Kila mnapozidi kumkosoa na kumtaja rais Magufuli, ndipo mnapozidi kumpa jina

stickvibration

JF-Expert Member
Feb 7, 2017
3,227
5,132
Wanajamvi wenzangu nimejaribu saana kufatilia MEDIAS zetu hizi, kila kona watu hawaishi kuilalamikia serikali yetu na kutoa kila aina ya kashfa kwa Mh, Rais wetu JPM na serikali yake.

Hawajajitambua kila wanapoibeza hii serikali ya awamu ya 5 ndipo wanapozidi kumpa kiki JPM
 
Kuna kuwa na jina mara mbili mkuu, ukiwa unakosolewa na kukubali ulipokosea huwa ni sifa nzuri lakini ukiona unakosolewa kwa mabaya tu na hauelewi hiyo ni sifa mbaya. Hakuna binadamu anaependa sifa mbaya duniani kote ukiondoa wale viongozi wa drug cartel kule Mexico na Columbia.
 
Inawezekana kabisa hii mtazamo wako ukawakinyume chake thus why unaangaaika kurudisha kwenye uhalisia may be ndo maana kuna watu wanapigwa risasi ili kuiludisha mtazamo wako kwenye uhalisia wake
 



Uzezeta nao ni kipaji,hata wewe ukivua nguo na kutembea uchi barabarani utapata jina,je jina hilo utakuwa umelipata kwa mambo chanya au hasi?Unaweza ukawa maarufu hata kwa mambo maovu na jamii ikakufanya kuwa SI.Unit ya uovu!
 
Jina alishapewa na wazazi wake na kama umaarufu anao na hata ukizidi hausaidii lolote kwenye uongozi wake yeye ni Rais tayari. La msingi hilo jina unalosema anapewa ni baya au zuri?
 
Wakereketwa wake wangekua wavumilivu km critism zinampa umaarufu
 
Rais wa nchi hana jina, mpaka akosolewe ndo apate jina!?
 
Too irrelevant! Hivi mtu akikuelekeza au kukushauri juu ya njia unayopita kuwa haipitiki kakuongezea kick?
Ukosoaji chanya au hasi hukuamsha ili kukuincourage au kukudicourage juu ya kile unachokifanya na hukunyima sifa ukipuuzia au hukuongezea sifa ukizingatia but haukupi kick wala credits kwani utakuwa online of duty! Umeelewa somo?
Usikute umetumwa na yule jamaa wa tccra aliyekuwa anawafunda wale wazee jinsi ya kufunga midomo na vidole pamoja na macho yao yasione wala kusema lolote!?
 
Kwa maoni yako tunyamaze afanye madudu yake? Hilo haliwezekani, sina jeshi kama yeye ila nikipata wasaa japo mate nitamtemea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…