Kinana na miradi ya maendeleo

Kinana na miradi ya maendeleo

LEO MWITA

Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
25
Reaction score
1
Wana jamvi naomba tujadili kwa pamoja uhalali wa katibu mkuu wa CCM kukagua miradi ya maendeleo ambayo imetokana na michango ya wananchi.

Leo Kinana alitaka kufungua shule ya sekondari moja Tarime Nyamongo lakini wananchi wamekataa na badala yake atafungua ofisi ya CCM kata ya Nyarero.

Hii tabia ni mbaya sana na kama yeye ana uhalali huo basi makatibu wakuu wa vyama vingine nao wafanye hivyo.

Naomba maoni yenu.

Source, ni mimi mwenyewe nipo Nyamongo.
 
Nashukuru kutujuza hayo mkuu.Siyo sahihi kabisa anavyofanya ila nashukuru wa huko kwenu wamemkataa shetani na mambo yake yote.ila fanya marekebisho ya kichwa cha habari...... [h=2]Kina na miradi ya maendeleo[/h]
 
wana jamvi naomba tujadili kwa pamoja uhalali wa katibu mkuu wa ccm kukagua miradi ya maendeleo ambayo imetokana na michango ya wananchi.leo kinana alitaka kufungua shule ya sekondari moja tarime nyamongo lakini wananchi wamekataa na badala yake atafungua ofisi ya ccm kata ya nyarero.hii tabia ni mbaya sana na kama yeye ana uhalali huo basi makatibu wakuu wa vyama vingine nao wafanye hivyo.naomba maoni yenu source ni mimi mwenyewe nipo nyamongo.

Hana hayo Mamlaka ya kufanya kama alivyotaka kufanya, kwa mujibu wa Katiba ya Nchi, 1977 labda kama anataka afanye jitihada Katiba Mpya impe huo uhalali wa kufungua miradi ya Maendeleo ya Wananchi.
Aidha, bado yupo kwenye usingizi wa enzi zile za Chama kushika hatamu (party supremacy) kwahiyo wakati mwingine mmpe elimu ya uraia kuwa hayo hayapo tena.

Kudos Nyamongo.
 
Ana haki kwani anasimamia utekelezaji wa ilani ya CCM!
 
Back
Top Bottom