Kilio cha yatima wa Mango Tree kwa William Fulton

Mbombo Nunu

Member
Feb 10, 2018
92
123
Toka 2014 mpaka sasa,inakaribia takribani miaka 5 tangu (WILLIAM FULTON) mmiliki na mkurugenzi wa kituo cha MANGO TREE ,kituo kilichokuwa kikihusika na Msaada Wa kielimu kwa Yatima,Wenye Mahitaji maalumu na waishio katika mazingira magumu ya kimaisha,alipowekewa zuio la kuingia nchini kuja kuangalia,kuendeleza na kusimamia miradi yake ya Ufadhiri aliyokwisha iasisi.

Sababu kubwa ni katika kile ambacho hata Mheshimiwa waziri Wa mambo ya ndani amewahi kukizungumza kuwa,haoni na hakuna ushahidi Wa kosa lolote lililowahi fanya kutolewa kwa zuio juu ya bwana Fulton, hajaliona na hakuliona kwenye ofisi yake na hata alipofika uhamiaji hakuiona wala kupewa sababu ya msingi,na hata waziri Mkuu aliwahi kukaririwa akikiri kuwa anafahamu na anataarifa juu ya uwepo wa kundi la watu wachache waliotengeneza mazingira ya dhurma na kujimilikisha Kituo kiubabe kwa sababu zao binafsi na kwa kutumia nguvu ya nafasi zao kiutawala ,hatimaye wakamtilia ndimu mzee Wa watu na kufanikiwa kwenye mipango yao.

Aibu yao ni kwamba walidhani mzee anafaidi,hivi tunavyozungumza ni habari nyingine tofauti,miradi yote ikawafia mikononi mwao miaka michache tu baada ya kujimilikisha ,watoto waliokuwa wamefaulu elimu za juu wakaanza kulia ukata Wa kutohudumiwa/kutosaidiwa kwa pesa ya kujikimu na ADA,hata wengine kupelekea kufukuzwa toka mashuleni kurudi majumbani,achilia mbali hata kituo chenyewe kushindwa tena kuwapokea watoto walio kwenye mazingira magumu na kuwasaidia kwa mujibu Wa usajiri Wa kituo hata kama walikidhi kuwa sehemu ya wasaidiwa kwa mujibu wa hali zao pia.

Hivi tunavyozungumza ni Habari nyingine kabisaaa,MANGO TREE imekufa kifo cha mende ,watoto wametawavyika hovyo hovyo wengine wamerudi kwenye kuomba Omba ili mradi wajisogeze mahala ,kila mmoja na njia yake,wangine wamerudi kwenye maisha yao ya kimatukio mtaani baada ya kuishia njia Kielimu na kukosa mkono Wa Heri mbadala Wa mzee William Fulton, kwa kipindi chote hicho wahanga wamekuwa WAKISALI NA KULIA KUOMBA MZEE FULTON ARUDI NCHINI kwa kurejea kauli ya waziri Mkuu kuwa hakuona na haoni tatizo lolote linalopelekea KUZUIWA KWA FULTON,lakini sasa MOYO WA UPENDO WA MZEE WILLIAM FULTON HAUJUI UTAWASAIDIA VIPI WALE WATOTO AMBAO ALIWAZOEA NA ALIWALEA KAMA SEMEMU YA FAMILIA YAKE NA KUWASAIDIA KUTIMIZA NDOTO ZAO,ALIKO NAYE ANATOKWA NA MACHOZI HASA PALE ANAPOPIGIWA SIMU NA BAADHI YAO NA KUAMBIWA KUWA mango tree IMEFARIKI kama kituo,na ZAO LAKE AMBALO NI CHUO CHA KPC kilichowafanya waheshimiwa sana kuwekeza huko walau kwa akili na nguvu zao ili wakitendee haki kibiashara zaidi wasijedondoka jumla jumla nacho pia ndio hivyoooo KINAKOSA UELEKEO kwa MITAFARUKU ISIYOISHA YA KIMGONGANO WA MASRAHI.

Chonde chonde waheshimiwa sana ,inawezekana mlitaka kujaribu lakini nia mbaya yenu ndio inayowatafuna nyinyi kwa nyinyi leo hii kwa sababu ya kutokuwa na mikakati thabiti na kutojua namna gani hizi Charity Institutions zinapaswa kusimamiwa na kuendeshwa,miroho yenu mibaya ya kutaka kurefusha matumbo yenu yatokee mbele ndio yanayoishi pamoja nanyi,figisu figisu zinawatokea puani.

Kilichoumiza na kinachoumiza ni kwamba bado mzee Wa watu baada ya kusikia kilio cha jamii ya walezi na watoto wa wana ukanda Wa nyanda za juu kusini ,pamoja na kwamba ana project nyinginezo kama hizo katika baadhi ya nchi barani afrika ,AMESEMA HANA KINYONGO NA JAMII HUSIKA KWA VILE ALIVYOISHI NAO na YUPO TAYARI KUJA KUWAFUTA MACHOZI ENDAPO MAMLAKA HUSIKA ZITAYAKUBALI MADHAIFU YA UPANDE WAKE ULIOJITOKEZA KUFUATIA ZUIO LAKE NA KUAMUA KUTENGUA,naye amesema amejaribu kuomba hivyo Mara kadhaa lakini ugumu huja kwa KUNG'ANG'ANIA kwa wale walioamua kujimilikisha na Kushindwa Kukabiliana na AIBU ya KUTENGUA ZUIO LISILOWAHI KUWA NA SABABU MAALUMU YA KIMAMLAKA zaidi ya misuko.

Swali ni NANI JASIRI WA KUMSEMEA MZEE KUTOKA KWENYE ZUIO LILE AMBALO ANALO HATA SASA AJE KUKIOKOA KIZAZI KILE KILICHOTAPANYWA NA WACHACHE KWA MASLAHI YA TAIFA HILI?

Nyuma ya pazia.......siasa za Kyela.......siasa za Tanzania zilichangia pakubwa kwenye kuirudisha jamii yake yenyewe nyuma.
ae0f90faac5d7d16e7b5d3beff116bef.jpg
9a22e088edb1e3de192cce3d829e72ba.jpg
36ae3f7a2b2033f4eb1e55964bd4086e.jpg
ebdca8243765339d679beb4ab629d9cc.jpg
 
Kwahiyo hao mabaradhuli wanataka kuyageuza hayo majengo guest house sio? Na adhma hiyo itatimia endapo tu yatima wote wataondoka na kurudi mitaani ili majengo yabaki matupu. Huyu PM nae anachekesha, kama haoni tatizo anashindwa nini kutoa amri mtu huyo aruhusiwe?, maana hakuna kesi mahakamani na hakuna ushahidi wala haoni kosa, sasa anasubiri nini kumruhusu? Au ni kwanini asihoji hiyo amri ya zuio imetoka kwa nani? Ndo yale yale ya JK, wananchi wanalia na viongozi waliopewa dhamana wanalia, si ujinga huu?
 
Haiwezekani wamzuie tu bila sababu...inawezekana labda alikuwa Jasusi ndiyo maana hawataki kusema hadharani....... nimawazo yangu tu
 
Huenda Usalama wa Taifa letu kwa namna yoyote ile ulikua hatiani, je hana mwakilishi? hawezi kutumia mtu mwingine kuleta hiyo misaada au mpaka aje yeye ndo shughuli zitaenda?
 
Viongozi wetu waoga sana....! Hivi mtu kaja kusaidia yatima anakosa gani ? Mbona wapo mitaani mnabishana nao kila siku lakini hamna chochote....! Endeleeni kutoa matamko ila mkumbuke kuna maisha baada ya uongozi...! Msijifanye miungu watu.
 
Kwa mujibu wa Mtanzania mwenzetu aliye uingereza na ambaye pia ni Engineer katika kampuni moja kubwa ya kimtandao nchini humo,anasema yeye aliifuatilia hii issue ya Fulton tokea mwaka 2014. Bahati nzuri wakati huo alikuwa na access na baadhi ya vigogo wa kwenye wizara husika.

Sehemu ya Uhuni aliofanyiwa ni huu na namnukuu yule bwana:

1. "Fulton hajaambiwa kosa lake mpaka Leo. Hii nilihakikishiwa na Fulton mwenyewe. Pia niliiona barua ya bàlozi wa UK nchini TZ akiongelea hivyo hivyo na pia kuna kigogo mmoja aliwahi kuniambia hivyo."

2. "Inaelekea taarifa za kosa la Fulton zilitoka Kyela na kwenda Ikulu. Ikulu wakaijulisha wizara na Idara ya uhamiaje kufuta visa yake. "

3." Kulingana na maelezo ya Fulton aliambiwa na ofisa mmoja wa uhamiaji kwamba kwenye file hakuna kosa lolote ila kuna tuhuma kwamba yeye anaichukia CCM. Ni mwanachama wa Conservative party ya UK na wamempa mapesa awasaidie chadema na ndizo alizitumia kwenye uchaguzi wa vitongoji vya Kyela mjini mpaka chadema wakashinda na ccm inaweza kupoteza jimbo 2015. Pia kwamba yeye ni shushushu na amewahi kufukuzwa Congo na Brazil. Kulingana na Fulton Congo hajawahi fika na Brazil hata mwaka jana au juzi alikuwa likizo huko.
Nayajua mengi zaidi ya hayo ila nisije kuharibu vibarua vya watu."

4. "Haya yote yalianza kutokea baada ya Mango Tree UK kumwondoa Mwenyekiti wa Mango Tree TZ kwa makosa ya kufuja pesa."

Anaendelea kwa kusema;

"Conclusion yangu mwanzo wa tatizo hili ni Kyela na hata solution yake ni Kyela.

Kipija atakuwa anajua vizuri maana ilisemwa kwamba hizo pesa zinapitia kwa Kipija na kwamba Kipija angejiunga chadema 2015. Na kwamba Ili kufanikisha hayo Kipija alialikwa na Fulton kuja UK. Ni kweli Kipija alikuja UK kwa Fulton kwa mambo tofauti. Baada ya kuona Kipija ana exposure na anapenda elimu. Fulton alitaka kumtumia kwenye board ya KPC.

Kwasasa ni hayo tu. Akili ya kuambiwa changanya na ya kwako. Huenda kuna version nyingine lakini nijuacho Mimi ni hicho.'

Hayo ni machache yenye kusisimua toka kwa Mtanzania mwenzetu aishiye Ughaibuni ambaye pia alipata Bahati ya kuonana na bwana Fulton nchini Uingereza baada ya kusikia masaibu yake na kuamua kwenda kumpa pole,pamoja na yote kwa mujibu Wa mtanzania mwenzetu huyo anasema Mpaka hivi sasa tunavyojadili hapa,bwana Fulton hajakata kamba ya kuwazila watoto na vijana Wetu walio katika sintofahamu ya nini hatima ya maisha yao tangu kuondoka kwake ,ameahidi kuwarudia kama zuio litaondolewa na atawafanyia makubwa zaidi ya pale bila kinyongo.

Huyu mzee kwa kweli ana moyo Wa huruma,Wa huduma ,na Wa ajabu sana......alafu tutambue na tumshukuru mungu na kujiuliza kwanini sisi?,vinginevyo angeshajiziria afanye mengine au kupeleka mradi huo nchi nyingine, ikumbukwe kwa Kenya na Tanzania miradi yake ilianza kufanya kazi tangu 2002 kabla ya Wa kwetu kudhoofu na kuondoka kwake,Kenya bado wanafaidi huduma ya Mango Tree,Malawi nako walimpokea kwa mikono miwili baada tu ya kuletewa figisu za kisiasa zikiongonzwa na Mwakyembe (being honest) ,na naskia anatoa huduma hiyo kwa nchi takribani 5 mpaka sasa za kiafrika na bado anakwambia hana roho ya kuzira kwa ajili ya taifa,Maana anasema kuliziria taifa kutakuwa ni kuisafirisha dhambi ya dhurma kwa watoto wake Yatima na wasiojiweza bila sababu za msingi.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom