Kipigo heavy

Habari wadau poleni kwa shughuli ya kujenga viwonder.....

Ivi ni kipigo gan ulichowahi kupigwa heavy na ukaona kabisa hiki kipigo siku stahili nimeonewa
............ ..... . .. ......................



Mimi nakumbukuka ilikua mwaka 2014 nikiwa monitor wa form two a sasa ilikua mishale ya sa nne darasa likawa linapiga kelele na amna ticha clas akapita second master akaulizia mbona clas amna ticha bhana bhana montres akasema monitor kagoma kwenda kumuita walahi mshkaji alinipiga fimbo kama mia na hamsin na nilimlaan sana jamaa ila mwisho wa siku akaja akafukuzwa....



Karibu na ww utupe kisa chako

Sent using boeing 737 max8
Sijawahi kupigwa wala kupiga
Napenda kuishi maisha ya Amani na Upendo

Kumbe jf kuna watoto
 
Nakumbuka mwaka 2003nikiwa shule ya Msingi nilichezea kichapo cha pande mbili kwa kosa la kusingiziwa kubaka katoto kamoja kakike hivi.
"
"Ilikuwa tunatoroka shule na wasela kama 4 hivi. Njiani wakati tunarudi kawaida yetu ilikuwa tunapita kwenye shamba la miwa la magereza lililokuwa karibu na shule tunaiba tunatoka tunatafuna njiani.
sa siku hiyo tukawa tumeongozana na haka katoto kufika maeneo ya mapori mapori
majamaa yakawa yanataka kula mzigo. wakakavuta vuta hapa na pale wakakichania unform zake ila hawakufanikiwa kulamba lolo.
kufika mtaani kanalia sana afu mama yake ni mbogo kinoma kakasema tulitaka kumvua pichu akaambiwa ataje wahuni akanijumlisha na mimi .

Jioni nimetoka kucheza mpira mother akaniteka.
nimsindikize kwa mama fulani nikamsalimie weweee !!! kufika baada ya story mbili tatu nikashangaa kale ka bi mdashi kananikwida na kichapo heavy' badae mother akaniungia tena hapo hapo nililainika vizuri kesho yake sikuweza kwenda shule . Mpaka leo nimemsamehe mama yangu tu yule mama na mtoto wake nimewaweka hivi kushoto.


"Quora"
 
zamani hiyo kitaa nilikua misele night siku ya mwaka mpya wahuni wakanisimamisha wakataka kunivua shoes moja kali sana nikagoma kaugomvi ka ajabu kaakanza walikua watatu mkono wa kufa mtu ukatembea pale sema nilikua peke yangu dah nilichoka wakanipa kipigo kikali sana na shoes wakachukua nikarudi home damu kama zote nafika mshua ananicheki vip nikamsimulia dah mzee hasira zilimpanda kinyama akaingia ndani then akatoka aniambia twende mhuni mmoja nilikua nampata sema bi mkubwa akamzuia akasema tutawatafuta kesho yake mzee akaniambia nikalale duh! bila hata ya dawa moro asubuhi kama sa tatu mzee kaniamsha ninamaumivi kinyama tukaongozana mpaka masikani kufika wahuni wote kimya kumbe kipindi wananipiga hawakujua kama mm ndo mtoto wa mshua weeeeeeee heeee mshua hajaanza hata kuongea jamaa amepiga magoti anaomba msamaha alipigwa vifuti kama vitatu chapu niliona tu nguo ya mzee imekua nyekundu kwenye goti nikajua mzee kaumia nini kumbe jamaa kang'oka meno mawili mpaka kesho hajaota meno dah! wele jamaa wengine wawili mpak leo sijawahi kuwaona tena sema mzee siku hizi kawa mzee sana ilkua balaaa wakuu huko shy town kitambo.shuleni ilikua kosa mwalimu kunirudisha home nikalete mzazi mzee anasema mimi huyo mtoto nimemleta kwenu mmfunze then mnanirudishia na kuniita mm iliweje kunaticha wa muda alinitimua eti nikalete mzazi father kaja skuli kaongea kama kawaida yake ticha anadakia kwa juu kama anataka kumfokea mshua mwalimu mkuu alimwambia yule ticha we mwl kimya hahhahahaha mzeee akaondoka nikapewa adhabu ya kuchimba mashimo ya takataka na kufyeka uwanja mzima wa shule .
Walikuwa fanta nini hahahaha
 
Mi bna nnachokikumbuka kuna mwalim mmoja hivi anaitwa Mwali oscar ni mzawa wa wilaya flani mkoani kagera, aliwahi kunionea bila ya sababu na kipindi hicho tukiwa form four tukijiandaa kuingia necta, dah nikwamba alikua akiulizia watu wapi makwao, mkoa gani, wilaya etc... Alipofika kwangu sikuwa nime mark chochote maana Mda huo nilikua nameza madesa ya physical geography dah!! Alinipiga sana akanidharirisha sana mbele ya darasa bila ya sababu yenye mashiko,, kiukweli tangu nizaliwe hata sijawahi kupata kipondo kama kile, hadi darasa walinihurumia mda huo alidai eti nna kiburi,, yaan mwalim mwenye degree yake aliye soma psychology za watoto kuanzia mimba mpaka mtu mzima anashindwa ku handle vitu vidogo kama vile, dah!! Mwalim alinitia bakora mpaka jioni nkanywa dawa za kutuliza maumivu, aisee sintokusahau we jamaa na wakati mda huo ulikua umekuja kutembeatu pale shuleni ukitokea shule jirani,, yaan kihereheretu sio kizuri katika maisha. Ila ipo siku

Mwalimu Oscar sintokaa nikusamehe hata iwe vipi, ilatu kwa sababu za kibinadam achatu niliamua kukufuta kichwani mwangu, mungu atanilipia.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daah! Nakumbuka Kuna siku moja mitaa ya uhindini mjini Dom hio daah! Nko na mwanangu mmoja sangu now marehemu tumeambatana na dogo mmoja hv anaitwa nata, tukaenda nyumba ya dingi moja hv liliwahi kua kuu la wilaya huko iringa lilikua refu afu KUBWA liko so powerful, lengo letu lilikua kuiba mapera maana yule dingi alikua anakaa peke yake Hana familia nyumba yake ilikua karibu na tbc Kanda ya Kati pale uhindini, mapera mekundu kinyaaama! Nyumba Ina fence ya michongoma! Ce tukazunguka pembeni ya nyumba yake kulikua na pagale, tukaanza tungua mapera, Sasa Mimi tamaa zangu zikaniponza, baada nichume mapera ya karibu c nikafata Yale ya mbali, nikawa nimeingia ndani ya nyumba ya yule mzee ingawa Niko juu ya mti, yule mzee akasikia kukurakakara zile akafurumuka ndani, mwenzangu mmoja akajificha pagaleni mwingine fasta akakimbia mie ile natua tuu dingi hili hapaaa! Limebeba mbao ngumu mkononi! Nikadesh nilipige chenga nkafanikiwa Sasa ile naruka mtaro likarusha mguu nikaenda chini!!!! Daaaah! Aisee Lile dingi lilinipiga Kama linaua nyoka!!! Lilinitandikaa mamaeeee!nilivimbaa mikono, miguu! Nikafanikiwa kuinuka ila nshaivisha vibaya nachechemeaa! Eti hasira za kitoto nlivofika mbele acha nianze kumporomoshea matusiii!!!
 
Back
Top Bottom