Kilakitu tutakiacha hapahapa duniani

Kilakitu tutakiacha hapahapa duniani

Rijali jandoni

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2018
Posts
2,174
Reaction score
2,262
Leo nimeamka tokea asubuhi nimekuwa nikisiliza nyimbo zilizo tamba enzi hizo napata masomo mengi sana na nyingine hata zina lenga maisha ya sasa tunayoishi
kikubwa tusikilize ujumbe pamoja.

Tuishi kwa upendo na umakini sana samehe ishi kwa furaha tajiri heshimu masikini maana kesho yako yeye ndie ambae atachimba kaburi mkubwa muheshimu mdogo,uzee wako utatunzwa na huyo mdogo,kijana heshimu wazee maana walikutunza kiburi chako kimetoka wapi watu walikupigania mpaka umefika hapo ulipo mshukuru MUNGU.

Tusijifunze kurudisha hekima busara na hata zawadi nzuri kwa jamii iliyokulea
Usiwalipe chuki na hasira watu waliokusaidia kisa tu leo umepata dunia hii bado mengi yanakuja magonjwa,shida na majanga mengine.

Tupendane haswa ukimchukia mtu kapatane nae unaweza samehe mtu ukajiweka mbali na mambo ambayo mnatofautiana ili amani na upendo wenu uendele.
tujifunze mambo mazuri kwa ambao wapo pembeni yetu maana kila mtu tunae kutana nae kwenye maisha anakitu ambacho atakijenga maisha kwetu.

*Tupendane marafiki*

 
Mkuu tafuta pesa na utaishi milele.
Jenga mahusiano mema kama unakufa kesho
 
Ishi maisha simple kama ya Bujibuji bujibuji,,, chekesha wengine ili na wewe karma ikuletee kicheko.
Wafariji walio taabuni, usijikombe wala kujipendekeza kwa mtu yeyote.
Ishi maisha yako hailisi.
Kula vizuri, kunywa maji mengi, dinyana sana na mkeo.
Mche Mungu
 
Back
Top Bottom