Kipi bora kwa huyu mtoto?

Kipi bora kwa huyu mtoto?

Roger Sterling

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2015
Posts
13,010
Reaction score
23,653
Jamaa ana mtoto wa kike, umri kama miaka mi-4 sasa. Hajaoa, wala hana mawasiliano na mama wa mtoto(Tuyaachie hapo tafadhali). Mtoto anaishi na wazazi wa jamaa. Jamaa anamuona mwanae mara kwa mara, na anajitahidi kuwa baba bora.

Ana kaka yake wa damu anayeishi na kufanya kazi America, ni marafiki wazuri pia. Anapofanyia kazi kaka yake, wanatoa benefits mbali mbali kama za matibabu, elimu, n.k. kwa wafanyakazi pamoja na familia zao. Kaka hajaoa, wala hana mtoto, anaishi na mpenzi. Katika maongezi, Kaka amependekeza jamaa ampeleke mwanae ili akafaidike na hizo benefits pamoja na mambo mengine. Jamaa kamuambia kaka yake ampe muda kidogo ili afikirie.

Jamaa ana uwezo wa kumtunza mwanae(fedha sio tatizo), na angependa pia wawe karibu ili kutengeneza bond baina yao. Ila pia, elimu na exposure atakayopata America ni tofauti sana, isipokuwa jamaa atakuwa na muda/uwezo wa kuwa na binti yake angalau mara 3 kwa mwaka.

Vaa viatu vya jamaa, unadhani kipi ni bora kwa huyu mtoto? Karibu.
 
I think He better let the kid go,I know he wants to be a good father but the child need that exposure atakua kiakili na kutopenda kuwa tegemezi jamii zetu nyingi za Afrika watoto wanakua na akili tegemezi kweli knowing dad is there,grandmom or grandpops na ndugu wengine lakini kuwa nje ya nchi kunabadilisha sana najifananishia mimi mwenyewe before na after. Ni mtazamo wangu.
 
Ningelikuwa mimi, mwanangu namlea mimi mwenyewe haijalishi maisha yangu yakoje. Mtoto anahitaji malezi ya mzazi mwenyewe angalau kwa miaka kumi ya mwanzo. Pamoja na kwamba huyo ni kaka yake, anauhakika gani na malezi atakayopewa mtoto.....!? Dunia ya leo imeota meno, anaweza kuwa ndugu yako wa damu lakini bado akamnyanyasa mwanao.
 
angekuwa amemaliza elimu ya msingi ningesema ampeleke kwa kaka yake sababu mtoto atakuwa anajitambua na kuelewa kibaya na kizuri kwa umri huo kwanza amekosana malezi ya mama basi apate upendo kutoka kwa baba kwanza
 
watu tunadhani marekani ndo kila kitu. Ataporudi hapa ana abuse drugs ndo mtaelewa, america is the worst place to rase a black child
 
I think He better let the kid go,I know he wants to be a good father but the child need that exposure atakua kiakili na kutopenda kuwa tegemezi jamii zetu nyingi za Afrika watoto wanakua na akili tegemezi kweli knowing dad is there,grandmom or grandpops na ndugu wengine lakini kuwa nje ya nchi kunabadilisha sana najifananishia mimi mwenyewe before na after. Ni mtazamo wangu.

Not entirely true, but thanx.

Kama jamaa anauwezo wa kumlea mwanae,basi ni vyema akae nae kuliko kumpa ndugu yake.
Kiuhalisia,malezi ya baba ni bora kuliko kitu kingine ktk dunia ya leo.
Atazame mbele zaidi kuwa atakuja kuwa nani katika familia yake.

Ana uwezo wa kumtunza, ila sio wa kumlea kutokana na sababu kadhaa zilizo nje ya uwezo wake. Mtoto analelewa na wazazi wa jamaa. Ila nimekuelewa Chief.

Ampeleke tu ila ahakikishe huyo mwanamke karidhia kukaa na mtoto hajalazimishwa

Hana tatizo kabisa mpendwa.

Ningelikuwa mimi, mwanangu namlea mimi mwenyewe haijalishi maisha yangu yakoje. Mtoto anahitaji malezi ya mzazi mwenyewe angalau kwa miaka kumi ya mwanzo. Pamoja na kwamba huyo ni kaka yake, anauhakika gani na malezi atakayopewa mtoto.....!? Dunia ya leo imeota meno, anaweza kuwa ndugu yako wa damu lakini bado akamnyanyasa mwanao.

Umeongea vizuri sana boss. Asante

angekuwa amemaliza elimu ya msingi ningesema ampeleke kwa kaka yake sababu mtoto atakuwa anajitambua na kuelewa kibaya na kizuri kwa umri huo kwanza amekosana malezi ya mama basi apate upendo kutoka kwa baba kwanza

Umeongea vyema. Asante.

Mmmh!!! Jinsi watoto wa kike wanavyofanyiwa ukatili na watu wanaowasaidia, sionagi haja ya kumkabidhi mtu mtoto, kwanin asiendelee tu kumuwezesha akiwa huku??

Mi tumbo la uzazi linaninyonga kwa habari za hvi.

Yeah. Moja ya sababu zinazompa jamaa kigugumizi kwa kuwa ni mtoto wa kike. Asante mama.

watu tunadhani marekani ndo kila kitu. Ataporudi hapa ana abuse drugs ndo mtaelewa, america is the worst place to rase a black child

Marekani ni nchi boss. America kuna mabara mawili, inaweza kuwa nchi yoyote. Na kuna watu wanatumia dawa za kulevya na hawajawahi hata kufika Kigamboni. Ila asante pia.

Kama mzazi.....

Ningekaa na mwanangu.
Malezi ya mzazi ni ya mzazi tu....
Miaka 4 ni mdogo mno.

Mama hayupo mpendwa. Vaa viatu vya baba hapa.

BTW, BADILI MWANDIKO, au usiwe una-type huku una-drive.:A S shade:

Huyo mwanamke aliyepo Amerika ameridhia kukaa na huyo mtoto??

Hana tatizo kabisa.
 
Kwa mustakabali wa maisha ya baadae ya mtoto ningempeleka America kama ni mimi Elimu ya America ni bora mara dufu na Elimu si tu ya Tanzania bali ya nchi mingi za Africa...Umri wa mtoto si mdogo sana kwani kuna watu wengi hapa Tz siku hizi wanapeleka watoto boarding school kuanzia baby class so mtoto anakuja home likizo mara 3 kwa mwaka si ni sawa tu na huyo jamaa mtoto akienda America kuna uwezekano wa kumuona mara 3 kwa mwaka.
 
Hata kama mama hayupo

Wewe baba kaa na mwanao

Mtoto anakuhitaji

Na kulelewa na baba mkubwa/mdogo ni tofauti na malezi ya baba

Ukizingatia dunia imevaa bukta siku hizi....
 
I could let her go... huyo mtoto akikua akajua baba alikataa asiende nje atanuna mpaka anakufa lol!!!
jua la bongo nani anapenda bora akapate exposure huko...

Hahaha. Sio kwamba Bongo ni pabaya, jamaa ana uwezo wa kumnunulia mwamvuli na ice cream kupunguza makali pia.
 
shida nini malezi elimu ama?Akae na mwanae asee malezi ya mzazi ni tofauti kabisaa na ndugu! Incase huyo mpenzi wa kakake wameachana what next?
 
At four years ni mdogo lakini ningeangalia jinsi kaka yake alivyo zaidi kabla sijafanya maamuzi..si mbaya pia akienda huko bana, exposure ni nzuri!
 
Back
Top Bottom