Kilio,manung'uniko ya walimu na anguko la elimu!!

Kilio,manung'uniko ya walimu na anguko la elimu!!

UTENDE

Senior Member
Joined
Jan 20, 2013
Posts
126
Reaction score
64
Mishahara duni, ukosefu wa makazi, mazingira magumu ya kufanyia kazi kwa walimu, ni kilio cha muda mrefu kwa walimu (walezi wa jamii). Ila kwa masikitiko makubwa serikali imeziba masikio na kutotaka kabisa kuwaboreshea walimu maisha yao na mazingira ya kazi ili wawe na ARI ya kufundisha na kutoa matunda bora....Mwaka jana, walimu wote nchini waligoma kufanya kazi takribani wiki nzima kuishinikiza serikali kuboresha maisha ya walimu ila dola ilikimbilia mahakamani kuzuia mgomo ule...Mahakama baada ya kuzuia mgomo, ilitoa sharti baina ya serikali na walimu kukaa meza moja kutafuta suluhu.CHA KUSHANGAZA,SERIKALI IMEKUWA IKIWAKIMBIA WALIMU KUKAA MEZA MOJA NA HADI LEO HAWAKO TAYARI KUFANYA SULUHU. Kwa manung'uniko walimu walirudi kazini wakiwa hawana ARI ya kufanya kazi, imepelekea MATOKEO YA DARASA LA SABA NA KIDATO CHA NNE 2012 KUWA MABAYA KUPINDUKIA. Kutokana na kelele nyingi na malalamiko ya watanzania juu ya ANGUKO LA ELIMU,waziri mkuu akaunda tume ya kutafuta kiini hasa cha matokeo mabaya.....Cha kushangaza tume kati ya matatizo yaliyo baini eti MASLAHI DUNI, KUKOSEKANA KWA ARI NA UTAYARI WA MWALIMU KUFUNDISHA SI CHANZO CHA MATOKEO MABAYA.....Walimu tumegundua kuwa tume husika haikuundwa kwa dhamira ya kutafuta mzizi wa ANGUKO LA ELIMU, na ndo maana wameelekeza mashambulizi yao yote baraza la mitihani. Watanzania, hv ni kweli kuw anguko la elimu Tanzania linasababishwa BMT?? Haya serikali inalitaka baraza la mitihani litumie huo mfumo wa 2011(50% ya wanafunzi walipata 0) je mwaka huu ndo watoto walifaulu sn?? KIUJUMLA WALIMU TUNAENDELEA NA MANUNG'UNIKO YETU JUU YA UKANDAMIZWAJI WA WALIMU NA UHUJUMU WA ELIMU. MUNGU IBARIKI TANZANIA!!
 
Wewe siyo mwalimu nashangaa unatumia neno sisi walimu,utakuwa upo milembe day itabidi wasilana na kigwangala kunadawa anayotumia lisu ili upate,tumeshuhudia serikali ikiendelea kuboresha mambo mbalimbali katika elimu na walimu kwa ujumla kwa mfano imebainisha kuwa mwaka huu walimu wataongeziwa mishara kwa kiwango kikubwa tofauti na watumishi wengine, sasa wewe unataka kutuaminisha ujinga wako ambao siyo kweli fanya kwanza tafiti ndipo useme na kama unafuata maelekezo ya mkuu wako kuwa na pande mbili yaani faida na hasala kwa maana ya kwamba kwa suala kama hili lazima serikali imefanya kitu hata kama ni kidogo ila siyo zero kabisa kama wewe unavyodai,unavyotumika siyo mbaya ila wanasiasa unaowatumikia siku wakipata madalaka wala hutawaona tena.
 
Mishahara duni, ukosefu wa makazi, mazingira magumu ya kufanyia kazi kwa walimu, ni kilio cha muda mrefu kwa walimu (walezi wa jamii). Ila kwa masikitiko makubwa serikali imeziba masikio na kutotaka kabisa kuwaboreshea walimu maisha yao na mazingira ya kazi ili wawe na ARI ya kufundisha na kutoa matunda bora....Mwaka jana, walimu wote nchini waligoma kufanya kazi takribani wiki nzima kuishinikiza serikali kuboresha maisha ya walimu ila dola ilikimbilia mahakamani kuzuia mgomo ule...Mahakama baada ya kuzuia mgomo, ilitoa sharti baina ya serikali na walimu kukaa meza moja kutafuta suluhu.CHA KUSHANGAZA,SERIKALI IMEKUWA IKIWAKIMBIA WALIMU KUKAA MEZA MOJA NA HADI LEO HAWAKO TAYARI KUFANYA SULUHU. Kwa manung'uniko walimu walirudi kazini wakiwa hawana ARI ya kufanya kazi, imepelekea MATOKEO YA DARASA LA SABA NA KIDATO CHA NNE 2012 KUWA MABAYA KUPINDUKIA. Kutokana na kelele nyingi na malalamiko ya watanzania juu ya ANGUKO LA ELIMU,waziri mkuu akaunda tume ya kutafuta kiini hasa cha matokeo mabaya.....Cha kushangaza tume kati ya matatizo yaliyo baini eti MASLAHI DUNI, KUKOSEKANA KWA ARI NA UTAYARI WA MWALIMU KUFUNDISHA SI CHANZO CHA MATOKEO MABAYA.....Walimu tumegundua kuwa tume husika haikuundwa kwa dhamira ya kutafuta mzizi wa ANGUKO LA ELIMU, na ndo maana wameelekeza mashambulizi yao yote baraza la mitihani. Watanzania, hv ni kweli kuw anguko la elimu Tanzania linasababishwa BMT?? Haya serikali inalitaka baraza la mitihani litumie huo mfumo wa 2011(50% ya wanafunzi walipata 0) je mwaka huu ndo watoto walifaulu sn?? KIUJUMLA WALIMU TUNAENDELEA NA MANUNG'UNIKO YETU JUU YA UKANDAMIZWAJI WA WALIMU NA UHUJUMU WA ELIMU. MUNGU IBARIKI TANZANIA!!
Mkuu unamoyo hata haya huna katika kusema uongo,eti serkali inawakimbia walimu imekimbia hadi wapi mbona majengo ya serikali na watumishi wake kila siku naona wapo kwenye hayohayo sasa wamekimbia kwenda wapi?,halafu detail zote kwenye post yako za uongo yani we hewa kweli.
 
Wewe siyo mwalimu nashangaa unatumia neno sisi walimu,utakuwa upo milembe day itabidi wasilana na kigwangala kunadawa anayotumia lisu ili upate,tumeshuhudia serikali ikiendelea kuboresha mambo mbalimbali katika elimu na walimu kwa ujumla kwa mfano imebainisha kuwa mwaka huu walimu wataongeziwa mishara kwa kiwango kikubwa tofauti na watumishi wengine, sasa wewe unataka kutuaminisha ujinga wako ambao siyo kweli fanya kwanza tafiti ndipo useme na kama unafuata maelekezo ya mkuu wako kuwa na pande mbili yaani faida na hasala kwa maana ya kwamba kwa suala kama hili lazima serikali imefanya kitu hata kama ni kidogo ila siyo zero kabisa kama wewe unavyodai,unavyotumika siyo mbaya ila wanasiasa unaowatumikia siku wakipata madalaka wala hutawaona tena.

wewe ndio mwehu na ni mpuuzi kabisa unatoana sisi walimu kama watoto wadogo, unaweza kumwambia mwanao kesho nitatakununulia nguo mpya ili anyamaze kulia leo na kesho usimnunulie! lakini sisi ni watu wazima havdanganyiki na ahadi za kitoto! ebo
 
Mkuu unamoyo hata haya huna katika kusema uongo,eti serkali inawakimbia walimu imekimbia hadi wapi mbona majengo ya serikali na watumishi wake kila siku naona wapo kwenye hayohayo sasa wamekimbia kwenda wapi?,halafu detail zote kwenye post yako za uongo yani we hewa kweli.

unaleta hoja za kitoto! we ni mpuuzi kabisa!
 
Kibwete unasawili kabisa na jina lako...usivo na haya unaonesha waz kuwa ww kuna watu unawatumikia, unaingiza siasa kwenye taaluma inayozalisha wataalamu!! Ww lete ngonjera zako ila tambua walimu wameshaamua kumwaga mboga maana ww na mabwana zako mulishamwaga ugali. Ipo cku tu mutawatafuta walimu kuwalamba miguu kunguni ww!!
 
nyie hamjui maana ya ualimu!!mimi ni mwl.niliyegoma toka naanza kazi !!serikali haijaffanya kitu kbisa
 
Ukweli uliopo n kuwa hali za hawa watu ni mbaya ktk kila nyanja(aspect). Walimu wana makaz duni, wanapata mlo duni n.k. Mwl anayenza kaz wa ngaz ya cheti anapewa wastan wa elfu 7 kwa siku na kwa hapo atatakiwa kulipa kodi ya nyumba ya km elf 40 kwa mwezi. Alipe gharama nyingine km maji na umeme ambapo ikifika tar 5 ya mwez anaanza mikopo.
Ila swali kwa walimu wa Tz, n kwanin mmeshindwa kuungana na kudai haki zenu. Mnalalamika, mnatishia kugoma na kusema elimu itashuka. Ushauri wangu ni kuwa fanyeni kweli kuitafuta haki, ila fuaten utaratibu
 
Utaratibu wa kudai haki tushafanya sn ila kilio chetu hakisikilizwi...sasa tumeamua kuwa "silent killers". walimu 2mesuswa na si serikali tu, bali na jamii pia. So 2meamua kugoma kimyakimya na hayo matokeo yao wata edit hadi wakome.
 
chonde chonde walimu msijibishane na magamba wamelishwa unga wa ndele hao, cha msingi tunajua hatuna kazi tuna ajira,
 
Kimyakimya

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom