DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mchezo wa Dabi nchini Libya kati ya Al-Ahli Tripol dhidi ya Al-Ittihad ulisimama katika dakika ya 39 baada ya Mashabiki wa Al-Ahli kuvamia uwanja kupinga goli la kutangulia la Al Ittihad.
Mwamuzi kutoka nchini Ureno Fábio José Costa, alijeruhiwa na mchezaji wa akiba na Mwamuzi akakataa kuendelea na mechi baada ya kutokea fujo ya mashabiki waliokuwa wanaonyesha kukataa goli hilo,
Wachezaji wa Al-Ittihad na wasimamizi wa mechi walilazimika kutoroka kwa usalama wao
Ghasia zilizuka ndani na nje ya uwanja.
Na Mashabiki wa Al-Ahli wakaamua kulichoma moto basi la timu ya Al-Ittihad na gari la polisi.
Chanzo: ManaraTv
Mwamuzi kutoka nchini Ureno Fábio José Costa, alijeruhiwa na mchezaji wa akiba na Mwamuzi akakataa kuendelea na mechi baada ya kutokea fujo ya mashabiki waliokuwa wanaonyesha kukataa goli hilo,
Wachezaji wa Al-Ittihad na wasimamizi wa mechi walilazimika kutoroka kwa usalama wao
Ghasia zilizuka ndani na nje ya uwanja.
Na Mashabiki wa Al-Ahli wakaamua kulichoma moto basi la timu ya Al-Ittihad na gari la polisi.
Chanzo: ManaraTv