Kila ninavyoitafakari Mbingu

Sijui itakuwaje Yesu na Magufuli wakikutana huko mbinguni. Mana Kuna majipu mengi ya kutumbuliwa
 
Hujajibu swali.

Kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Kuna sisimizi anaangukiwa na mti na kufa, kifo ni kitu kibaya, kwa nini Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao kifo cha sisimizi huyu kinawezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao ubaya wowote hauwezekani?
 
Mwache Mungu Ahimidiwe na haitwe Mungu

Katuachia maswali mengi sana na hakika majibu anayo yy muumba
 
Nadhani nimeshajibu.Mungu alitengeneza kifo na kuzaliana ili kuleta uwiano mzuri wa viumbe duniani.Katengeneza mazuri na mabaya na amempa mwanadamu utashi ili ajue namna ya kuchagua zuri na baya na aweze kuvitawala viumbe vingine.
kungekuwa hamna mabaya basi ata shetani asingekuwepo na mwanadamu asingekuwa na haja ya kuwa na ubongo.
Mimi sio msemaji wa Mungu ila nina amini uwepo wake na sina tatizo na imani yako ya kutokuwapo Mungu.Ni haki yako.
 
Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao hauna kifo lakini una uwiano mzuri wa viumbe?
 
Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao hauna kifo lakini una uwiano mzuri wa viumbe?

Kifo ni sehemu ya uumbaji utake usitake.
Ni dhahiri unaogopa sana kifo.Kila binadamu anaogopa kifo.Kifo ni mojawapo ya sababu inayodhihirisha utukufu wa Mungu.
 
Kifo ni sehemu ya uumbaji utake usitake.
Ni dhahiri unaogopa sana kifo.Kila binadamu anaogopa kifo.Kifo ni mojawapo ya sababu inayodhihirisha utukufu wa Mungu.
Hujajibu swali nililouliza.

Kifo si kitu kinacholetwa na mwenye mapenzi. Ndiyo maana Baba hamuui mwanawe. Ila Baba anafanya kila njia mwanawe asife.

Kwa nini Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aksumba ulimwengu ambao unaruhusu kifo wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hauruhusu kifo?

Issue si mimi kuogopa kifo. Issue ni logical consistency ya Mungu wenu.

Dhana ya Mungu wenu kuwepo haina logical consistency.

Vitu ambavyo havina logical cinsistency vinaashiria uongo.

Mungu wenu ni wa uongo. Hayupo. Ndiyo maana hana logical consistency.

Unaelewa hilo?
 
Alafu unaambiwa zipo Saba. Uwingu wa Saba ndipo alipo mungu
Cha ajabu anajua kila analolifanya mtu hapa duniani.
 
Upo sahihi kuamini mungu hayupo.Na ni haki yako.Mimi nina amini yupo.Tukubaliane kutokubaliana katika hilo.

Mungu alikuwa na maana yake kuweka kifo.Mimi na wewe hatuwezi kujua alikuwa ana maana gani na mimi na wewe wote tutakufa na kuoza na tutamuacha Mungu.Na haya malumbano kati yangu mimi na wewe juu ya uwepo wa Mungu ni dalili kuwa siku zetu za uwepo hapa duniani zimeshapungua sana.

Kibiblia tunaambiwa Adam na Hawa hawakutakiwa kufa.Walikuwa wanakula mimea na hakuna mnyama yoyote aliyekufa.Mungu akawapa utashi Adam na Hawa na akawakanya wasile tunda lililokatazwa.Adam na Hawa wakamkaidi Mungu wakala tunda.Mungu akakasirika akawapa kifo.Hivyo kifo kibiblia ni sehemu ya uumbaji na imetokana na dhambi ya wazazi wetu wa mwanzo.
Adam, Eve and all the animals were created to eat only vegetation ( Genesis 1:29-30). Nothing died prior to the spiritual fall of Adam and Eve (Genesis 3:19 and 3:21).

Sayansi pia inakubali kuwa kifo ni sehemu ya uumbaji.Sayansi inasema kifo kimeweza kubadilisha viumbe mbalimbali viweze kuendana na ugumu wa mazingira yao yaani evolution through natural selection and survival of fittest.Kwa mtizamo wa kibinadamu kifo kinaweza kuwa ni kibaya ila kisayansi kifo kimeweza kumbadilisha binadamu kutokuwa kuwa kama nyani akitumia zana za mawe mpaka leo ameweza kurusha chombo kwenda sayari ya mars na kurudi.

Kwa kifupi biblia na sayansi vyote vinaonyesha kifo ni sehemu ya uumbaji wa Mungu na sababu za uwepo wa kifo katika uumbaji.
 
Hakuna sehemu halisi inayoitwa mbingu kama vile kuaivyokuwa na eneo maalumu kama makazi ya kudumu ya Mungu. Hivyo mbingu ni wazo la kiimani zinakowlekwa roho na kuishi ktk umilele pamoja na Mungu
 
Eti Mungu anakasirika kwa kitu alichokiumba, maajabu haya, hivo vitabu vinaitwa vitakatifu nina shaka navyo sana.
 
Eti Mungu anakasirika kwa kitu alichokiumba, maajabu haya, hivo vitabu vinaitwa vitakatifu nina shaka navyo sana.
Ndio maandiko hayo.Na hilo ni neno la Mungu kwa mujibu wa historia.
 
Eti Mungu anakasirika kwa kitu alichokiumba, maajabu haya, hivo vitabu vinaitwa vitakatifu nina shaka navyo sana.
Mbona mzazi anakasilika kwa matendo mabovu ya mwanae ilihali yeye mwenyewe ndiye anayemlea na kumkuza .
 
Kifo ni sehemu ya uumbaji utake usitake.
Ni dhahiri unaogopa sana kifo.Kila binadamu anaogopa kifo.Kifo ni mojawapo ya sababu inayodhihirisha utukufu wa Mungu.
That's true
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…