Kila tukipanga kukutana anakuja na girlfriend wake, nimechoka

Queen V

JF-Expert Member
Jan 19, 2012
775
1,332
Ni rafiki yangu wa kama miaka mitano, tumezoeana sana tangu tuko chuo. Tumekuwa marafiki kwa kipindi kirefu huku tukiwa na mahusiano yetu ya kimapenzi na watu wengine. Katika kipindi chote hiki, mahusiano yetu na watu wengine hayajawahi kuathiri urafiki wetu hata kidogo.

Hivi karibuni rafiki huyu ameanza uhusiano na mtu mpya. Huyu dada mimi ni classmate wangu wa enzi za sekondari ila hatukuwahi kuzoeana kwakweli (namuona anaringa, uzungu mwingi so damu zetu haziendani). Uhusiano huu naona unaelekea kuvunja urafiki wetu aisee na sifurahishwi.

Siku hizi wote tunafanya kazi hivyo kuonana ni nadra sana lakini tunajitahidi kupanga kukutana mahala na kupeana updates za maisha. Kila akija kuonana na mimi anakuja na girlfriend wake. Yani anaweza akaja alone ila baadae lazima huyo dada aje kutujoin.

Simchukii huyu dada wala sio kwamba nina hisia za kimapenzi kwa rafikiangu wala nini ila tukiwa watatu kunakuwa na awkward situation fulani yani. Wenyewe tunaongeaga saana na vicheko havikauki ila akiwepo yeye inakuwa ni ukimya tu na vimaneno vichache kutoka kwa rafikiangu akijaribu kuneutralize situation lakini bado kunakuwa ovyoovyo yani.

Sasa nawaza sijui nimwambie tu mshkaji kuwa awe anakuja mwenyewe au niwe nakataa mialiko?

Naomba ushauri
 
You are indeed a good example of a secret admirer kwa huyo rafikiako...inaonekana subconsciously unamuonea wivu wifi yako...kuwa mkweli wa hisia zako. Nashauri uwe makini pia least urafiki huo utatumbukia nyongo. Pole sana na kila la kher best
Wivu sina ila roho inauma. Kwanini asiniachie tu hivo vidakika niwe na maongezi ya amani na rafikiangu?
 
You still love the boy. Unampenda Sana,unachojaribu kukifanya ni kuipumbaza akili yako mwenyewe. Cha Msingi, acha kukutana na Jamaa na badala yake ongea na kutumiana naye ujumbe mfupi kupitia simu kuhusu kile mnachokududia kuongea faragha. Usipojiangalia,utakuja kudundana siku moja na shemeji yako.

Kama huna mwanaume,tafuta wa kukuweka busy ambaye mtawekeana mipango na ambaye utakuwa ukiongea naye kuhusu maisha na harakati za baadae.
 
It's high time you learned and accepted that the brothaman will always pay less attention to you, when the missus is around.

Bring King V to them rendezvous, that way y'all keep it the same.
There z no King V, and even if there was one, i would not bring him around when meeting with my friends. It is kinda disrespectful
 
Back
Top Bottom