KITU CHA KUFANYA PALE WATU AMBAPO HAWAKUAMINI KAMA UNAWEZA KUFANYA

Galacha Maestro

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
1,353
2,229
KITU CHA KUFANYA PALE WATU AMBAPO HAWAKUAMINI KAMA UNAWEZA KUFANYA
Kama unataka kufanya jambo jipya, kama unataka kufanya jambo
tofauti na wengine walivyozoea kufanya, naweza nikakuhakikishia jambo moja, WATU HAWATAKUAMINI.
Watu hawatakuamini kwamba unaweza kufanya jambo hilo.
Watu hawatakuamini kwamba kuna uwezekano wa jambo hilo kufanyika kwa tofauti.
Na hapa ndipo watu wengi hukata tamaa na kuamua kuacha. Na hivyo watu wale walioshindwa kuwaamini mwanzo wanakuwa sahihi na wanazidi kupata nguvu ya kuwaambia wengine kwamba hawawezi au haiwezekani.
Leo nataka nikuulize, je unajua unatakiwa kufanya nini pale ambapo watu hawakuamini kwamba unaweza?
Au umekuwa mtu wa kukatishwa tamaa mara nyingi na wewe kukubali?
Sasa kuna kitu kimoja muhimu sana unachotakiwa kufanya pale ambapo watu hawakuamini kama unaweza.
JIAMINI WEWE MWENYEWE.
Wewe ndio umekuja na mawazo hayo uliyonayo, wewe ndiye ambaye umekuwa unafikiria usiku na mchana jinsi unavyoweza kubadili hali ya mambo. Wewe ndiye uliyefikiria na kuona kuna njia mbadala na ambayo inawezekana.
Sasa kwa nini ukubali kumsikiliza mtu ambaye amefikiria kwa upande mmoja tu wa kwamba vitu haviwezekani?
Kama utawasikiliza watu hawa utakuwa hujajitendea haki kabisa,
kwa sababu hata watu hawa sio kwamba wana uhakika haiwezekani, ni vile tu hawajawahi kuona mtu mwingine akifanya hicho unachotarajia kufanya.
Kama watu hawaamini kwamba unaweza, huo ndio wakati wa kujiamini
na hata kufurahia sana kwenye maisha yako. Unajua ni kwa nini? Kwa sababu
unapoanza kufanya kitu ambacho wengi wanaona hakiwezekani, jua unafanya kitu
ambacho sio cha kawaida, unafanya kitu kikubwa.
Na mafanikio yanakuja kwa kufanya vitu ambavyo sio vya kawaida.
 
Kazi ndio kipimo cha Utu,

Eeeh bwana weee jina kubwa sana hili na sijui kama wengi tunalichukulia uzito wake.

Na hakika nakubaliana na wewe sana toka jina ambalo limefaa sana kulingana na kijiwe hiki. Bila kazi hakuna utu, bila kazi hakuna uzalishaji na wala hilo neno biashara na uchumi zitabaki hadithi za simulizi....

Tunarudi kulekule ktk swali letu la Uhuru, ikiwa Afrika na hasa TZ bado hatujapata Uhuru zaidi ya huo wa hewa, tutaijenga vipi nchi yetu na imani ya Utandawazi?
Jamberi,

Ndugu yangu hakika umenipa somo!...

Maelezo yako yanatisha pamoja na kwamba ndio ukweli wenyewe...Kusema kweli Afrika kila kiongozi huingia Ikulu kutatua matatizo yaliyoachwa na kiongozi aliyemtangulia...Leo hii tunaona JK akijifunga kibwebwe kufagia machafu yote ya Mkapa, wala hatufahamu itachukua muda gani ufagizi huu na kwa kipindi gani patakuwa safi!... Hapo hapo hakuna maandalizi la kuhakikisha uchafu huo haurudi tena yaani ufagiaji unatupiwa chini ya uvungu. wakati zoezi la kusaka majambazi linaendelea Dar huko mikoani hakuna kitu.. yaani majambazi yanakimbia na kujichimbia bara. Hakuna mpango wa kuhakikisha wananchi wanapewa vitambulisho vya uraia nje ya passport!..hatuna data base ya aina yeyote zaidi ya akaunti ktk benki zetu. Hakuna jitihada za kuhakikisha mishahara haitolewi kwa fedha taslimu na wazawa wanapewa nafasi kwanza mbele ya mgeni. Vitu kama hivi vidogo vidogo lakini vinaweza kabisa kuleta mabadiliko makubwa.

Nafikiri, kulingana na maelezo yako hapo juu kuhusu Uhuru wetu, labda dawa - Watawala wa wilaya hadi mikoa wanatakiwa warudi ma-chief ambao walikuwa na uchungu na himaya zao na kulingana na tamaduni za mwafrika nimegundua kwamba kila kiongozi aliyeshika madaraka (rais na mawaziri) ameweza kuleta mabadiliko kwao zaidi. Sio rais wala waziri wote wamejenga makwao na wale ambao hawakufanya hivyo basi wamejenga kwa mke ambako kapewa ufalme mdogo wa nyumba. Kuna haja ya kuwa na senate inayoongozwa na machief badala ya viongizi wa vyama vya kisiasa ambao wanazidi kututenganisha siku hadi siku.
Asant kwa kusoma.
 
Kazi ndio kipimo cha Utu,

Eeeh bwana weee jina kubwa sana hili na sijui kama wengi tunalichukulia uzito wake.

Na hakika nakubaliana na wewe sana toka jina ambalo limefaa sana kulingana na kijiwe hiki. Bila kazi hakuna utu, bila kazi hakuna uzalishaji na wala hilo neno biashara na uchumi zitabaki hadithi za simulizi....

Tunarudi kulekule ktk swali letu la Uhuru, ikiwa Afrika na hasa TZ bado hatujapata Uhuru zaidi ya huo wa hewa, tutaijenga vipi nchi yetu na imani ya Utandawazi?
Jamberi,

Ndugu yangu hakika umenipa somo!...

Maelezo yako yanatisha pamoja na kwamba ndio ukweli wenyewe...Kusema kweli Afrika kila kiongozi huingia Ikulu kutatua matatizo yaliyoachwa na kiongozi aliyemtangulia...Leo hii tunaona JK akijifunga kibwebwe kufagia machafu yote ya Mkapa, wala hatufahamu itachukua muda gani ufagizi huu na kwa kipindi gani patakuwa safi!... Hapo hapo hakuna maandalizi la kuhakikisha uchafu huo haurudi tena yaani ufagiaji unatupiwa chini ya uvungu. wakati zoezi la kusaka majambazi linaendelea Dar huko mikoani hakuna kitu.. yaani majambazi yanakimbia na kujichimbia bara. Hakuna mpango wa kuhakikisha wananchi wanapewa vitambulisho vya uraia nje ya passport!..hatuna data base ya aina yeyote zaidi ya akaunti ktk benki zetu. Hakuna jitihada za kuhakikisha mishahara haitolewi kwa fedha taslimu na wazawa wanapewa nafasi kwanza mbele ya mgeni. Vitu kama hivi vidogo vidogo lakini vinaweza kabisa kuleta mabadiliko makubwa.

Nafikiri, kulingana na maelezo yako hapo juu kuhusu Uhuru wetu, labda dawa - Watawala wa wilaya hadi mikoa wanatakiwa warudi ma-chief ambao walikuwa na uchungu na himaya zao na kulingana na tamaduni za mwafrika nimegundua kwamba kila kiongozi aliyeshika madaraka (rais na mawaziri) ameweza kuleta mabadiliko kwao zaidi. Sio rais wala waziri wote wamejenga makwao na wale ambao hawakufanya hivyo basi wamejenga kwa mke ambako kapewa ufalme mdogo wa nyumba. Kuna haja ya kuwa na senate inayoongozwa na machief badala ya viongizi wa vyama vya kisiasa ambao wanazidi kututenganisha siku hadi siku.
Asante kwa kusoma.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom