Bonde la Baraka
JF-Expert Member
- Sep 22, 2016
- 4,580
- 7,953
Habari wanajukwaa!
Bila kumwonea mtu aibu napenda kuonyesha mambo ambayo wanaCCM wamepungukiwa. Kati ya haya machache nitakayoorodhesha chini ndiyo wenzetu wamepungukiwa aidha moja au zaidi. Mambo hayo ni;
1.Uzalendo. Haiingii akilini mtu au mbunge kufurahia miswada ya dharura ya maliasili ambayo ipo tu haiishi au kuharibika kesho. Yapo mambo yanayohitaji miswada ya dharura ila si madini wala gesi.Wabunge wanaangalia posho na kumfurahisha Rais na si kwa manufaa ya watanzania wa leo na wa kizazi kijacho.
2.Elimu. Wengi wanaoshabikia mambo ya CCM na serikali yake ni waliokosa elimu ambayo ingewapa mwanga wa kujua na kuweza kuibua hoja zenye nguvu.
Mfano:Muulize mtanzania ni nini faida ya zoezi zima la utumbuaji majipu la rais Magufuli? au nini faida za zoezi la uhakiki wa watumishi kwa Tanzania utajibiwa majibu ya ajabu yasiyoeleweka.
Mwingine atajibu sasa tunaheshimiana,mwingine atasema walikuwa wapiga dili n.k
3.Uchafu wa kocha mkuu. Watanzania wengi hawajui kuwa huyu mtumbua majipu huko nyuma (mgongoni mwake) yake yeye mwenyewe ana majipu makubwa yanayoonyesha kuwa yeye si mzalendo na wala hana uchungu na taifa hili bali anachokifanya sasa ni kuonyesha tabia yake ya asili ya ubabe.
Mtu kama mimi nitamshangilia vipi mtu aliyelitia hasara taifa maradufu kwa maamuzi yake ya kukurupuka kabla hajaingia Magogoni.
Bila kumwonea mtu aibu napenda kuonyesha mambo ambayo wanaCCM wamepungukiwa. Kati ya haya machache nitakayoorodhesha chini ndiyo wenzetu wamepungukiwa aidha moja au zaidi. Mambo hayo ni;
1.Uzalendo. Haiingii akilini mtu au mbunge kufurahia miswada ya dharura ya maliasili ambayo ipo tu haiishi au kuharibika kesho. Yapo mambo yanayohitaji miswada ya dharura ila si madini wala gesi.Wabunge wanaangalia posho na kumfurahisha Rais na si kwa manufaa ya watanzania wa leo na wa kizazi kijacho.
2.Elimu. Wengi wanaoshabikia mambo ya CCM na serikali yake ni waliokosa elimu ambayo ingewapa mwanga wa kujua na kuweza kuibua hoja zenye nguvu.
Mfano:Muulize mtanzania ni nini faida ya zoezi zima la utumbuaji majipu la rais Magufuli? au nini faida za zoezi la uhakiki wa watumishi kwa Tanzania utajibiwa majibu ya ajabu yasiyoeleweka.
Mwingine atajibu sasa tunaheshimiana,mwingine atasema walikuwa wapiga dili n.k
3.Uchafu wa kocha mkuu. Watanzania wengi hawajui kuwa huyu mtumbua majipu huko nyuma (mgongoni mwake) yake yeye mwenyewe ana majipu makubwa yanayoonyesha kuwa yeye si mzalendo na wala hana uchungu na taifa hili bali anachokifanya sasa ni kuonyesha tabia yake ya asili ya ubabe.
Mtu kama mimi nitamshangilia vipi mtu aliyelitia hasara taifa maradufu kwa maamuzi yake ya kukurupuka kabla hajaingia Magogoni.