Amanikwenu
Senior Member
- Dec 1, 2009
- 187
- 0
Wote naamini tunakumba kuwa mwezi uliopita Rais Kikwete alizindua mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari Awamu ya Pili. Mpango huu unapatikana katika tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (www.moe.go.tz/documents). Kwa ujumla ni mpango mzuri japo kuna maeneo ambayo yanapaswa kuboresha zaidi na kutengewa fedha zaidi. Pamoja na malengo yaliyomo katika mpango huu nimeshangazwa sana na lengo kuwa, ufaulu wa Wasichana katika Hisabati umepangwa kuongezeka toka asilimia 16 (mwaka 2009) mpaka asilimia 25 (ifikapo mwaka 2015). Hapa maana yake ni kuwa bado tumepanga kuwa mpaka kufikia mwisho wa mwaka wa utekelezaji (2015) wa mpango huu Wasichana waendelee kufeli Hisabati kwa asilimia 75. Hii haingii akilini hata kidogo. Binafsi ningefikiri lengo lingekuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi yeyote atafeli somo la Hisabati na mengine ifikapo mwaka huo wa 2015. Hii inawezekana kabisa ni suala la kuamua na kutenda. Naamini Hisabati ndiyo somo rahisi kuliko yote na ndiyo somo ambalo ukiamua na kujituma una uhakika wa kupata alama ya A bila tatizo.