Kasie
Platinum Member
- Dec 29, 2013
- 21,236
- 36,268
Subal kheri mpenzi wangu usiyechosha wala usiyentoka akilini
Hakika umejua kunipumbaza, kila nikihadaa mawazoni umenijaa
Nafurukuta weeeh nikigeuka kulia nakukuta wanitazama kwa huba
Nikigeuka kushoto waninyanyulia mikono kunikaribisha kifuani mwako unikumbatie
Nikirudi nyuma kabla sijajikwaa ushanidaka mikononi mwako na kunisemesha kwa macho yako yenye bashasha na huba la kitwana...
Niende wapi Kasie mie, natafuta nini mie huku na huko, shurti wanituliza na kuniliwaza...
Japoo, japoo... kuna muda wanipeleka uwanja wa mapambano, wanidunda dunda mfano wa kitenesi, kisha wanidanadana mfano wa mpira wa ngozi, kisha wanipiga tikitaka na wewe kupiga samasoti mithili ya Sonic kuniwahi kabla hujafunga goli kwa madaha, wanituliza kwenye goti na kuendeleza danadana za aste aste kisha wanipandisha kifuani na kunirushia kichwani kwako hapo utapiga vichwa kadhaa na ukiona sasa niko tilalila hoi bin rojorojo unaongeza makeke na mbio na spidi ohh lala la la la la la la la la gooooooooooooooooooooooal.....!!!
Huku nikiwa nimefumba macho, najikuta natamka maneno nisiyoyasikia wala kuyaelewa na kuishia kusema asante mahabuba.
Rukhsa sasa uzime taa tulale.
Nakupenda Mahabuiba wangu wa pekee (Dadii) kwa vyovyote sikushuku...
K' Mahaba.
Hakika umejua kunipumbaza, kila nikihadaa mawazoni umenijaa
Nafurukuta weeeh nikigeuka kulia nakukuta wanitazama kwa huba
Nikigeuka kushoto waninyanyulia mikono kunikaribisha kifuani mwako unikumbatie
Nikirudi nyuma kabla sijajikwaa ushanidaka mikononi mwako na kunisemesha kwa macho yako yenye bashasha na huba la kitwana...
Niende wapi Kasie mie, natafuta nini mie huku na huko, shurti wanituliza na kuniliwaza...
Japoo, japoo... kuna muda wanipeleka uwanja wa mapambano, wanidunda dunda mfano wa kitenesi, kisha wanidanadana mfano wa mpira wa ngozi, kisha wanipiga tikitaka na wewe kupiga samasoti mithili ya Sonic kuniwahi kabla hujafunga goli kwa madaha, wanituliza kwenye goti na kuendeleza danadana za aste aste kisha wanipandisha kifuani na kunirushia kichwani kwako hapo utapiga vichwa kadhaa na ukiona sasa niko tilalila hoi bin rojorojo unaongeza makeke na mbio na spidi ohh lala la la la la la la la la gooooooooooooooooooooooal.....!!!
Huku nikiwa nimefumba macho, najikuta natamka maneno nisiyoyasikia wala kuyaelewa na kuishia kusema asante mahabuba.
Rukhsa sasa uzime taa tulale.
Nakupenda Mahabuiba wangu wa pekee (Dadii) kwa vyovyote sikushuku...
K' Mahaba.