Kipimo ndani ya uchumba

Kipimo ndani ya uchumba

FORWARD

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2014
Posts
740
Reaction score
296
Habari wanajukwaa,

Leo napenda kuwahusia vijana wenzangu ambao wamefikia umri wa kuoa kupata chaguo sahihi. Tunaona miaka ya hivi karibuni ndoa nyingi zipo kwenye migogoro ya hapa na pale na nyengine zimevunjika kutokana na kutojuana vyakutosha katika kipindi cha uchumba.

Kitu cha muhimu kipindi cha uchumba ndicho kipindi muhimu hasa katika kufahamiana udhaifu wa kila mmoja. Njia nzuri ya kujua kikomo cha uzalendo wa mwenzi wako mtarajiwa ni kwa kutengeneza kaugomvi kwa makusudi ili umuone akikasirika huwa ana uzalendo wa kupoa ama moto usio zimika.

Jaribio hilo ni zuri maana kwenye ndoa kupishana lugha na kurushiana maneno hutokea mara kwa mara mpaka wengine hujuta kuwa na hao wenza.
 
Inategemea na ugomvi utakaoanzisha,mwingine ukijifanya kumchokoza kwa kuomba 0713 inakuwa mwiso

Huo wa kuomba 0713 mkuu bora uanzishe mapema maana kuna watu ndo udhaifu wao huo ili ukikataliwa ujue moja.
 
Hapo kwenye uhisiano kabla ya ndoa wengi wao wanaficha makucha,hasa yule anaemuhitaji mwenzie kuna watu hata uwafanye vipi wana stahmili,salam zake utazipata akisha kuweka ndani au ukisha muweka ndani hapo ndio utauona mpili pili na maua yake..
 
Hapo kwenye uhisiano kabla ya ndoa wengi wao wanaficha makucha,hasa yule anaemuhitaji mwenzie kuna watu hata uwafanye vipi wana stahmili,salam zake utazipata akisha kuweka ndani au ukisha muweka ndani hapo ndio utauona mpili pili na maua yake..

Very true.. the way to know who are you going to marry is fasted and prayer that's it.. Thanks..
 
Ni vizuri lakini hekima na busara ni muhimu itumike ktk kufanya jaribio hilo, la sivyo badala ya kufanya jaribio utafanya UE
 
Uchumba siku hizi una USER MANUAL SCRIPT!!!!!!!! Mambo kama maigizo tu mpaka UOE. KUNA CODE OF CONDUCT KABISAAA na FRATERNITY za wadada kujadiliana namna gani umuhadae mkaka mpaka pete ipatikane.:lol:.
 
Mimi napingana nawe kidogo na sababu ya kufanya hivyo ni kama ifuatavyo;

Mwanaume na mwanamke waelekeapo ndoa hupitia hatua kadhaa ikianza na urafiki, uchumba na hatimaye ndoa...

Binafsi naamini hatua ya uchumba si hatua stahiki ya kumchunguza mtarajiwa wako na wengi hukosea hapa...

Kwanza uchumba hupaswa kufanyika kwa muda mfupi mno, kwa kuwa hatma ya mahusiano tayari huwa bayana...

Hatua pekee ambayo ni muhimu sana ni ile hatua ya mwanzo ya urafiki na kufahamiana kwa kawaida...

Huu ndio wakati haswa wa kumchunguza mwanaume au mwanamke, ni wakati ambao hupaswi kutoa ahadi yoyote itafsiriyo hatma ya mahusiano...

Wengi waliofanya haya hawajawahi kujuta na mbinu hii ndio ilitumika zamani, na uchunguzi ulienda mbali zaidi kwa watu kuchunguzana hadi asili ya familia, miiko n.k
 
Hapo kwenye uhisiano kabla ya ndoa wengi wao wanaficha makucha,hasa yule anaemuhitaji mwenzie kuna watu hata uwafanye vipi wana stahmili,salam zake utazipata akisha kuweka ndani au ukisha muweka ndani hapo ndio utauona mpili pili na maua yake..

wewe ulifanya hivyo?ulivyowekwa ndani ndo ulimuonesha rangi zote?
 
Mimi napingana nawe kidogo na sababu ya kufanya hivyo ni kama ifuatavyo;

Mwanaume na mwanamke waelekeapo ndoa hupitia hatua kadhaa ikianza na urafiki, uchumba na hatimaye ndoa...

Binafsi naamini hatua ya uchumba si hatua stahiki ya kumchunguza mtarajiwa wako na wengi hukosea hapa...

Kwanza uchumba hupaswa kufanyika kwa muda mfupi mno, kwa kuwa hatma ya mahusiano tayari huwa bayana...

Hatua pekee ambayo ni muhimu sana ni ile hatua ya mwanzo ya urafiki na kufahamiana kwa kawaida...

Huu ndio wakati haswa wa kumchunguza mwanaume au mwanamke, ni wakati ambao hupaswi kutoa ahadi yoyote itafsiriyo hatma ya mahusiano...

Wengi waliofanya haya hawajawahi kujuta na mbinu hii ndio ilitumika zamani, na uchunguzi ulienda mbali zaidi kwa watu kuchunguzana hadi asili ya familia, miiko n.k

Umeelezea vizuri sana mkuu, lakini urafiki hauna uzito katika mahusiano kiasi kwamba unaweza kuwa na rafiki wa kike mwenye rafiki mwengine wa kiume akiangalia bingo ya uchumba itaangukia wapi! Sasa akishakuwa mchumba ndipo atlist anakuwa na kauhakika kwamba ndoa itafuata, ndipo hapo majaribio yaanze.
 
Uchumba siku hizi una USER MANUAL SCRIPT!!!!!!!! Mambo kama maigizo tu mpaka UOE. KUNA CODE OF CONDUCT KABISAAA na FRATERNITY za wadada kujadiliana namna gani umuhadae mkaka mpaka pete ipatikane.:lol:.

Bila mwongozo, pressure+kisukari+bp juu. Ndo maana kale kausemo ka kale "Ndoa ndoano" kanaendelea kufanya kazi, ukijichanganya ukanasa tu umekwisha.
 
Madogo acheni kujidanganya. Wakuoa huja naturally, yani hata udhanii
Naeza kubali hii dhana coz huwa sielewi kbs mda stahiki wakukaa kwenye mahusiano mpk kufunga ndoa ni upi watu wanaeza kaa miaka3 wakahisi wanajuana vyakutosha lkn bado wakaja kuachana wengine wakakutana na ndani ya mwaka wakafunga ndoa na ikadumu vilevile kiukweli kwa sasa sielewi hasa ni nini kinachoendelea katika ulimwengu huu wa mapenzi nahisi kuvurugwa tu nakuona nyota....theres no formula
 
muda wa uchumba fekero nyingi mana mtu umwambie ukweli akikumwagaaa,inakuejee afu ndo ushamzimikia,
tutajuana mbele kwa mbele,
kuna vitu being a woman huwezi ukatajaa tuu ili mwanaume wako akufahamu vizur,mfano ur sexual past n relationships,hapo.lazma upunguze namba,ikibidi useme hujawah kuwa serious na hzo habar,unaangalia lakn na mtu
haya kuna ingine let's say.kazi za nyumbani hupendi na huwa hufanyii mfano kufua labda au.deki,hivi uanze kabsa kupiga.promo oh me sipendi.kufua,say.whooo,ndani ya ndoa ndo utajua,
haya labda napenda viwanja sanaa,kwa mupenzi ambae unaona ana mwelekeo inabidi u regulate kdogo hii sekta,nk...
fekero.ztaendele kuwepo mana some of us can't handle real shit,mbele ya safari sasaaa heheheh,Mungu atusaidie ndoa zidumu
 
Naeza kubali hii dhana coz huwa sielewi kbs mda stahiki wakukaa kwenye mahusiano mpk kufunga ndoa ni upi watu wanaeza kaa miaka3 wakahisi wanajuana vyakutosha lkn bado wakaja kuachana wengine wakakutana na ndani ya mwaka wakafunga ndoa na ikadumu vilevile kiukweli kwa sasa sielewi hasa ni nini kinachoendelea katika ulimwengu huu wa mapenzi nahisi kuvurugwa tu nakuona nyota....theres no formula

Vijana mnaanza sana na kutamani. Mimi mke wangu nilivokutana nae nilikuwa hata sifikirii nitakuja kuwa naye kimapenzi...Ghafla, upendo ukaanza kujengeka na yeye kujengeka. Hakuna aliyemtongoza mwenzio, it naturally occured.

Sema kazi mnayo vijana, MIDORI imekuwa mingi sana siku hizi. Mtachepukiana mpaka akili ziwakae sawa
 
Back
Top Bottom