Kilio cha Mwendokasi, Vifo na Changamoto Zilizokosa Suluhisho

Mk54

JF-Expert Member
Dec 29, 2016
1,997
3,933
Miongoni mwa Project zilizoanzishwa kwa muktadha wa Public Private Partnership ni mradi wa mwendokasi.

Kampuni iliyoshinda tenda ya ujenzi wa barabara na miundombinu ni Strabag kutoka Ujerumani kwa mkataba wa EUR 179. 6 Million huku Serikali ikiwa ni muangalizi wa miundombinu.

—Tumeona kwa upande wa Serikali ilivyoshindwa kusimamia miundombinu ya mradi huu. Tumeona jinsi ambavyo barabara zinavyoharibiwa, traffic light zinavyotolewa yaani barabara zinazidi kuharibika siku hadi siku pasipokuwa na action yoyote.
IMG_9218.JPG


Nchi hii ina Wajumbe,Madiwani , Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Mikoa , Waziri wa Tamisemi na Usalama wa Taifa wote hawa ni Makada wa CCM lakini wameshindwa kujua chanzo cha uharibifu huu na kuwakamata wote wenye kuhusika na uharibifu.
IMG_9223.JPG


Hivi hii nchi ni nini shida? Maana hizi barabara zinaharibiwa na watu wa mitaani, wanatoa zile nondo na kwenda kuuza, wanavunja vizingiti na kutengeneza njia, hakuna anayefuatilia hili swala.
IMG_9236.JPG


Haya ndiyo mambo ambayo Makonda unapaswa kuwa na majibu nayo. Mkoa wa Dar unaongoza kwa uchafu, kila kitu ni hovyo halafu unapoteza muda kupambana na Konki Likwidi—Makonda unakwama wapi ? Wewe si ndiyo Rais wa Dar ?
IMG_9239.JPG

-------------------------------

— kwa upande wa Kampuni iliyopewa dhamana ya uendeshaji wa mabasi wamefeli kwenye kila idara, kuanzia kwenye kutoa Huduma, kukusanya Mapato, kuwalipa Mishahara Wafanyakazi na vifo vya Raia kwa uzembe wa Madereva.

Aidha , Madereva wamekuwa na hasira ya kutolipwa hivyo kwa uzembe na makusudi wamekuwa wakigonga hovyo hovyo, spidi 120 hata sehemu zenye mkusanyiko wa watu, au sehemu zenye mataa.
IMG_9208.JPG


Sipati picha huko mbagala itakuwaje.

Mwendokasi ulianza kuua kiwete pale Msimbazi, ukaja kuua mtoto pale Gerezani, ukaja kuua Mdada wa Kihindi pale Kisutu, ukaja kuua muendesha Boda Boda pale Manzese, ukaja kuua muendesha gari pale Mapipa Magomeni siku ya Ijumaa 19, Aprili 2019, what is wrong ?
IMG_9209.JPG


Hawa traffic na wasimamizi wa barabara, wanafanya kazi gani?

Yote haya yamekuwa chini ya kapeti na hatuoni Action yoyote ikichukuliwa, are they above the law? —BS !

Mmeshindwa kusimamia mradi, Na watu wetu pia bado mnatuulia Kwakweli hii nchi inahitaji maombi, tena maombi ya wapagani maana maombi ya watu wa dini yamefeli kwa dhiki na njaa zao za matumbo yao makubwa.

—Zile mbio za Jaffo za kutatua kero za mradi huu ziliishia wapi vile
IMG_9210.JPG


Hivi ripoti ya CAG Imesemaje kuhusu huu mradi

Tunatambua mchango wa John Magufuli, na jitihada za kuweka nchi sawa. Lakini tunapata
Kigugumizi as in why Rais halitolei ufafanuzi hili swala ikiwa ni pamoja na kumuwajibisha Mkurugenzi mwenye dhamana ya kusimamia huu mradi, na Waziri wake.

Mbona kina Nape, Mwigulu na wengineo walimalizwa on spot bila ya kupoteza muda.

Rais Magufuli wewe ndio unamajibu ya haya maswali na utawapunguzia kero raia wako endapo haya maswali yatajibiwa kwa HERUFI KUBWA.

Katika Utendaji,

MK54, Raia Mwema

Jumamosi 20, Aprili 2019.
-----------------------
 
Duu
Wacha niwe wa kwanza siti ya mbele ya mwendokasi....

Mimi nimekuwa mtumiaji mzuri wa huu mradi kutoka Kimara kwenda Town..

Kwa sasa changamoto zimepungua ukilinganisha na wiki 02 zilizopita
 
Duu
Wacha niwe wa kwanza siti ya mbele ya mwendokasi....

Mimi nimekuwa mtumiaji mzuri wa huu mradi kutoka Kimara kwenda Town..

Kwa sasa changamoto zimepungua ukilinganisha na wiki 02 zilizopita

1. Elezea maana ya changamoto isijekuwa tuna definition tofauti za Changamoto.

2. Mention hizo changamoto zilizopungua ili tuweze kujadili kwa mapana.

Asante!
 
Shida ya nchi yetu ni kukosa watu wa kusimamia sheria na taratibu zilizopo. Na pale wanaposimamia wanabagua nani achukuliwe sheria na nani asichukulie. Hili ni tatizo kubwa na karibu Africa yote inachangamoto hiyo.

Viongozi wanaongoza kwa mihemko na matukio badala ya taratibu za sheria zilizopo. Matokeo yake kila mahali ni fujo
 
Huku kwetu mbagala hatuhitaji kabisa huo mradi wa BRT.
Sisi wakazi wa mbagala tunaiomba serikali hii ya magufuli chonde chonde huu mradi pelekeni kwingine huku mbagala tunahitaji bus terminal ya kisasa tu inatosha,tunapenda kuona daladala zetu zikiongezeka hiyo inatosha kabisa
 
1. Elezea maana ya changamoto isijekuwa tuna definition tofauti za Changamoto.

2. Mention hizo changamoto zilizopungua ili tuweze kujadili kwa mapana.

Asante!
Naelewa changamoto zipo
Ila nakumbuka wiki 02 zilizopita tulikuwa tukijazana kituoni magari hakuna


Kugombania mpaka nakumbuka marehemu simu yangu ambayo vile tulivyobanana mtu alinibana nikaua screen
 
Sikujua kama mwendokasi imeua watu takribani 5 hadi sasa. Hili ni tatizo kubwa.
 
Maendeleo yanachangiwa sana na ustaarabu wa watu....

Lazima tukubali kwamba watanzania bado sio wastaarabu na washamba na bado tuna Safari ndefu ya kwenda......

Ni kama yuke Boya mmoja aliyebomoa lami zile kokoto akaweka ndani kwake kisa nyumba ya vumbi.

Narudia Tena waTZ bado hatujastaarabika, Ni ngumu kuyazoea maendeleo hasa yanayohusisha teknnolojia
 
Naelewa changamoto zipo
Ila nakumbuka wiki 02 zilizopita tulikuwa tukijazana kituoni magari hakuna


Kugombania mpaka nakumbuka marehemu simu yangu ambayo vile tulivyobanana mtu alinibana nikaua screen

Yaani changamoto za kugombania ni moja ya Changamoto ndogo sana katika changamoto zinazokabili mradi huo.

Kampuni iliyopewa Zabuni ya kuendesha mradi huu wa mabasi, je unajua terms za contract zinasema nini ?with that failure, ni kwa muda gani watakuwa wanaendesha huo mradi? Yaani contract yao ni ya Muda gani , na je terms za kuvunja mkataba kwa failure zina semaje? Kwanza hicho kipengele cha kuvunja mkataba kipo ?

Bob, make sure you always learn how to see things in a Big Picture.

Ni nani anapaswa kuwawajibisha kwa hii failure inayoendelea?

Changamoto ni kwamba hii mikataba haipo transparent na haya mambo ndiyo kikwazo cha maendeleo katika nchi hii na miradi mikubwa.
 
Hili halitajadiliwa BUNGENI kama hospital ya vichaa ilivyojadiliwa yaani mambo yasiyokuwa na maana yanapewa mda lakini suala kama hili hakuna atakaeliongelea kabisa

Usafiri ni uti wa mgongo wa nchi maana ndio unaendesha nchi na kama kuna watu wanauharibu (ambapo haya hutokea) lazima kuwepo kampuni za kupitia na kurekebisha na kuja na mbinu mpya za kubadilisha hata hivyo vyuma wanavyoiba.

Sisi watu wa ajabu sana yaani huwa hatuna plan B kabisa na hatujui kubuni na kubadili vitu pindi tunapoona tatizo na hakuna mkuu wala idara inayoomba ushauri hata kama hawajui la kufanya wangeweka masanduku ya maoni na wenye akili au wanaojua kitu au mbadala wa kitu wangetoa maoni yao
Tatizo letu wapigaji ni wengi sana halafu neno UZALENDO lingeondolewa kwenye kamusi
 
Maendeleo yanachangiwa sana na ustaarabu wa watu....

Lazima tukubali kwamba watanzania bado sio wastaarabu na washamba na bado tuna Safari ndefu ya kwenda......

Ni kama yuke Boya mmoja aliyebomoa lami zile kokoto akaweka ndani kwake kisa nyumba ya vumbi.

Narudia Tena waTZ bado hatujastaarabika, Ni ngumu kuyazoea maendeleo hasa yanayohusisha teknnolojia

Ustaarabu utakuja kwa ku implement miongozo.

Kwa mara Tatu mfululizo watu wakiwajibishwa hadharani lazima watu watajua mambo ni serious.

Mbona maandamano wanaweza kuyatolea kauli na watu hawathubutu,

Tuseme wazi kuwa haya mambo sio kipaumbele cha serikali ndio maana ustaarabu hauzaliwi Tanzania.

Hujiulizi zile dust bin Kwenye kila kituo cha mwendokasi zimekwenda wapi?

Unaweza kuniambia ni katika mazingira gani unaweza kuzivunja ?

Lakini leo Hii makonda na waangalizi wake hawawezi kuwa na majibu ya huu uharibifu, yeye ni rais wa Dar anapaswa kuwa na majibu, haya mambo yanatokea Kwenye himaya yake.

Serikali haina kushindwa kitu ikiamua, Wewe leo Hii tangaza maandamano uone, utatafutwa hata kama upo shimoni na utachukuLiwa. Why not this, bodaboda Wote wanamajibu wa huu uharibifu, wawatumie hao kuwatolea mfano kwa wachache
 
Ustaarabu utakuja kwa ku implement miongozo.

Kwa mara Tatu mfululizo watu wakiwajibishwa hadharani lazima watu watajua mambo ni serious.

Mbona maandamano wanaweza kuyatolea kauli na watu hawathubutu,

Tuseme wazi kuwa haya mambo sio kipaumbele cha serikali ndio maana ustaarabu hauzaliwi Tanzania.

Hujiulizi zile dust bin Kwenye kila kituo cha mwendokasi zimekwenda wapi?

Unaweza kuniambia ni katika mazingira gani unaweza kuzivunja ?

Lakini leo Hii makonda na waangalizi wake hawawezi kuwa na majibu ya huu uharibifu, yeye ni rais wa Dar anapaswa kuwa na majibu, haya mambo yanatokea Kwenye himaya yake.

Serikali haina kushindwa kitu ikiamua, Wewe leo Hii tangaza maandamano uone, utatafutwa hata kama upo shimoni na utachukuLiwa. Why not this, bodaboda Wote wanamajibu wa huu uharibifu, wawatumie hao kuwatolea mfano kwa wachache
Tatizo ni ustaarabu na kufundishwa tangu utotoni hilo ndio tunashindwa kulielewa
Unapomfundisha Mtoto ndio akuavyo mkuu
Halafu tukiona wengine wanajitenga na society yetu mbovu wengine wanasema ni Racist ooh hawataki kuwa na sisi
Sina mengi ya kuandika natumaini utaelewa nina maana gani
 
Huku kwetu mbagala hatuhitaji kabisa huo mradi wa BRT.
Sisi wakazi wa mbagala tunaiomba serikali hii ya magufuli chonde chonde huu mradi pelekeni kwingine huku mbagala tunahitaji bus terminal ya kisasa tu inatosha,tunapenda kuona daladala zetu zikiongezeka hiyo inatosha kabisa
Serikali inahitaji mapato ujue
 
Back
Top Bottom