Kipi bora kwa huyu mtoto?

Kipi bora kwa huyu mtoto?

Leo kiswahili na Mimi nimeelewa hahaa..mimi naona binti bado mdogo,bora angekuwa na 7 years hivi..akae nae tu mpaka awe na akili angalau kidogo,halafu kama hiyo nafasi bado itakuwepo amruhusu aende.
 
Kama inawezakana huyo kaka mtu amchukue mtoto na baba yake waje wote USA,
ila mtoto kuja peke yake akose malezi ya baba mzazi si vizuri.
Kama anawaamini ndugu zake basi aweza wapa mwanae. Atakuwa anamuandalia future nzuri mtoto.
 
Lea mtoto wako mwenyewe kama kweli unampenda. Huko unakotaka kumpeleka mtoto siafiki coz you never know huyo unaempelekea sio damu yake. Katika makuzi ya mtoto kuna mambo ambayo mzazi anatakiwa azingatie ili mtoto akue ktk maadili. Nani kakwambia huyo mke wa nduguyo atahangaikia maadili ya mwanao. Jikaze kiume pambana na malezi ya mwanao hata kama ataharibika ataharibikia mikononi mwako kuliko kuharikia mikonononi mwa mtu mwingine ukaanza kutupa lawama.
 
watu tunadhani marekani ndo kila kitu. Ataporudi hapa ana abuse drugs ndo mtaelewa, america is the worst place to rase a black child
nikweli kabisa,sio drugs tu atarudi akiwa hana upendo na babaake yeye ni marafiki zake tu wa states tena kama Huyo ndugu atakua amepigika ndio atamzarau kabisa,mtoto mlee ktk njia impasayo akiw MTU mzmima umpeleke sasa states mana pia hujui atapa uangalizi gani huko kama anauwezo wa kimtunza mwanae amtunze asije akampoteza akiwa bado hai
 
Ampeleke mtoto kwa kaka yake.
Mzazi ni mzazi tu, akikua atawatafuta wazazi wake.
Ule upendo alioukosa atautafuta tu kwa wazazi wake.
 
Hapana akae na mtoto wake. Hao wa huko marekani wazae mtoto wao apate hzo benefit zao. Kiroho hiyo bond ni kitu muhimu sana.
Kwanza hao watu wazima wenyewe huko marekani kujilea kazi mtoto akashinde daycare noo akae na bibi na babu yake i see.
 
Jamaa ana mtoto wa kike, umri kama miaka mi-4 sasa. Hajaoa, wala hana mawasiliano na mama wa mtoto(Tuyaachie hapo tafadhali). Mtoto anaishi na wazazi wa jamaa. Jamaa anamuona mwanae mara kwa mara, na anajitahidi kuwa baba bora.

Ana kaka yake wa damu anayeishi na kufanya kazi America, ni marafiki wazuri pia. Anapofanyia kazi kaka yake, wanatoa benefits mbali mbali kama za matibabu, elimu, n.k. kwa wafanyakazi pamoja na familia zao. Kaka hajaoa, wala hana mtoto, anaishi na mpenzi. Katika maongezi, Kaka amependekeza jamaa ampeleke mwanae ili akafaidike na hizo benefits pamoja na mambo mengine. Jamaa kamuambia kaka yake ampe muda kidogo ili afikirie.

Jamaa ana uwezo wa kumtunza mwanae(fedha sio tatizo), na angependa pia wawe karibu ili kutengeneza bond baina yao. Ila pia, elimu na exposure atakayopata America ni tofauti sana, isipokuwa jamaa atakuwa na muda/uwezo wa kuwa na binti yake angalau mara 3 kwa mwaka.

Vaa viatu vya jamaa, unadhani kipi ni bora kwa huyu mtoto? Karibu.
Inshort, Nitamlea Mwanangu Tuu Mkuu
 
Ningekuwa ni mimi kwanza ningemwacha mwanangu amalizie darasa la saba then aende Marekani. Au amalizie secondary then aende marekani kwa ajili ya kuingia college. Marekani ipo tuu asiwe na haraka sana maana anaweza kuja kujuta ile mbaya. Kuna watu wanalea watoto wa watu kama vile ni wao wa kuwazaa.
 
I think He better let the kid go,I know he wants to be a good father but the child need that exposure atakua kiakili na kutopenda kuwa tegemezi jamii zetu nyingi za Afrika watoto wanakua na akili tegemezi kweli knowing dad is there,grandmom or grandpops na ndugu wengine lakini kuwa nje ya nchi kunabadilisha sana najifananishia mimi mwenyewe before na after. Ni mtazamo wangu.

Kama ubaba umemshinda ampe mdogo wake kwa kisingizio cha elimu na exposure bora. lakini kwa anayejua maana ya majukumu yake kama baba au mama hawezi kamwe kujivua huo wajibu kwa sababu ya kipande cha mkate.

Siku hizi mama na baba wengi wameshindwa umama na ubaba ndio maana baadhi yao wanapeleka boarding hata mtoto wa chekechea.

Ila ukikwepa umama au ubaba baadae lazima utajuta kwani watoto hawatakuwa na mapenzi na wewe. Uliza waliopeleka boarding watoto wakiwa wadogo
 
Ningelikuwa mimi, mwanangu namlea mimi mwenyewe haijalishi maisha yangu yakoje. Mtoto anahitaji malezi ya mzazi mwenyewe angalau kwa miaka kumi ya mwanzo. Pamoja na kwamba huyo ni kaka yake, anauhakika gani na malezi atakayopewa mtoto.....!? Dunia ya leo imeota meno, anaweza kuwa ndugu yako wa damu lakini bado akamnyanyasa mwanao.

nawengine wanaiman za ajabu sana sikuiz za vyama vya siri anaweza kumsadaka kama uwezo wa kumlea upo amlee tu
 
Back
Top Bottom