituchoma mpaka tukauza Ramani ya vita kwa Mjeshi....
Babaaaake tulikula mboko za hatari, maana nyuma kulikuwa na mnazi, alitufunga kwenye mnazi na tukala mboko za maana, maana hata sijui tulikula mboko ngapi, na tukapewa adhabu ya kulala bila kula...ila tulichezea kichapo cha mbwa koko
Ila house girl alicheza kama pele, aliposikia tunapewa adhabu ya kulala bila kula, alipakua ubwabwa fasta , sahani mbili za ubwabwa akaenda kuziweka chini ya kitanda....tukafunguliwa kwenye mnazi maana alitaka tulale pale pale kwenye mnazi, Bi mkubwa akatutetea sana, tukaenda kulala zetu ndani, mara House girl akatugongea kwenye dirisha....Ta kamugisha ebu angalieni uvunguni mwa Kitanda..
Mara paaa wali ndondo, tuliula na kucheka sana .....na kumshukuru house Girl wetu, kuànzia siku hiyo atukuiba tena Ashikilimu, maana mboko za mjeshi zilikuwa matata sana aisee....si mnazijua mboka za maafande!!!
Hiki kisa mpaka leo siwezi kukisahau maana Ashikilimu zilituchoma mpaka tukauza Ramani ya vita kwa Mjeshi wa JWTZ
Ila tulikuwa na tabia ya kuiba Ice cream, kwa jina maarufu ziliitwa "ashikilimu" nadhani wote mnazifaham. Tulikuwa tunaziiba tulipokuwa tunataka kwenda kuoga maana friji ilikuwa inakaa kwa mfanyakazi "House Girl"
Tulipigwa marufuku kula Ashikilimu kwa sababu ya kifua, si unajua utoto ukikatazwa kitu ndio kwanza unatengeneza njia ya kukifanya ulichokatazwa
Sasa basi, siku za mwizi ni 40, maana ilikuwa ni desturi yetu kuiba ashikilimu kila siku na kwenda kuzilia bafuni, hapa naongelea miaka 90's. Maana tulipendelea kuogea bafu la nje ili tujinafasi na ashikilimu zetu, ukiiba nyingi unakula nyingi.
Siku hiyo tumezama chumba cha house girl kumbe Mjeshi yupo dirishani anatuchora maana dirisha lilikuwa halijafungwa na sisi tulimuacha nje ya geti anaosha gari lake, tukachukua zile ashikilimu tukazibana na taulo kwenye tumbo au kiunoni kila mmoja tukaiba tatu tatu, ukishaziiba unazifunga vzr kiunoni na kutoka speed mpaka bafuni.
Ukishaziweka kiunoni unatakiwa utoke nduki ya hatari mpaka bafuni maana zinachoma kwa ubaridi si unajua barafu inavyochoma!!!
Kumbe mjeshi anatuchora tu dirisha maana pazia hatukuzifunga, ile tunatoka nje kwa speed ya umeme ili tuwai bafuni, mara mjeshi akatusimamisha.....kah....
Dah ilikuwa hatari, akaaza kutuuliza maswali madogo madogo....kwanini mmechelewa kuoga?....kwanini mmechelewa toka uwanjani? .....shuleni mmesoma nini? Yaani alituhoji maswali kama dakika 10......
Aisee uku sisi tunacheza mguu pande...mguu sawa maana barafu zilikuwa zinaunguza balaaa, uzalendo ukatushinda aisee tukazitupa chini.....
Mjeshi sasa....akasema hii ndio nilitaka kuona maana nilijua zitawaunguza tu.....zilituchoma mpaka tukauza Ramani ya vita kwa Mjeshi....
Babaaaake tulikula mboko za hatari, maana nyuma kulikuwa na mnazi, alitufunga kwenye mnazi na tukala mboko za maana, maana hata sijui tulikula mboko ngapi, na tukapewa adhabu ya kulala bila kula...ila tulichezea kichapo cha mbwa koko
Ila house girl alicheza kama pele, aliposikia tunapewa adhabu ya kulala bila kula, alipakua ubwabwa fasta , sahani mbili za ubwabwa akaenda kuziweka chini ya kitanda....tukafunguliwa kwenye mnazi maana alitaka tulale pale pale kwenye mnazi, Bi mkubwa akatutetea sana, tukaenda kulala zetu ndani, mara House girl akatugongea kwenye dirisha....Ta kamugisha ebu angalieni uvunguni mwa Kitanda..
Mara paaa wali ndondo, tuliula na kucheka sana .....na kumshukuru house Girl wetu, kuànzia siku hiyo atukuiba tena Ashikilimu, maana mboko za mjeshi zilikuwa matata sana aisee....si mnazijua mboka za maafande!!!
Hiki kisa mpaka leo siwezi kukisahau maana Ashikilimu zilituchoma mpaka tukauza Ramani ya vita kwa Mjeshi wa JWTZ