chakii
JF-Expert Member
- Sep 15, 2013
- 21,369
- 27,785
Katika kumbukumbu za mwaka 1995 wakati wa mchakato wa kupata wagombea wa kushika nafasiya urais, Kingunge Ngombale Mwiru alikuwa mjumbe wa kamati kuu CCM.
Kama kawaida mchakato wa vikao vikuu CCM uliwadia, lakini kabla ya kuanza kwa vikao hivyo, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alikuwa amekutana mahali fulani na Kingunge jijini Dar es salaam na kunong'onezana kuhusu uadilifu wa Lowassa, mwanasiasa kijana tu wakati huo ambaye alikuwa ameamua kutaka kuongoza Taifa hili.
Mwalimu alikuwa anamwamini sana Kingunge, ama pengine kutokana na uelewa wake au kutokana na utiifu wake wa " ndiyo mzee". Kamati Kuu ilipoanza kikao chake na jina la Lowassa kuwasilishwa mbele ya wajumbe wa kikao hicho ili waweze kulijadili, mtu wa kwanza kusimama ndani ya kikao kwa lengo la kueleza sifa za Lowassa alikuwa ni Kingunge.
Huyu huyu tunayemjua kuwa ni miongoni mwa wanasiasa wakongwe hapa nchini, ambao sisi wengine tuliwafahamu na kuwaamini kwamba siasa zao na itikadi zao zinaongozwa na ujamaa au ukomunisti. Moja ya itikadi ambayo Baba wa Taifa, aliikubali nakuiamini kwamba inaweza kuwaondoa Watanzania kwenye unyonge wa kifikra katika kukabiliana na umaskini, ujinga na maradhi.
Ni kingunge aliyewaeleza wajumbe wa Kamati Kuu jinsi Lowassa asivyofaa hata kujadiliwa na kikao hicho kutokana na utajiri mkubwa alionao wa fedha na mali nyingi, yakiwemo majumba ya kifahali wakati umri wake na muda wake wa utumishi wa umma, havifanani na utajiri wake huo.
Zipo pia taarifa kuwa ni Kingunge aliyewakumbushawajumbe kuwa CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi wanyonge, hivyo hakiwezi kuongozwa na Kada wake mwenye utajiri usiokuwa na maelezo ni wapi ameupata mali hizo na kwa njia gani!
Baada ya maelezo hayo ndipo Mwalimu Nyerere akapigilia msumari kuwa Lowassa hana sifa za kuliongoza Taifa hili. Kuna wakati marafiki zake Lowassa walipopata taarifa hizi walimjulisha Lowassa kuwa aliyepigilia msumari jina lake kukatwa alikuwa Kingunge Ngombale Mwiru.
Lowassa baada ya kupata taarifa hizo alimtolea uvivu Mzee Kingunge na kumwendea, kabla ya kumtamkia kuwa "wewe mzee ni mtu mbaya sana siwezi kuongea na wewe tena katika maisha yangu." Lakini baadaye Nyerere aliwapatanisha baada ya Kingunge kulalamika na kushitaki kwake.
Cha kushangaza sasa katika Hotuba yake Kingunge aliyoitoa kwa niaba ya wazee wa CCM katika safari ya Matumaini hiyo ya Lowassa siku ile ya Jumamosi ya Mei 30, mwaka huu, katika Uwanja wa Sheikh Amani Abeid, imewashangaza wengi na kumuonyesha kuwa Kingunge hana nia nzuri kwa chama chake cha CCM na Tanzania kwa ujumla wake.
Kifupi kabisa niseme mapema hapa; kwamba kama Kingunge alidhani hotuba yake ile imemjenga mtu wake Lowassa, atakuwa amejidanganya mwenyewe. Kwa maoni yangu, hotuba ile imerahisisha sana jukumu la vyama vya siasa nchini vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kuing'oa CCM katika Uchanguzi Mkuu wa Oktoba 25 Mwaka huu!
Tuendelee kuona mengi na kuyafahamu.
Kama kawaida mchakato wa vikao vikuu CCM uliwadia, lakini kabla ya kuanza kwa vikao hivyo, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alikuwa amekutana mahali fulani na Kingunge jijini Dar es salaam na kunong'onezana kuhusu uadilifu wa Lowassa, mwanasiasa kijana tu wakati huo ambaye alikuwa ameamua kutaka kuongoza Taifa hili.
Mwalimu alikuwa anamwamini sana Kingunge, ama pengine kutokana na uelewa wake au kutokana na utiifu wake wa " ndiyo mzee". Kamati Kuu ilipoanza kikao chake na jina la Lowassa kuwasilishwa mbele ya wajumbe wa kikao hicho ili waweze kulijadili, mtu wa kwanza kusimama ndani ya kikao kwa lengo la kueleza sifa za Lowassa alikuwa ni Kingunge.
Huyu huyu tunayemjua kuwa ni miongoni mwa wanasiasa wakongwe hapa nchini, ambao sisi wengine tuliwafahamu na kuwaamini kwamba siasa zao na itikadi zao zinaongozwa na ujamaa au ukomunisti. Moja ya itikadi ambayo Baba wa Taifa, aliikubali nakuiamini kwamba inaweza kuwaondoa Watanzania kwenye unyonge wa kifikra katika kukabiliana na umaskini, ujinga na maradhi.
Ni kingunge aliyewaeleza wajumbe wa Kamati Kuu jinsi Lowassa asivyofaa hata kujadiliwa na kikao hicho kutokana na utajiri mkubwa alionao wa fedha na mali nyingi, yakiwemo majumba ya kifahali wakati umri wake na muda wake wa utumishi wa umma, havifanani na utajiri wake huo.
Zipo pia taarifa kuwa ni Kingunge aliyewakumbushawajumbe kuwa CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi wanyonge, hivyo hakiwezi kuongozwa na Kada wake mwenye utajiri usiokuwa na maelezo ni wapi ameupata mali hizo na kwa njia gani!
Baada ya maelezo hayo ndipo Mwalimu Nyerere akapigilia msumari kuwa Lowassa hana sifa za kuliongoza Taifa hili. Kuna wakati marafiki zake Lowassa walipopata taarifa hizi walimjulisha Lowassa kuwa aliyepigilia msumari jina lake kukatwa alikuwa Kingunge Ngombale Mwiru.
Lowassa baada ya kupata taarifa hizo alimtolea uvivu Mzee Kingunge na kumwendea, kabla ya kumtamkia kuwa "wewe mzee ni mtu mbaya sana siwezi kuongea na wewe tena katika maisha yangu." Lakini baadaye Nyerere aliwapatanisha baada ya Kingunge kulalamika na kushitaki kwake.
Cha kushangaza sasa katika Hotuba yake Kingunge aliyoitoa kwa niaba ya wazee wa CCM katika safari ya Matumaini hiyo ya Lowassa siku ile ya Jumamosi ya Mei 30, mwaka huu, katika Uwanja wa Sheikh Amani Abeid, imewashangaza wengi na kumuonyesha kuwa Kingunge hana nia nzuri kwa chama chake cha CCM na Tanzania kwa ujumla wake.
Kifupi kabisa niseme mapema hapa; kwamba kama Kingunge alidhani hotuba yake ile imemjenga mtu wake Lowassa, atakuwa amejidanganya mwenyewe. Kwa maoni yangu, hotuba ile imerahisisha sana jukumu la vyama vya siasa nchini vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kuing'oa CCM katika Uchanguzi Mkuu wa Oktoba 25 Mwaka huu!
Tuendelee kuona mengi na kuyafahamu.