SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
Na Mwandishi Wetu,
Moshi, Kilimanjaro.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana, amepongeza ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Marekani kwa kusema kuwa italeta faida kubwa kwa nchi.
Amesema ziara hiyo imemkutanisha na viongozi wakubwa akiwemo Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris ambaye nchi yake Ina ushawishi mkubwa duniani.
Kinana ameyasema hayo katika mkutano wa ndani wa chama hicho mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro akiwa katika ziara ya kikazi kukagua uhai wa chama na kujitambulisha baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo hivi karibuni.
"Sasa hivi anafanya ziara nje huko, kwa kukutana na wawekezaji, wafanyabishara, wafadhili na watoa mikopo ili tuweze kupata fedha nyingi zaidi kwa maendeleo ya taifa letu na kukuza uchumi kupitia biashara na uwekezaji." Amesema Kinana
Kinana aliendelea kusema "Rais yuko Marekani, ameonana na Makamu wa Rais wa Marekani. Marekani ni nchi kubwa, Marekani Ina kauli duniani, Marekani ni mshiriki wetu wa maendeleo katika sekta mbalimbali zinazowagusa wananchi,"
Amesema Rais Samia pia amekutana na viongozi wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha duniani (IMF), Taasisi ambazo ni washirika muhimu wa maendeleo na uchumi wa Tanzania, hivyo anastahili pongezi.
Moshi, Kilimanjaro.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana, amepongeza ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Marekani kwa kusema kuwa italeta faida kubwa kwa nchi.
Amesema ziara hiyo imemkutanisha na viongozi wakubwa akiwemo Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris ambaye nchi yake Ina ushawishi mkubwa duniani.
Kinana ameyasema hayo katika mkutano wa ndani wa chama hicho mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro akiwa katika ziara ya kikazi kukagua uhai wa chama na kujitambulisha baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo hivi karibuni.
"Sasa hivi anafanya ziara nje huko, kwa kukutana na wawekezaji, wafanyabishara, wafadhili na watoa mikopo ili tuweze kupata fedha nyingi zaidi kwa maendeleo ya taifa letu na kukuza uchumi kupitia biashara na uwekezaji." Amesema Kinana
Kinana aliendelea kusema "Rais yuko Marekani, ameonana na Makamu wa Rais wa Marekani. Marekani ni nchi kubwa, Marekani Ina kauli duniani, Marekani ni mshiriki wetu wa maendeleo katika sekta mbalimbali zinazowagusa wananchi,"
Amesema Rais Samia pia amekutana na viongozi wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha duniani (IMF), Taasisi ambazo ni washirika muhimu wa maendeleo na uchumi wa Tanzania, hivyo anastahili pongezi.